Naomba ushauri: Nataka niwaunganishe wauzaji na wanunuaji wa mazao na mifugo kwa njia ya mtandao

Naomba ushauri: Nataka niwaunganishe wauzaji na wanunuaji wa mazao na mifugo kwa njia ya mtandao

Habari wana JF

Nina wazo moja la biashara ambalo naomba ushauri. Wazo langu ni hili nataka niwaunganishe wauzaji na wanunuaji wa mazao na mifugo kwa njia ya mtandao. Nina uelewa na Blogs hivyo nitaifungua blog ambayo ndo itakua kama soko la mtandaoni.

Hapa mkulima au mfanyabiashara atabofya kipengelewe cha kutangaziwa mazao yake kisha atajaza details zote ambazo ataulizwa kujaza kisha taarifa zake nitazipokea mm na kisha nitaweka tangazo la mazao yake na mawasiliano yake ili wanunuaji wamtafute.

Hakuna ununuaji mtandaoni lakin lengo la blog hii litakua kuwakutanisha tuu wauzaji na wanunuaji kisha wataanza kuwasiliana kwa ajili ya biashara.

Sasa kuhusu mimi kufaidika na biashara hii ni kwamba, mwanzo mfumo huu utaanza kwa free kabisa mpaka nitakapofikisha wauzaji wengi na wanunuaji wengi kuitembelea blog na tayari ntakua nafanya survey kwa wauzaji kama kweli wanapata wateja kupitia mfumo huu wa mazao online,

Hapo ndipo nitaweka ada fulani ambayo muuzaji atailipa kama ada ya membership katika mfumo huu kwa muda flan ambayo ni affordable ili awe anatangaziwa mazao yake bila shida yoyote na kwa wale ambao wao watakua temporal tuu labda alikua anauza mara moja tuu hawa nao pia watalipia kiasi flani tuu kidogo, na pia kutakua na offer flani kwa member ambao ndo wanaanza wakishaona mfumo unafaa nao watalipa membership cost.

Kwa upande wa mtaji , Skills za mambo ya mtandao ninazo na kingine labda ni kulipia domain name ya blog ili iwe ni rahisi watu kuisearch na vyote hivo vipo chini ya uwezo wangu. Naombeni ushauri juu ya wazo hili la biashara kipi kifanyike iwe nzurii zaid au kipi kitolewe.

Karibuni wote.
@computerengineer
Umefikia wap
 
Wazo zuri sana !!! Changamoto utakayokutana nayo ni kwamba wakulima walio wengi hawajaelewa matumizi ya Internet !!! Lakini waweza kuanza taratibu na wazo lako likafanikiwa !!!
Wakulima gani hao unaowazungumzia ambao hawajui matumizi ya internet!
 
Kwa wazo lako hilo hakikisha unafanya promotion nje ya mtandao mana ndiko wakulima wapo
Inabidi uwatafute kwanza wakulima waweze kupost bidhaa zao kabla ya wanunuzi
lakini pia sijui wewe utakuja na kitu gani cha kitofauti kitachowapa faida wakulima mana hawa wakulima wengi hivi vitu vya kuuza bidhaa mtandaoni bado kwahiyo unakazi yakuwabadilisha watu
 
Maswali ya kujiuliza kabla ya kujikita kwenye IDEA yako kwa 100%:
1. Je kuna hali ya ucheleeshwaji katika malipo kwa wakulima na wafugaji?
2. Je madalali wanachukua % ngap wakishauza mazao au mifugo?
3. Je gharama ya usharishaji wa mazao au mifugo inawagharimu sh ngap wakulima na wafugaji kupeleka soko husika?
4. Ni changamoto gani kubwa inayowakabili wakulima na wafugaji ukiachana na maswali 1, 2, 3 hapo juu.
 
Nimeona Lakin Mmetoa Bei tuu za mazao katika market mbalimbali za mwanza, Lipitie wazo langu vizuri ulielewe mkuu
Yaani mkuu jinsi unavyoielezea hiyo biashara yako utafikiri sijui ni very unique idea ambayo no one had ever implemented. Sikia idea yako sio mpya ni idea ambazo hata hapa tz tayari kuna watu washaanza kufanya na tayari naweza sema ni biashara yenye competitors tayar so labda cha kufanya ni wewe kuleta utofauti wako katika hiyo site yako lakini in short hii ni E-commerce km zlivyo ecommerce zingine zozote utofauti ni kua hii ime base kwny agriculture industry. Kila la heri mkuu ukihitaji wataalam wa kilimo tupo!
 
