Usimfanyie hivyo, mpe muda andikishiana nae kwa mjumbe kwamba hadi kufikia let say Disemba mosi ulipe pesa yangu laa nitafunga chumba na nitazuia vitu vyako hadi hapo utakapokuja kulipa pesa yangu.
Exactly, Cha msingi hawezi ondoka na jengo lakoSawa kabisa mimi jamaa alishindwa kunilipa shg. 1,500,000/= . akahama na sikumdai mpaka leo. Nyumba ikapata mpangaji mwingine na maisha yanaendelea. Hakuna haja ya kugombana maana akihama nyumba ipo tu.
we acha tu mkuu, na ujenzi wenyewe ulivyo mgumu kipindi hikiHakuna Cha kuachana nae mkazie tu kwa namna yoyote. Ujenzi ata Kama ni banda unapasua vichwa. Makazie kabisaa mkuu
Kuna namna labda alishaedit,itakua ni jambo zuri maana nilistaajabishwa mno na swali lakoKumbe kweli mkuu. Huyu katuingiza Mjini Magharibi
Tehteh....kama kuna kaukweli flani hivi ndani yakeAlinunuliwa bia
Kuna jamaa yangu alipanga nyumba akakutana na mpangaji mtata ,miezi 6 ikapita bado anakwepa kulipa,akamwambia ondoka bado anasema ili niondoke lazima unipe notice . Mwenye nyumba alichofanya ni kumwita mjumbe mbele ya jamaa akasema nataka kurepair nyumba yangu aondoke ,mafundi wakaanza kutoa bati,chumba ikawa wazi kwa juu halafu akaacha hapo hapo ,mvua ikija au jua likiwaka watajua wenyewe au akiibiwa atajijua ..mbona aliondoka mwenyewe
Ni rahisi kusema hivyo.Pia wapangaji wengi ukimuachia mda mrefu labda mwaka au miezi 6.Siku akizipata pesa utoroka uona bora akapange kwingine kuliko kulipa deni.Dah sema wenye nyumba wanakuwaga wababe sana huwa wanaona wameyapatia maisha. Halafu watoto wao wakina kuwa wakubwa wanapitia madhila Yale Yale waliyopitia wapangaji wao. Kama unaweza msamehe tu nyumba hayiami utapata mpangaji mwingine.
Akifanya hivyo atakuta chumba kitupu mkuuUsimfanyie hivyo, mpe muda andikishiana nae kwa mjumbe kwamba hadi kufikia let say Disemba mosi ulipe pesa yangu laa nitafunga chumba na nitazuia vitu vyako hadi hapo utakapokuja kulipa pesa yangu.
Ngojea nijaribu kufanya hivyo boss,japo nipo mbali nae,hofu yangu hasije kuhama usiku
Akifanya hivyo atakuta chumba kitupu mkuu
Mwachie bill za umeme awe analipa yeye hadi pale pesa yako itakapoisha.Wakuu habari:
Unajua hizi nyumba za kupangisha zina matatizo Sana,mtu umetumia pesa kibao kuwekeza,Bado Tena unakuja kupangisha majitu ambayo hayajielewi.
Ni hivi, Kuna mpangaji wangu now anakaribia miaka miwili kama na nusu kwenye mabanda yangu, Sasa huyu tangu kipindi cha Corona ya kwanza hile mambo yake hayajakaa sawa, nilikuwa namdai milioni , alilipa laki nne Bado laki sita, Sasa saundi zimekuwa nyingi, mara subiri kidogo, mara week ijayo, mara mwisho wa mwezi ,
Sasa nilichofikiria huyu bwana mdogo labda nikuzuia vitu vyake vyote,na kufunga nyumba Hadi hapo atakaponilipa pesa yangu,
Sasa je nikiwa na mjumbe siinatosha kiushaidi kwenda kumtimua hili nifunge nyumba Hadi atakapolipa Deni!!?
Au wazee wenzangu mwashaurije katika hili, maana sitaki kutumia ubabe sheria itanibana
Ila we jamaa una roho ngumu kumdai pesa mtu anaumwa looh,Ni heri tu ahame atafute mpangaji mwengine amlipe kodi.
