Naomba ushauri kuhusu Mazda MPV

Mwasandube_

Member
Joined
Jan 31, 2022
Posts
22
Reaction score
33
Habari wadau! Katika pita pita zangu nimetokea kuipenda sana mazda mpv niwaza maybe siku za mbeleni walau na mimi niweze kuagiza.

Naomba ushauri kwa wanaoijua hii gari especially kwenye nyanja za ulaji wa mafuta,spare, management yake kwa maana ya service, matatizo common ya engine yake kama yapo.

Naomba kuwasilisha.





 
Kimuonekano

Ni gari zuri
Ila sijajua uimara wake kwa hapa kwetu ikiwa na maana jinsi gani mafundi wetu wanazimudu n.k
 
Mi ni fun wa mazda nimeshaimiliki hiyo gari , na kwa sasa nina mazda cx5, ni gari nzuri imara na himilivu sana kuanzia engine ,bodi imekqza sana kinachonifurahisha zaidi ni fuel consuption ,space ya ndani na coftability hii gari huwez kulinganisha na toyota wishi hata siku moja bro kama unafikiria kuagiza agiza tu ....vipuli vipo engine parts baadhi zinaangiliana na Toyota hata body parts ...karibu chama la wana mazda 4 life
 

Asante sana mkuu na shukuran kwa experience umetupatia
 

Mkuu nikusumbue tena naona hapa kuna za 2WD na 4WD je ipi ni best option? Na mafuta zinatofautiana sana ulaje wake?
 
Utawasikia mafundi wa kibongo, hiyo gari ina umeme mwingi....

Sijui walitaka badala ya umeme itumie kokoto?
 
Mkuu nikusumbue tena naona hapa kuna za 2WD na 4WD je ipi ni best option? Na mafuta zinatofautiana sana ulaje wake?
Kwa upande wa 2wd ina fuel consuption nzuri zaidi kuliko 4WD , ila inategemea na mazingira kama upo mazingira yenye milima sana na off road muda mwingi chagua yenye 4WD but consuption inashuka kidogo ...ila kwa ujumla ni gari nzuri sana [emoji106]
 
Utawasikia mafundi wa kibongo, hiyo gari ina umeme mwingi....

Sijui walitaka badala ya umeme itumie kokoto?
Magari ya kisasa yana umeme mwingi lengo ni kufanya efficience iwe nzuri zaidi na kutoipa engine kazi nyingi mfano ,kama feni ya rejeta ,water pump ,compresor ya Aic vinapotumia umeme engine inakuwa haina mzigo mkubwa ....hivyo inakupa consuption nzuri Tatizo mafundi bongo michosho sana wavivu kufikiria sana ...shule hawaendi wanataka watu wanunue magari wanayoweza wao huu ni uwenda wazimu
 
Kwa upande wa 2wd ina fuel consuption nzuri zaidi kuliko 4WD , ila inategemea na mazingira kama upo mazingira yenye milima sana na off road muda mwingi chagua yenye 4WD but consuption inashuka kidogo ...ila kwa ujumla ni gari nzuri sana [emoji106]

Shukrani limeisha hili
 
Kwa upande wa 2wd ina fuel consuption nzuri zaidi kuliko 4WD , ila inategemea na mazingira kama upo mazingira yenye milima sana na off road muda mwingi chagua yenye 4WD but consuption inashuka kidogo ...ila kwa ujumla ni gari nzuri sana [emoji106]
Mkuu Mazda kumbe inakula wese vzr
 
Mazda MPV iko vzr sana hutojuta, kitu pekee ambacho naweza sema kwa gar za siti 7 kwa space ya mizigo Ipsum iko vzr ila kama sio abt hiyo space ya mizigo MPV iko fresh na space ya kutosha kwa abiria lkn pia cku hz spare zipo za kutosha tu, ni ww tu. Karb chama la Mazda
 

Asante mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…