Habari wana JF

@computerengineer
kitu kikubwa unatakiwa kutenga mda kidogo kufanya utafiti na pengine hata kuwatembelea hawa wakulima na wafugaji kuelewa mazingira yao. Mfano unaweza kufanya assumotions kwamba wana access na internet kumbe ukifika unakuta ni basic phone. Pia kuwatembelea unaweza kujua jinsi wanavyozitumia simu zao kwenye biashara yao ya kilimo ua ufungaji. Kwa kufanya hivyo utapata picha halisi ya wapi uanzie.
 
tekno zimesharahishisha sana mkuu mtu ana tecno ya elfu hamsini na anashinda facebook kama kawaida. matter ni kufanya system hii ifahamike kwa watu weng mpaka vijijin huko kwa sabab haitakua system complicated kias kwamba mpaka mtu awe na smart phone tuu pekee ake hapana ni blog ambayo anaweza kuiaccess hata kama ni sim ga kawaida. So i will make sure wakulima wanaielewa so hapo mrketing and advatisement strategies ndo zitatumika kuhakikisha inakua exposed to the community
suala la penetration ya smartphone si kweli. Mjini tu bado watu wengi bado wanatumia basic feature phone. Na pia adoption ya smartphone inategemana na umri na elimu. Ukitaka kujua bado ni ndogo anza na madereva wa boda boda au mama Ntilie. Utajua smartphone si kila mtu anayo. Mimi ni mtaalamu wa Technology For Development kwa hiyo naelewa hali halisi. Kuna mtu amaetengeneza portal inaitwa nauza.co.tz. Alichofanya ni kwamba ameintegrate USSD na Web na nadhani amewaza kuhusu changamoto ya wakulima wengi kutokuwa na smartphone. Hii ni idea nafikiri imekuwa funded na Data For Local Impact Innovation Challenge.
 
suala la penetration ya smartphone si kweli. Mjini tu bado watu wengi bado wanatumia basic feature phone. Na pia adoption ya smartphone inategemana na umri na elimu. Ukitaka kujua bado ni ndogo anza na madereva wa boda boda au mama Ntilie. Utajua smartphone si kila mtu anayo. Mimi ni mtaalamu wa Technology For Development kwa hiyo naelewa hali halisi. Kuna mtu amaetengeneza portal inaitwa nauza.co.tz. Alichofanya ni kwamba ameintegrate USSD na Web na nadhani amewaza kuhusu changamoto ya wakulima wengi kutokuwa na smartphone. Hii ni idea nafikiri imekuwa funded na Data For Local Impact Innovation Challenge.

nauza .co .tz mbona haipo online
 
Habari wana JF

Nina wazo moja la biashara ambalo naomba ushauri. Wazo langu ni hili nataka niwaunganishe wauzaji na wanunuaji wa mazao na mifugo kwa njia ya mtandao. Nina uelewa na Blogs hivyo nitaifungua blog ambayo ndo itakua kama soko la mtandaoni.

Hapa mkulima au mfanyabiashara atabofya kipengelewe cha kutangaziwa mazao yake kisha atajaza details zote ambazo ataulizwa kujaza kisha taarifa zake nitazipokea mm na kisha nitaweka tangazo la mazao yake na mawasiliano yake ili wanunuaji wamtafute.

Hakuna ununuaji mtandaoni lakin lengo la blog hii litakua kuwakutanisha tuu wauzaji na wanunuaji kisha wataanza kuwasiliana kwa ajili ya biashara.

Sasa kuhusu mimi kufaidika na biashara hii ni kwamba, mwanzo mfumo huu utaanza kwa free kabisa mpaka nitakapofikisha wauzaji wengi na wanunuaji wengi kuitembelea blog na tayari ntakua nafanya survey kwa wauzaji kama kweli wanapata wateja kupitia mfumo huu wa mazao online,

Hapo ndipo nitaweka ada fulani ambayo muuzaji atailipa kama ada ya membership katika mfumo huu kwa muda flan ambayo ni affordable ili awe anatangaziwa mazao yake bila shida yoyote na kwa wale ambao wao watakua temporal tuu labda alikua anauza mara moja tuu hawa nao pia watalipia kiasi flani tuu kidogo, na pia kutakua na offer flani kwa member ambao ndo wanaanza wakishaona mfumo unafaa nao watalipa membership cost.

Kwa upande wa mtaji , Skills za mambo ya mtandao ninazo na kingine labda ni kulipia domain name ya blog ili iwe ni rahisi watu kuisearch na vyote hivo vipo chini ya uwezo wangu. Naombeni ushauri juu ya wazo hili la biashara kipi kifanyike iwe nzurii zaid au kipi kitolewe.

Karibuni wote.
@computerengineer
GREAT IDEA MY BRO, i think we can do something together tho on a large scale,i wish we had such people like you with such ideas, this world is moving very fast an E-COMMERCE and digital world are becaming king,
 
Idea iko vizuri...
Ila walau ukitaka ku present Idea yako usiifanye Open Kiivyo. Niliwwhi present Idea fulan zaman, kwenye forum ya njee kuomba ushauri kama wewe ulivyofanya..Rafiki yangu ali execute faster, Na anaimiliki....

Ikitokea umeandika humu kwa detail maybe You Have Nothing to loose
Idea is only 20 percent...Execution ndo ina matter. Kwa hiyo if you think your idea is innovative enough, it will be hard for people to copy it.
 
Back
Top Bottom