Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Karibu kwenye ufugaji ila gharama za chakula zinategemeana na sehemu ulipo ingekua vizuri ungeulizia sehemu ulipo bei za vyakulaWakuu husikia kichwa habari hapo juu nilikuwa naomba muongozo wa ufugaji kuku wa mayai.
Idadi kuku mia tano wa mayai bajeti yake ipoje hadi kutaga wazoefu nipe msaada.
Karibu kwenye ufugaji ila gharama za chakula zinategemeana na sehemu ulipo ingekua vizuri ungeulizia sehemu ulipo bei za vyakula
Kwa mradi wa kuku mayai, kuku mia tano ndo wenyewe haswaaa ila sasa ukitaka kufuga kwa faida kwa jamii ya sasa haina budi uwe na cages za kufugia kuku ndipo ambapo kuku watatoa mayai mengi kuliko kuwafuga chini
Ila ukitaka ushauri mzuri wa kuku nakupa no ya dokta huyu wasiliana nae atakufahamisha mengi kuhusu ufugaji
+255685561554 dr.Elisia
Ilikurahisisha zoezi lako la kupata makadirio gawanya gaharama zako katika makundi matatu au manne ukiona inafaa.apo ndioo mm natk nijue mtaji sh ngp had wanaanz kutag
Umempa picha ya kutosha.Ilikurahisisha zoezi lako la kupata makadirio gawanya gaharama zako katika makundi matatu au manne ukiona inafaa.
1. Miundombinu (hapa nazungumzia mabanda, vifaa vya kulia na kunywea maji, vifaa vya kutagia, vifaa vya kuwapatia joto vifaranga nk) mabanda inabidi uamue kama ni ya kukodi, unajenga ya kwako, unanunua cage nk. Unaweza kuulizia bei hizi katika eneo ulilopo ukapata kuchagua vizuri kulingana na mazingira yako
2. Gharama za chakula na madawa. Kwa uzoefu wangu mdogo kanuni ninatumia kanuni ya kuku mmoja kutumia chakula cha sh. 13,000 hadi 15,000 hadi kuanza kutaga. Kwenye madawa watakusaidia wataalam
3. Gharama nyingine za uendeshaji mradi mfano kumlipa kijana wa kazi, umeme, usafiri kuchukua chakula cha kuku, maji, bwana mifugo, ulinzi, nk.
4. Dharura. hii ni hiari kuiweka hua nachukua 5% hadi 10% ya jumla ya gharama za kipengele cha kwanza hadi 3 (ukubwa waproject ndio unaamua nitumie % ngapi) Hii imenisaidia hasa pale inapotokea jambo la muhimu ambalo nililisahau katika bajet yangu.
Naamini itakusaidia katika kufanya makadirio yanayoendana na mazingira uliopo
Kuanzia kuku 200 unahitaji mtaji wa 3M mpaka kuku watage kwaio apo utakua unazidisha ww mwenyewe kulingana na kuku unaotaka kufugaMtaji wao ni kama kiasi gani mpaka wanaanza kitaga chief...?
Hapo nimekupata vyema kabisa. Nashkuru...!Kuanzia kuku 200 unahitaji mtaji wa 3M mpaka kuku watage kwaio apo utakua unazidisha ww mwenyewe kulingana na kuku unaotaka kufuga
Nahisi umenielewa mkuu
Ndo ivo mkuu ukiwa na mtaji wa 6M unaanza na ufugaji wa kuku 500 na ndo vizuri kwa ufugaji wa kuku wa mayai ni bora ukaanza na kuku 500 angalau ndo utaona faida yakeHapo nimekupata vyema kabisa. Nashkuru...!
[emoji1488]
mkuu nakaa kitunda nimekuw kwenye ufugaji wakt nakua now ninafuga kuki wa nyama mia tatu ilaa nilitak ni move kufnya ufugaji wa kuku mayai ambao natajri kianzia mwez tisa kuhsu soko ninapokaa kitunda soko lipo na kuhs bei ya chakula cha layers mash stater grower na finisher najua kifup najua had kampun ganii napasw kuchukua interchick ilaa mm nilitak nijue niandae bajet ya sh ya kuwalisha yaan chakula cha kilog 50 napsw kuwa sh ngp had watimize izo week 20 wafike mda wa kutagaUmempa picha ya kutosha.
