Naomba Ufafanuzi Kuhusu Biashara ya Hisa

Naomba Ufafanuzi Kuhusu Biashara ya Hisa

MiniActivist

Member
Joined
Dec 9, 2011
Posts
66
Reaction score
44
Biashara ya hisa inakuaje?
CWT wanauza hisa na ninahitaji kununua ila sina elim ya biashara hii.
 
Biashara ya hisa inakuaje?
CWT wanauza hisa na ninahitaji kununua ila sina elim ya biashara hii.

Okay Nisiwe Mchoyo..........

Tunaanza na Maana ya hisa (share).

Hisa ni vipande vidogo vidogo au cheti ambacho kinawakilisha umiliki wa kamapuni fulani. Hisa huwa zinatofautiana bei kutokana na kampuni inafanya shughuli gani na inapokelewaje Katika jamii.

MASOKO YA HISA.
Hisa unaweza kununua sehemu yoyote Duniani na baadhi ya masoko makubwa ni New York Stock Exchange (NYSE) Na London Stock Exchange (LSE). Hapa Tanzania tuna Secondary market ya hisa ambayo inaitwa Dar-es-salaam Stock Exchange (DSE) Ni moja kati ya Masoko Bora kabisa ya hisa Barani Afrika sina uhakika sana ila ina makampuni kama 21 hivi. Ambayo ni SIMBA,NMB,CRDB,TBL,TWIGA,MKOMBOZI bank,ACCASIA,TCC, na Mengineyo.....


HISA ZIPI MTU ANATAKIWA ANUNUE.
Malipo ya hisa yanategemea sana Shughuli katika soko na jamii tunayoishi hapo ndipo bei yake hupanda au kushuka. Mfano kampuni ya TBLmiaka mitatu nyuma hisa yake moja ilikua ikiuzwa hadi Tshs. 5000 lakini sasa hivi ipo kwenye Tshs.14,500 inapanda haraka sana hii inaonesha kuwa kampuni inafanya vizuri hivyo itakushawishi kununua hisa japo inahitaji Mtaji mkubwa...

Pia katika Mabenki Tunaona Benki ya N.M.B, CRDB na Mkombozi benki.Katika mambo ya Uwekezaji N.M.B iko vizuri zaidi ya CRDB. CRDB ina struggle sana hadi sasa inataka kuzidiwa hata na mkombozi bank ambayo imeanzishwa mwaka 2009 hisa zao walikua wakiuza Tshs. 300 lakini sasa hivi zipo kwenye 1200 wakati CRDB yenyewe ipo kwenye sh. 500 mara sh. 490 na kama nilivyosema awali bei ya hisa hupandishwa nashughuli katika soko kama hisa zinanunuliwa sana bei yake huongezeka na kama hazinunuliwi bei yake hudorora ambapo kwa mwekezeji unakuwa na hofu. Kwani kampuni yako inakua inafanya vibaya. Hivyo basi mwanahisa yoyote anapenda kuona hisa zikipanda bei ili apate Capital gain.


KIASI CHA UNUNUZI WA HISA / UWEKEZAJI

Hisa unazinunua kutokana na mtaji wako ulionao na kwenye makampuni Ukiwekeza Hela yako nyingi (ukinunua hisa nyingi) inamaanisha kuwa unamiliki kampuni kwa kiasi kikubwa hivyo unaweza kuwa kiongozi katika hiyo kampuni unaingia katika board of Directors na hapa unapata mshahara kwa mwezi.


FAIDA ZA HISA.
Hisa zinafaida za aina mbili yaani unaweza kupata gawio (Dividend) au ongezeko la mtaji (capital gain). Tunaanza na

Gawio hiki ni kiasi cha pesa ambacho huamuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ili kuwalipa wanahisha kutokana na Faida iliyopatiana kwa mwaka husika na hulipwa mara baada ya kulipa kodi (Corporate Tax 30%). Katika sheria ya Makapuni Companies Act ya mwaka 2002 haitoi ulazima wa kulipa gawio kwa wanahisa hivyo basi kulipwa gawio siyo lazima. Na hulipwa pale kampuni inapopata faida pia hiyo faida wanaweza kuilekezea kwenye mambo mengine ya uwekezaji.

Ongezeko la Mtaji Capital gain hii hutokea pale mwanahisa anapouza hisa zake. Mfano kama mwaka 2012 ulinunua hisa za TBL 500 Moja kwa Sh. 5,000 Sasa hivi 2015 unauza hisa za TBL 500 moja 1400 hapo kuna Capital gain ya Sh. 9000×500 =4.5Million ukijumlisha na Dividend unapata hela nyingi tuu kama uliwekeza mtaji mkubwa na mara nyingi hakunaga kodi.


Anayejua zaidi atujuze pia kama una swali uliza.
 
