Naomba ufafanuzi kuhusu marufuku ya matumizi ya US Dollar hapa ndani ya Nchi. Je US Dollar inaenda kuporoka kuanzia hiyo July 2024?

Naomba ufafanuzi kuhusu marufuku ya matumizi ya US Dollar hapa ndani ya Nchi. Je US Dollar inaenda kuporoka kuanzia hiyo July 2024?

Coffee

JF-Expert Member
Joined
Jul 16, 2017
Posts
1,304
Reaction score
1,312
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza ningependa kupata elimu kidogo kwa kinachowezekana kutokea kuanzia July mosi juu ya Dollar Vs Tshs. Naomba kuwasilisha.
 
Hahahaaaa

Linear thinking hii

Hatare sana
 
Masahihisho naomba isomeke Marufuku
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza ningependa kupata elimu kidogo kwa kinachowezekana kutokea kuanzia July mosi juu ya Dollar Vs Tshs. Naomba kuwasilisha.
Hata aliye andikiwa asome hayo ulio yasikia, sidhani kama alielewa alicho kitamka mazee...🤔
 
Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba ameelekeza kuanzia tarehe 1 Julai, 2024, Wadau wote wa ndani, Taasisi za umma, Wafanyabiashara, Asasi za kiraia, Mashirika ya kimataifa na Watu wote waliopo Nchini Tanzania wenye tabia ya kuweka bei kwenye huduma au kuuza bidhaa kwa fedha za kigeni, kuacha mara moja na kuhakikisha bei za bidhaa na huduma hizo zinatangazwa na kulipwa kwa Shilingi ya Tanzania.

Akiwasilisha Bajeti Kuu ya Serikali ya Mwaka wa Fedha 2024/2025 Bungeni Jijini Dodoma leo June 13,2024, Mwigulu amenukuliwa akisema “endapo una fedha za kigeni unatakiwa kuzibadilisha kupitia Benki au maduka halali ya kubadilishia fedha ndipo ufanye malipo kwa kutumia shilingi ya Tanzania, naielekeza Benki Kuu pamoja na vyombo vingine vinavyohusika kuendelea kudhibiti suala hili, kufuatilia kwa ukaribu ili kubaini wote wanaoendelea kufanya makosa hayo na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria, tunafanya kila malipo kwa fedha za kigeni, halafu shilingi ikishuka thamani tunajiuliza tumekosea wapi.

“Watanzania tunalikuza tatizo la upungufu wa dola kwa baadhi ya Watu kudai malipo au kufanya malipo ya bidhaa na huduma zinazotolewa ndani kwa kutumia fedha za kigeni yaani, dollarization, Taasisi ipo Tanzania na pengine hata Taasisi ya Serikali inamuuzia huduma Mtanzania inamwambia alipe kwa dola, Taasisi nyingine zinataka Mtu alipe ada kwa dola, alipe kodi ya nyumba kwa dola, vibali vya kazi, leseni na kadhalika kwa dola”

“Tunawafanya Watanzania wahangaike kuitafuta fedha ya kigeni kununua huduma zinazotolewa ndani ya Nchi yao badala ya kuwafanya Wageni wahangaike kuitafuta shilingi ya Tanzania wanapotaka huduma ndani ya Nchi, jambo hili linasababisha kuongezeka kwa mahitaji yasiyo ya lazima ya fedha za kigeni na kuwanyima fursa Watu wanaohitaji fedha za kigeni kwa ajili ya kulipia bidhaa na huduma muhimu kutoka nje ya Nchi, kitendo cha kuuza bidhaa au huduma za ndani kwa kutumia fedha za kigeni ni kosa kwa mujibu wa kifungu cha 26 cha sheria ya Benki kuu ya mwaka 2006 ambacho kinabainisha kwamba shilingi ya Tanzania ndiyo fedha halali pekee kwa malipo ya ndani ya Nchi"

“Aidha, nazielekeza taasisi zote za Serikali zinazotoza ushuru, ada na tozo mbalimbali kwa fedha za kigeni kurekebisha kanuni zao ili tozo hizo zilipwe kwa shilingi, hata Mgeni akija na fedha za kigeni ni vyema akaibadilisha kuwa fedha ya kitanzania ili aweze kupata huduma” ——— Dr. Mwigulu. #MillardAyoUPDATES
 
Marufuku ni kufanya malipo kwa Dollar,unapaswa kuibadilisha Dollar iwe kwenye TShs ndiyo ufanye malipo.
 
Ni fursa ya kufungua byuro di chenji huko US. Watalii wakitaka kuja TZ wanunue kwanza Shillingi yetu waje nayo
 
Mambo siyo mepesi namna hiyo, vinginevyo watu wangetengeza ukwasi wa kutisha kutokana na exchange rate , kwamba upandishe thamani ya Shilingi yako ndani ya wiki moja au mwezi mmoja tu kwa maelekezo ya kisiasa?

Sisi hatujawa na ubavu wa kufanya hivyo, labda huko Marekani na nchini nyingine tajiri, Trump katika utawale wake aliweza kufanya hivyo.

Ingekuwa rahisi hivyo nafikiri hata Zimbabwe wasingekuwa hapo walipo leo
 
POS za Mahoteli zinakusanya pesa za kigeni USD na Tshs kwa ku swap visa cards na kupeleka kwenye akaunti husika moja kwa moja NmB,NBC,CRDB,KCB,Stanbic bank nk je na zenyewe ni makosa tuelemishwe. Basi POS zote zifungwe upande wa usd ili zikusanye Ths tu.
 
Je tunaolipa usd za viza, hati za uhamiaji, viingilio TANAPA, Huduma za Mahoteli nk sheria ziangaliwe upya tuache au tuendelee kwa vile ni kuingiza dola kwenye mfumo halali wa uchumi na zinakatwa kodi kama mapato. fafanueni
 
Back
Top Bottom