Lakini nina wasiwasi juu yake kama haya yatamsaidia.
Wasiwasi wangu ni kutokana na uvivu anaouonyesha hata katika kuomba msaada. Andiko lake tu linaonyesha kuwa huyu bwana ni mvivu, au ni mtu asiyekuwa makini na jambo analotafutia msaada.
Haelezi chochote kama anao uzoefu wowote wa kazi hiyo, au hata kuona wafugaji wengine katika eneo lake wanachofanya. Haelezi chochote amefikia hatua gani katika azma yake hiyo ya kutaka kuwa mfugaji, ili watu wanaotaka kumsaidia wajue wapi pa kuanzia ushauri wao.
Kiufupi ni kwamba, huyu bwana hana msisimko na kazi anayotaka kuifanya. Hata habari tu za soko kwake haimo kichwani mwake. Kaamua tu anataka kufuga kuku mia tano wa mayai, lakini hajui hata wapi pa kuanzia!
Anataka watu waanze ushauri wao toka A hadi Z, yeye yupo yupo tu hana hata kimoja anachojua?
Kazi yoyote inahitaji kutia nia na kuwa na moyo thabiti wa kuifanya kazi hiyo. Huyu haonyeshi kuwa yupo tayari kufuga. Akilazimisha, hata baada ya kupewa miongozo itakuwa ni hasara tupu kwake, na atalaani sana hata waliokuwa na nia ya dhati kumpa ushauri.
Unaona sasa?mkuu nakaa kitunda nimekuw kwenye ufugaji wakt nakua now ninafuga kuki wa nyama mia tatu ilaa nilitak ni move kufnya ufugaji wa kuku mayai ambao natajri kianzia mwez tisa kuhsu soko ninapokaa kitunda soko lipo na kuhs bei ya chakula cha layers mash stater grower na finisher najua kifup najua had kampun ganii napasw kuchukua interchick ilaa mm nilitak nijue niandae bajet ya sh ya kuwalisha yaan chakula cha kilog 50 napsw kuwa sh ngp had watimize izo week 20 wafike mda wa kutaga
lengo langu kuwa kuku zaid elf kumi miak mitano ijayo
sawa mkuu nafuatiriaa nitatoa mrejesho wang kilaa hatua nitayofk hadi sk nitimize kuku elf kumi kwa miak mitanoUnaona sasa?
Ulitakiwa uanze hivi mkuu na wenye kusaidia wangejua wapi pa kuanzia.
Kwa hiyo mabanda yapo, na unao uelewa mzuri wa kufuga kuku kwa ujumla bila kujali ni kuku wa aina gani.
Kwa hiyo ni kazi rahisi sasa kukupa makadirio.
Mimi nitakuchangia ifuatavyo:
1. Gharama za maandalizi ya kupokea vifaranga. Kufuatana na maelezo yako, hizi unazifahamu kutokana na uzoefu wako wa kufuga kuku wa nyama.
