Naomba ushauri: ukifiwa, unavukaje maumivu na kusonga mbele na maisha?

Mshangazi dot com

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
1,345
Reaction score
3,503
Rafiki yangu amefiwa na mama mzazi na mdogo wake siku moja kwenye ajali. Anaumia sana, imepita wiki sasa, ila bado analia kila siku na kuongea peke yake mpaka tunaogopa.

Kama umeshawahi kufiwa na mtu wa karibu, nini kilikusaidia kutuliza maumivu na kuweza kusonga mbele?


 
Sito danganya, mwacheni alie ili maumivu na uchungu umtoke.

Maana uchungu wa kupoteza watu wa karibu, ana uelewa yule anae pitia maumivu hayo.

Kikubwa tafuta mtu mzima aliye shika dini ya muhusika, au mwenye utu na akili.
ajaribu kumpa nasaha ili amrudishe katika utimamu wake.
kidogo kidogo, ata jirudi

ZIngatia, Kama wali kuwa Wana kaa nyumba Moja, basi mtoeni hapo haraka maana ni Kama ana ziona kumbukumbu.
ZITAKAZO zidi kumchoma.
 
Hili jambo halinaga uzoefu .............maumivu yake hata huwa hayasimuliki kabisa............da nimekumbuka kwa mshua ...........baba mungu naomba uendelee kumuweka salama kamanda dingi.........
 
 
Anapitia kipindi kigumu. Mungu amtie nguvu na kumpa faraja. Anaishi mkoa gani... Wana JF tukamtembelee
 
Mwambie hivi,

Yupo mfariji,

Yupo baba wa yatima na wajane,

Yupo mshauri wa Kweli,

Yupo mfalme wa Amani,

Yupo baba wa milele,

Na huyo ni Yesu Kristo/YESHUA HAMASHIACH.

Mungu ni MMOJA na YESU KRISTO/YESHUA HAMASHIACH ndilo JINA lake. Amen
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…