Naomba nipatiwe elimu kuhusu umaliziaji wa kujenga nyumba juu (Gypsum Board na PVC Board)

Mhakiki

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2012
Posts
2,385
Reaction score
2,101
Wakuu nisiwachoshe naomba nijikite kwenye mada.

Nina kibanda changu Cha vyumba vinne kimoji ni self, public toilet, sebule, dinning, jiko na stoo na Niko kwenye hatua ya finishing.

Naomba nipate Elimu kuhusu gypsum board aina zake, wazalishaji na ubora wake pamoja na bei zake za mjini(DSM).

Pia, naomba nipate Elimu kuhusu pvc board gharama zake zikoje kwa bei ya mjini DSM na wazalishaji wake na ubora wao.

Kuna tofauti Gani za ubora wa hizi materials tajwa hapo juu na udhaifu wake hasa kwa kuzilinganisha.

Natanguliza shukrani.
 

Mafundi Mko Wapi?

Njoo Huku

 
Nenda maduka tofauti uliza bei. Nyingi ni Kati ya 14,000-30,000. Brand ya Andika ndio bei ghali. Binafsi sioni tofauti yoyote.
 
Ina maana mtaani kwako hakuna mafundi? Au ulipenda tu kuja kutuzodoa hapa jukwaani kwamba nawe una ka kibanda? Tuheshimiane bro!😁😁
 
Nakushauri tu chukua yoyote yenye gharama nafuu, usitoboe mfuko sana kwenye hiyo sehemu ya gypsum maana iwe brand yoyote ikivujiwa na maji ni lazima eneo lililovujiwa ulibadilishe

Gypsum ni majina tu lakini ukifunga kama haijapata bughudha inaishi sana. Mie nimejenga nyumba kadhaa za wapangaji mwanzo nilikuwa naweka ANDIKA ila baadae nikawa naweka za bei nafuu ila zote zina mwonekano sawa na hazijawahi kusumbua. Hapo mchawi kuvujiwa tu
 
Haina manufaa yoyote hio thickness. Board haibebi uzito wowote. Uzito unabebwa na mbao.


Hapa naona watu wote watatu wana recommend yoyote ile, maana naona utofauti ni thickness yake labda na majina ya kampuni
 
Nakushauri utumie gypsum board instead of pvc (kwa dsm) pvc zinasharabu joto zaidi na kama nyumba yako fupi haina ac utajuta!
Board azitofautiani sana ila kuna za thailand (most expensive) na za tz! Kuna standard, bbg, andika, double elephant etc.
Hapo bbg ndio cheap zaid ila skushauri utumie kwa kuwa ni laini zaid ukiztoa 100 kkoo site zitafika nzima 90 na kwnye kuzikata znakatika vibya! Tumia double elephant kwa kkoo now znauzwa 15-16k
 
Wewe unawaza kama mimi tu. Zikishakaa pale juu hakuna tofauti yoyote. Hata zikivujiwa nene,nyembamba zinaharibika tu.
 
Jibu zuri sana la kiutaalam na uzoefu
 
Umemshauri vizuri naongeza nyama kidogo. Kwa sehemu ya nje kwenye fascia boards kwa chini huwa ndipo PVC hutumiwa. Gypsum boards kwa nje hazifai kutokana na unyevu na maji ya mvua. So atatumia zote pvc na gypsum, pvc kwa nje na gypsum kwa ndani.
 
Umemshauri vizuri naongeza nyama kidogo. Kwa sehemu ya nje kwenye fascia boards kwa chini huwa ndipo PVC hutumiwa. Gypsum boards kwa nje hazifai kutokana na unyevu na maji ya mvua. So atatumia zote pvc na gypsum, pvc kwa nje na gypsum kwa ndani.

Nlielewa kama anaomba ushauri kati ya pvc au gpysum coz kuna watu wanafunga pvc board ndani kbsaa achana na nje pale kwenye soffit. Pale ni kawaida kuweka pvc mkuu upo sahihi uwez kuweka board
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…