Nakumbuka nishakuwaga na Mpangaji akapata changamoto ya ugonjwa alikonda jamaa hadi kitaa wakawa wananiambia yule mpangaji wako ameungua.
Jamaa alichoka kazi zake zikakwama mke wake akaondoka na vitu Kama vyote akaenda kwao.
Kodi yake ilipoisha akawa hana uwezo wa kulipa, ukapita mwezi wa 1,2,3 ananipiga sound ila nilikuwa na Mimi namuonea huruma flani kodi yake ilikuwa laki 2 kwa mwezi.
Nikaona isiwe tabu nikampeleka kwa Mtendaji wa Mtaa, akaitwa kwa barua tukaenda jamaa akasema hayupo vizuri na pia ni mgonjwa ,kaenda hospital I ugonjwa hauonekani.
Dah unaambiwa alikuwa anatia huruma.
Mtendaji akamwandika notisi ya mwezi ahame na anilipe kodi anazodaiwa au alipe kodi Kama kawaida ya miezi 6.
Mwezi wa notisi ukaisha jamaa hana kitu nikaenda kumripoti kwa Mtendaji ,Mtendaji mwenyewe akawa anamuonea huruma jinsi anavyoumwa yaani we acha .
Dunia Ina majaribu Sana, Mtendaji anamkoromea jamaa anamwambia kesho nakuja na mgambo kukutoa kwenye hiyo nyumba jamaa anabaki analia , anaambiwa haya nenda kesho ujiandae tunakuja kukutoa.
Mtendaji ananiambia nibaki ,Mtendaji ananiambia nimsikilizie jamaa ni mgonjwa akija kumtoa anaweza asieleweke na jamii. Na Mimi nikawa namkubalia tumsikilizie ikawa ndio hivyo had ikafika miezi 4 Mtendaji anasita kumtoa.
Kuna siku na hasira zangu nikapiga zangu konyagi za kutosha nikasema wacha nikamtoe yule Mpangaji Mimi mwenyewe Mtendaji anazingua.
Nikaenda pale kwangu had I anapoishi nasikia ndani jamaa anakohoa kugonga anauliza wewe nani namjibu mwenyewe nyumba ananiambia ingia ndani.
Dah kuingia ndani nikakuta jamaa alikuwa anatapika kishenzi ndani ya ndoo nyumba chafu jamaa anakitanda nagodoro tu nikamwambia we jamaa unataka kufia hapa kwangu nini. Halafu na kodi hulipi unataka kunipa mzigo nini.
Unaambiwa jamaa akawa analia akaniomba nauli aende kijijini kwao.
Nikashikwa na huruma nikampa elfu hamsini nikamwambia na kodi yangu nimekusamehe .
Kweli jamaa kesho yake tu akatoa vitu vyake akataka kuviuza akakosa mteja akasepa akaviacha nje.
Ikabidi niviweke stoo vitu vyake nikapiga rangi nyumba nikapangisha mtu mwingine.
Baada ya Kama mwaka jamaa alikuja kunisalimia Bahati nzuri akanikuta alikuwa amenawiri amepona yupo fresh,
Aliniambia alivyokwenda kijijini kwao ikaonekana alikuwa ametupiwa majini na ndugu yake hivyo wakamfanyia matibabu akapona.
Jamaa alinishukuru Sana akaniambia amekuja kunilipa kodi niliyokuwa na mdai Yaani bila kutegemea nikala laki nane.
jamaa hadI Leo rafiki yangu.
Kwenye haya maisha kuna watu wanapitia mitihani mikubwa Sana si vyema kumcheka,kumdharau au kumnyanyasa mtu ni swala la kumshukuru Mungu kila wakati Kama amekujalia kuepukana na dhiki ,karaha, na magonjwa.
[emoji3][emoji3] alikuwa mhindi nini??Mbabe wa kijenge yeye alikua hataki Kodi ya miezi 3,ye kila mwisho wa mwezi anakuja na baunsa wake mida ya jioni.Huna Kodi anaondoka na mlango wa nyumba.Ukienda kulipa Kodi yake ndipo utaondoka na mlango wako.