Naomba Ushauri:Namna ya Kuhamisha Kesi

Naomba Ushauri:Namna ya Kuhamisha Kesi

Head teacher

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2012
Posts
1,796
Reaction score
412
Kuna ndugu yangu anasota mahabusu, tulishindwa kumwekea dhamana Mahakama ya mwanzo baada ya hakimu kuweka masharti magumu ya dhamana. Tuna mashaka na mwenendo wa kesi ya ndugu yetu katika mahakama hii, polisi wanakandamiza dhamana isitolewe kirahisi. Hivyo basi tuna mpango wa kuhamisha kesi iende mahakama ya wilaya. Je kuna taratibu ganiza kufuata ikiwa hatutaki kuweka wakili. Asanteni
 
ninakushauri, kwa njia rahisi ambayo mahakama haitakuwa na jinsi ila kufanya ombi lako, utafute wakili wa kujitegemea, aandike barua kuwa anaata kukuwakilisha mahakamani, sasa mawakili wa kujitegemea do not appear in Primary courts, hivyo unataka kuhamisha kesi yako toka primary court ambako mawakili hawafanyi kazi ili iende district ambako mawakili huwa wana appear. kwa njia hii, mambo yataenda haraka, la sivyo ukiwa unachelewa, maamuzi yanaweza kufanywa haraka juu ya kesi yako ili ukandamizwe kama wakistuka kuwa unataka kuhamisha kesi. hii ni njia ya haraka na nyepesi ambayo nimeona watu wanatumia. kuna njia nyingine ambazo siwezi kukuambia kwasababu huwa sio productive sana kwasababu mahakama za mwanzo mara nyingi huwa zinaweza kutumiwa vibaya sana na watu wenye pesa waka delay au kusambaratisha haki ya mtu chapchap hasa pale wanapoona unataka kuwawahi. huwezi amini, kuna baadhi ya mahakama za mwanzo nilishawahi kufanya uchunguzi, hata kesi za jinai za watoto zinafikishwa mahakama za mwanzo bila hata kupitia polisi, na zikifika pale mahakama ya mwanzo, wanaiharakisha mno na kumfunga (uchunguzi ulipofanyika ilionekana kuna wazazi wengine wana ugomvi wa kifamilia, hivyo anabambika kesi halafu anaenda kumhonga hakimu wa mahakama za mwanzo anaendesha kesi haraka kambla hujatulia ameshamfunga mtoto yule au mtu mzima yule)....tulienda polisi, polisi nao wanashangaa kwasababu wamekuwa bypassed. kati ya vitu vinavyotakiwa kufanyiwa restructuring hapa Tanzania ni mahakama za mwanzo. ni kichaka kibaya sana (i am sory to say this).

bofya hapa kujua haki zako SHERIA KWA KISWAHILI

View attachment 104675

View attachment 104676View attachment 104676
 
ninakushauri, kwa njia rahisi ambayo mahakama haitakuwa na jinsi ila kufanya ombi lako, utafute wakili wa kujitegemea, aandike barua kuwa anaata kukuwakilisha mahakamani, sasa mawakili wa kujitegemea do not appear in Primary courts, hivyo unataka kuhamisha kesi yako toka primary court ambako mawakili hawafanyi kazi ili iende district ambako mawakili huwa wana appear. kwa njia hii, mambo yataenda haraka, la sivyo ukiwa unachelewa, maamuzi yanaweza kufanywa haraka juu ya kesi yako ili ukandamizwe kama wakistuka kuwa unataka kuhamisha kesi. hii ni njia ya haraka na nyepesi ambayo nimeona watu wanatumia. kuna njia nyingine ambazo siwezi kukuambia kwasababu huwa sio productive sana kwasababu mahakama za mwanzo mara nyingi huwa zinaweza kutumiwa vibaya sana na watu wenye pesa waka delay au kusambaratisha haki ya mtu chapchap hasa pale wanapoona unataka kuwawahi. huwezi amini, kuna baadhi ya mahakama za mwanzo nilishawahi kufanya uchunguzi, hata kesi za jinai za watoto zinafikishwa mahakama za mwanzo bila hata kupitia polisi, na zikifika pale mahakama ya mwanzo, wanaiharakisha mno na kumfunga (uchunguzi ulipofanyika ilionekana kuna wazazi wengine wana ugomvi wa kifamilia, hivyo anabambika kesi halafu anaenda kumhonga hakimu wa mahakama za mwanzo anaendesha kesi haraka kambla hujatulia ameshamfunga mtoto yule au mtu mzima yule)....tulienda polisi, polisi nao wanashangaa kwasababu wamekuwa bypassed. kati ya vitu vinavyotakiwa kufanyiwa restructuring hapa Tanzania ni mahakama za mwanzo. ni kichaka kibaya sana (i am sory to say this).

bofya hapa kujua haki zako SHERIA KWA KISWAHILI

View attachment 104675

View attachment 104676View attachment 104676
Asante sana, huenda hakimu anataka kuiendesha haraka haraka, maana kesi ametaja tena baada ya siku mbili za kazi ili tukose mudawa kuhamisha kesi.
 
Kuna ndugu yangu anasota mahabusu, tulishindwa kumwekea dhamana Mahakama ya mwanzo baada ya hakimu kuweka masharti magumu ya dhamana. Tuna mashaka na mwenendo wa kesi ya ndugu yetu katika mahakama hii, polisi wanakandamiza dhamana isitolewe kirahisi. Hivyo basi tuna mpango wa kuhamisha kesi iende mahakama ya wilaya. Je kuna taratibu ganiza kufuata ikiwa hatutaki kuweka wakili. Asanteni

Dhamana ni haki yako kikatiba lazima upate kama shauri lako lina dhamana, lakini ifahamike dhamana huja na masharti yake, je wewe umepewa masharti gani hayo ambayo unahisi hayatimiziki, maana masharti ya dhamana ni kwa mujibu wa sharia, pengine husifikiri kushindwa kwako kutimiza masharti ya dhamana ndio kisingizio cha kusema umeonewa.
Swala la kuhamisha shauri sidhani kama linawezekana kirahisi ka unavyofikiri, kama mahakama ina mamlaka ya kusikiliza kesi yako ni kinyume cha sheria kuruka mahakama moja yenye mamlaka na kwenda mahakama ya juu labda kama kuna swala la kisheria limeibuka linatakiwa kutolewa ufafanuzi na mahakama za juu, kusema unaweza andika barua mahakama kwamba unaomba shauri lako liamishiwe mahakama ya juu ili uweke wakili sidahani ka ombi lako linaweza fanikiwa maana kuna hukumu ka sikosei ya mahakama kuu (I stand to be corrected) ilishawai toa msimamo kwamba.."sababu ya kutaka kuweka wakili haiwezi simama kama kigezo cha kuamisha shauli toka mahakama ya mwanzo kwenda mahakama ya juu"
ushauri wangu kama kabisa umejiridhisha na unaamini hakimu anasikiliza shauli la huyo ndugu yako ananyimwa haki yake ya msingi ya kikatiba ya kupata dhamana kwa njia zisizo halali (rushwa) basi unawezafanya yafutayo:
1. Nenda kwa msajili wa mahakama utoe malalamiko yako na kuomba ubaridishiwe hakimu au
2. unaweza omba revision (mapitio) ya maombi yako dhamana katika mahakama ya wilaya
 
Back
Top Bottom