Naomba ushauri: Natamani kuanzisha bishara ya jumla

Naomba ushauri: Natamani kuanzisha bishara ya jumla

Nimekua katika biashara ya mafuta. Biashara ya mafuta ni nzuri ila sasa hivi imekosa mzunguko ikichangiwa na kupanda vitu bei. Biashara ya mafuta kikawaida kila dumu la litre 20 faida haizidi 5k kama upatikanaji wa mafuta huko sahihi sokoni.

Ili mafuta yakupe wafaida unatakiwa ununue inbulk ambapo changamoto ndio inaanza hapo.

Ntakupa mfano umeenda kununua pale korie, wale bila kununua gari ya ndoo 800 hawatoi semi yao kukuletea. Nafikiri ukiitaji pungufu ya hapo itabidi ununue kwa msambazaji wakuu.

Kipindi tunafanya biashara hii tulikua tunaweza kununua dumu la lita 20 hadi 25k miaka iyo kumaanisha kwa mtaji wa million 40 ulikua unauwezo wa kununua dumu 1600. Mfano pia mwaka jana dumu lilikua linauza 70- 80 na kitu kwa mtaji wa million 40 unapata mafuta 500 na kitu. Sasa mafuta yanasomeka 100plus kwa mtaji wa million 40 unapata ndoo 400.

Ni biashara ambayo kila msimu wa mafuta unapoanza mafuta yanapanda bei hii inapelekea mtaji kukua kwa ukwasi faida italiwa na mtaji. Ili ufanye kwa nguvu na raha inakuitaji mtaji mkubwa walau million 100 Kuuza jumla

Kila bei inapopanda inapunguza purchasing power kwa wateja wako. Mfano alikua anatumia million kununua ndoo 10 akikuta zimepanda atatumia million kununua ndoo 8

Bulk sellers wapo kuna kiwanda cha korie pale vingunguti, kuna supplies tu wakubwa hasa wahindi.

Leseni ni kawaida kwa mafuta utaitaji leseni halamshauri, TIN, VAT registration maana mafuta yanamauzo makubwa, Fire watapiga kusumbua, na watu wa chakula na dawa.

Biashara ya kuoanisha na mafuta ni chumvi na sukari.

Faida ipo ndio maana watu wanaendelea kufanya.

Ata sijui naandika nini ila naandika mengi mengi. Utauliza vingine kwa msaada zaidi
Mkuu, nakushukuru sana, Hakika umenifungua sana, Mungu akubariki
 
Mimi naona ungeuza bidhaa za majumbani mchanganyiko usibase kwenye biadhaa moja tu.
Mfano sukari,mafuta,sabuni,dawa za mswaki,majani ya chai,juice,ngano,mchele n.k.
Halafu unakuwa unawauzia jumla na mtu akitaka rejareja pia unamuuzia nadhani itakupatia wateja sana mfano sukari wewe hutopima robo wala nusu unaanzia kg 1.
Hapo utapata wateja wa jumla na rejareja pia.
Kuhusu wapi pa kupatia bidhaa wajuzi watakujuza.Sio mwenyejinwa huko hivo sijui.
Pia huwa naona kama unachukua mzigo mkubwa Kuna makampuni yanakuletea mpaka dukani mfano dawa za mswaki na bidhaa nyingine.
Hapa sasa kama sehemu fremu ilipo maduka ya rejareja yapo mbali kidogo au sehemu ambayo kuna mzunguko wa watu wengi pia mfanyabiashara wa rejareja anaweza kununua bidhaa kwa urahisi bila usumbufu wa kuzifuata mjini hasa kama mzigo anaoutaka ni mdogo tuseme ameishiwa mfano sabuni ya unga ambayo inauzwa 15000 kuzifuata mjini ni mbali plus gharama ya usafiri hivo itampasa kuichukulia kwako ambapo unaweza kumuuzia 15500 au 1600.
Nadhani pia leseni yake unalipia kama unavyolipa duka la rejareja.Namaanisha gharama zinafanana.Kama nakosea wajuvi watanirekebisha.
Kuhusu TRA sijui.
Kila la kheri ndugu.


Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
Mkuu, asante sana kwa ushauri
 
Back
Top Bottom