Hello, habari za muda huu! Wapendwa, naombeni ushauri kutoka kwa yeyote aliye na uzoefu na hali kama yangu na jinsi alivyofanikiwa kuondokana nayo. Mimi ninasumbuliwa sana na tatizo la kupata hedhi endelevu; naweza nikableed hata miezi mitatu mfululizo. Kwakweli, napitia changamoto kubwa na bado sijapata mtoto.
Juzi nilijaribu kumshirikisha ndugu yangu na akanishauri ninunue dawa ya Duphaston nitumie. Je, hii ni sahihi? Kama kuna daktari humu tafadhali naomba ushauri wako kuhusu hili.
Na kabla sijamaliza, napenda kusema kwamba niliwahi kwenda kufanya kipimo cha ultrasound mara tatu na majibu yalikuwa yanaonyesha kwamba kwenye mfuko wa uzazi kuna uchafu mwingi. Walinishauri nisafishe. Swali langu ni kwa nini kila mara imekuwa hivyo? Shida inaweza kuwa nini?
Naomba msaada wenu, asanteni.
Juzi nilijaribu kumshirikisha ndugu yangu na akanishauri ninunue dawa ya Duphaston nitumie. Je, hii ni sahihi? Kama kuna daktari humu tafadhali naomba ushauri wako kuhusu hili.
Na kabla sijamaliza, napenda kusema kwamba niliwahi kwenda kufanya kipimo cha ultrasound mara tatu na majibu yalikuwa yanaonyesha kwamba kwenye mfuko wa uzazi kuna uchafu mwingi. Walinishauri nisafishe. Swali langu ni kwa nini kila mara imekuwa hivyo? Shida inaweza kuwa nini?
Naomba msaada wenu, asanteni.