Naomba ushauri wa kisheria hapa.

Naomba ushauri wa kisheria hapa.

kyanyangwe

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2018
Posts
1,275
Reaction score
3,316
Kuna sehemu nilipata kazi private sector sasa yapata mwezi mmoja umepita,mkataba nilisaini sehemu yangu ile ya employee ila employer hakua amesaini,nikamkabidhi HR wa kampuni na taratibu nyingine za kuwa on borded zikafuatwa.sasa mpaka Leo hr hajanipa copy ya mkataba wangu ambayo imesainiwa na pande zote mbili(mwajiri na mwajiriwa) nikajaribu kuuliza kwa staff wenzangu wakongwe hapa kazini wakaniambia ndo kawaida ya hii kampuni huwa hawatoi copy za mikataba kwa staff wao kwa sababu eti kufukuzwa ni nje nje hivyo wao wanajihami na mambo ya CMA.so baada ya kuangalia mazingira ya kazi yalivyo nikajiona kama mimi ni kibarua tu hapa hivyo nimepanga nikishachukua mshahara wangu wa mwezi huu nisepe bila hata kuaga.
Je hii kisheria imekaaaje wakuu?
 
Mpaka sasa ni kitu gani kinachokutambulisha wewe kama ni staff wa hiyo kampuni?
Ikitokea wamekufukuza ghafla utaanzia wapi kudai haki zako kama tu mkataba huna?
 
Mpaka sasa ni kitu gani kinachokutambulisha wewe kama ni staff wa hiyo kampuni?
Ikitokea wamekufukuza ghafla utaanzia wapi kudai haki zako kama tu mkataba huna?
Hamna kitu,ndo maana nimeshtuka
 
Kama ni kwa wachina sepa tu,hawana future hao.na hao sunda wanaajiri kila siku
 
Back
Top Bottom