Last edited by a moderator:
Allen Snr

Ahsante sana mkuu umenipa somo ambalo mtu wa BED nisiyejua hata definition ya book keeping au commerce hakuna namna ningeipata. Swali; Je unanishauri nini nataka kuwekeza katika kampuni changa?
 
Last edited by a moderator:
Sasa Kama mtu wangu anamiliki hisa na Sasa anataka kurithisha hizo hisa inawezekana nikachukua hisa zote zilizopo ili nijiondoe kabisa? Tafadhali nijulishe
 
Sasa Kama mtu wangu anamiliki hisa na Sasa anataka kurithisha hizo hisa inawezekana nikachukua hisa zote zilizopo ili nijiondoe kabisa? Tafadhali nijulishe

Akirudi atatujulisha,
Pia unaweza kufungua hiyo link apo juu kujifunza zaid
 
Sasa Kama mtu wangu anamiliki hisa na Sasa anataka kurithisha hizo hisa inawezekana nikachukua hisa zote zilizopo ili nijiondoe kabisa? Tafadhali nijulishe

MKUU IKUMBUKWE KUWA HISA NI MALI (PROPERTY) HIVYO UNAWEZA KUIUZA ,KUMPA MTU KAMA ZAWADI N.K KAMA UNATAKA KUTOKA KWENYE HIYO KAMPUNI UNAUZA HISA ZAKO ZOTE NA KAMA UMEZEEKA UNAWEZA KURITHISHA WATOTO WAKO AU WAJUKUU NAKUMBUKA SECTION (78) of Companies Act (2002) inaelezea hayo mambo ya Transfer of shares pia Kampuni zimepewa nguvu kuna nyingine zinaweza kukataza mambo ya kurithishana hivyo inakubidi uziuze tuu!
 
Ahsante sana mkuu umenipa somo ambalo mtu wa BED nisiyejua hata definition ya book keeping au commerce hakuna namna ningeipata.

Swali; Je unanishauri nini nataka kuwekeza katika kampuni changa?

Ni vizuri kuwekeza katika kampuni mpya kwanza bei ya hisa inakua ipo chini lakini pia Ni risk kwa sababu inatakiwa ufanye utafiti sana ile kampuni jamii imeipokeaje, inavivutio gani katika uwekezaji Nampenda kutolea mfano TBL ukiona Castlelight& Lager watu wanazipenda sana kila ukienda kwenye bar na sherehe mbalimbali unazikuta hapo kimoyomoyo unawaza kuwa kampuni hii inafanya vizuri na uwezekano wa ku generate profit ni mkubwa hivyo utawekeza vilevile Kwenye kampuni Kama ACCASIA hii inamiliki migodi ya Dhahabu ya Buzwagi, Bulyankulu na Lyamungo kama unavyojua Dhahabu zinahitajika sana duniani na bei yake huwa haishuki hivyo Uwezekano wa kupata faida ni mkubwa..... Kwa kifupi kama unamtaji mkubwa nakushauri nenda kwenye kampuni Kubwa moja kwa moja. ili uweze kurudusha Faida mapema!
 
Ni vizuri kuwekeza katika kampuni mpya kwanza bei ya hisa inakua ipo chini lakini pia Ni risk kwa sababu inatakiwa ufanye utafiti sana ile kampuni jamii imeipokeaje, inavivutio gani katika uwekezaji Nampenda kutolea mfano TBL ukiona Castlelight& Lager watu wanazipenda sana kila ukienda kwenye bar na sherehe mbalimbali unazikuta hapo kimoyomoyo unawaza kuwa kampuni hii inafanya vizuri na uwezekano wa ku generate profit ni mkubwa hivyo utawekeza vilevile Kwenye kampuni Kama ACCASIA hii inamiliki migodi ya Dhahabu ya Buzwagi, Bulyankulu na Lyamungo kama unavyojua Dhahabu zinahitajika sana duniani na bei yake huwa haishuki hivyo Uwezekano wa kupata faida ni mkubwa..... Kwa kifupi kama unamtaji mkubwa nakushauri nenda kwenye kampuni Kubwa moja kwa moja. ili uweze kurudusha Faida mapema!

Mkuu Allen Snr,
Ahsante sana nimeelewa vizuri.
 
MKUU IKUMBUKWE KUWA HISA NI MALI (PROPERTY) HIVYO UNAWEZA KUIUZA ,KUMPA MTU KAMA ZAWADI N.K KAMA UNATAKA KUTOKA KWENYE HIYO KAMPUNI UNAUZA HISA ZAKO ZOTE NA KAMA UMEZEEKA UNAWEZA KURITHISHA WATOTO WAKO AU WAJUKUU NAKUMBUKA SECTION (78) of Companies Act (2002) inaelezea hayo mambo ya Transfer of shares pia Kampuni zimepewa nguvu kuna nyingine zinaweza kukataza mambo ya kurithishana hivyo inakubidi uziuze tuu!

Asante nimekuelewa,
 
Back
Top Bottom