2. Kununua na Kulea vifaranga vya kuku wa mayai. Hapa pia gharama zake huwezi kushindwa kuzifahamu kutokana na uzoefu ulio nao. Tofauti tu ni kwenye bei ya vifaranga, ambayo unaijua kwa vile unajua utavipata wapi. Chakula cha hao vifaranga, Layer Starter, nayo sina shaka taarifa zake tayari unazo. Kwa mfano bei ya hicho chakula kwa mfuko, kama unajua wapi utapata chakula hicho, bei utaijua. Kiasi gani hao vifaranga watakula kwa siku, kwa wiki, pia utakuwa unajua kwa sababu hao vifaranga unajua ni wa aina gani, Hy-line Brown, au ISA Brown; kampuni watakupa hesabu ya chakula anachokula kifaranga wao. Kwa hiyo ni rahisi kujua gharama kwa muda utakaowalisha hicho chakula hao vifaranga; kama ni hadi wiki sita au wiki nane, ni rahisi kupiga mahesabu
3. Baada ya kulisha Layer Starter kwa wiki sita au nane, utawapa Layer Grower. Hiki chakula nacho kina bei yake kwa mfuko, ikitegemea unanunua wapi. Jumla ya chakula hicho watakachokula kwa siku utaijua kutokana na tarakimu utakayoipata toka kwa kampuni inayokuuzia hao kuku. Kwa hiyo gharama ya chakula kwa kila wiki wanayokula hao kuku itafahamika. Ni juu yako kupiga mahesabu kujua ni kiasi gani wanakula kwa wiki. Hiki chakula utawalisha hadi wiki ya 17/18 kabla hawajaanza kutaga. Hapa ndipo utakapopambana na gharama kubwa. Kuku wanakula,tuuu, lakini hawaingizi chochote. Hapa ndipo penye uzito hasa
4. Baada ya muda huo, ukitegemea wataanza kutaga kwenye wiki ya 20 na kuendelea, utawabadilishia chakula. Bei ya mfuko wa hiki chakula pia utapashwa kuijua toka kwa unayemwamini utengenezaji wake wa chakula. Ukijua bei, na unajua kila siku kuku mmoja anakula kiasi gani, utapata hesabu ya chakula kwa wiki na ukishajua hilo utajua gharama yake pia.
5. Kuna gharama za ziada, kama usafirishaji wa mahitaji kama hicho chakula kila unapokwenda kununua. Hizi hakuna yeyote anayeweza kukwambia ni kiasi gani, ni wewe mwenyewe utazijua, hasa kutokana na uzoefu ambao tayari unao.
6. Kuna uwezekano wako kujitengenezea chakula kama unao ujuzi wa kutosha. Kuna wanaodai unaweza kupunguza gharama kwa kufanya hivyo. Hili siyo rahisi, mtu asikudanganye. Utapunguza gharama na hapo hapo unapunguza ufanisi wa kuku wako wa mayai, ambayo ni hasara.
Kwa hiyo, nikufahamishe tu kwamba hakuna mtu atakayekupa mchanganuo sahihi wa gharama za ufugaji, nawe ukafuatiliza vile vile kama mwenzio ilivyomgharimu.
Chukua kalamu (siyo mimi), na karatasi, piga mahesabu upate makadirio yanayokuhusu wewe mwenyewe. Ni kazi nyepesi tu ya chini ya saa moja kuikamilisha.
Kabla ya hiyo "...elfu kumi..." weka mkazo wa mawazo yako kwa hao mia tano kwa sasa hivi. Hawa ndio watakaoamua kama hao "elfu kumi" wanawezekana.sawa mkuu nafuatiriaa nitatoa mrejesho wang kilaa hatua nitayofk hadi sk nitimize kuku elf kumi kwa miak mitano
sawa nimekuelew nitawek mchanganuo huoKabla ya hiyo "...elfu kumi..." weka mkazo wa mawazo yako kwa hao mia tano kwa sasa hivi. Hawa ndio watakaoamua kama hao "elfu kumi" wanawezekana.
Usifanye kazi Kiswahili. Hadithi ndeeeefu, kumbe hakuna kinachoendelea!
Hujaeleza chochote kuhusu hao wa "nyama", huenda ulipoanza huko hadithi zilikuwa hivi hivi!
Kwa sasa hivi ningekuona mtu wa maana sana na kukupa heshima stahiki kama ungeweka hapa mchanganuo wa hizo gharama za hao 500, baada ya kushika kalamu na karatasi kama nilivyokushauri hapo juu.
Lakini kwa haya maneno matupu unayoweka hapa, inanifanya kukutilia shaka sana kuhusu umakini wako.
Inanibidi nicheke tu mkuu 'mabestejr'!sawa nimekuelew nitawek mchanganuo huo