Naomba ushauri wenu nataka kujenga nyumba

ladyfurahia

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2011
Posts
14,753
Reaction score
9,575
WanaJF habari
naomba ushauri wenu kwani nataka kujenga ya kawaida ambayo haitagharimu pesa nyingi kwani
mimi ni mtoto wa mkulima naomba maoni, na vifaa mniandikie hapa namna gani naweza kujenga nyumba ya
kawaida yenye vyumba sita na sitting room na choo kiwe cha ndani maana kutoka nje naogopa
waungwana nisaidieni basi kwa mchangowenu wa ushauri na maoni
kiwanja ninacho kina urefu wa futi 50 x60upana sasa nianzaje kuweka hiyo ramani na je nitafanyeje
nisaidieni kwa ushauri wenu
 
no ni urefu wa mita 18 kwa upana wa mita15

Atakuwa amekosea huyu. Maana yake kiwanja kina ukubwa wa mita za mraba 270 tu? Hiyo inatakiwa labda iwe ndo saizi ya nyumba na si kiwanja maana hata vile vya high density viko kwenye mita za mraba zipatazo mia sita hivi na kidogo.
 

https://www.jamiiforums.com/business-and-economic-forum/271912-laki-5-nitajenga-nyumba.html
 
Nimesubiri huo ushauri hamjanijibu waungwana nisaidieni mwenzenu hasa mainjiiniazi pls
 
hapana ni upana na urefu kwa mita za miguu yaani unapima kwa miguu kwenda urefu na kurudi upana sijui umenielewa au bado ujaelewa
yaani futi za mraba 50x60 ndugu yangu nadhani mpaka hapo utanielewa vizuri na je vifaa ni vipi naomba nitumie mchanganuo wako
 
Naona requirements zako kama hazijaeleweka vizuri,vyumba sita vyote vya kulala?kama ndiyo nadhani space uliyonayo haitotosha.

Lakini kama una maana nyingine i.e sitting room,dinning, kitchen,other bedroms na masterbedroom inawezekana ila kwa kujibana sana,pia tambua unahitaji pia upate nafasi uweke pits za vyoo, so jaribu kuweka bayana zaidi, ila bila kukukatisha tamaa waweza pata nyumba ndogo yenye kila kitu ndani na ukafurahia.

Je wataka kujenga wapi?eneo limepimwa?una mchoro wa hicho unachotaka kujenga,kama hujanielewa uliza kadili unavyojua nitakuelekeza.karibu!
 
Hapa utakumbana na madalali fundi hapa.
Maana inaonekana kilamtu anaweka ugum ili uende chamber of kibano.
Huko atakuletea mambo ya upembuzi yakinifu, Fizibility studies,menobility studies akiingia kwenye chemibility study umeibiwa.

Kuna link humu ilieleza kwa kirefu sana,kwepa sana mtu kujifanya ni mtaalam wa mambo hayo eti aje akusaide kutokea humu,ujue ana njaa huyo utaumia.

Sie wengine tumejenga na mafundi wa mtaani mpaka leo nyumba zetu zipo.
 

Hahahaaa, umenichekesha. Lakini kama ana mchoro naweza kumuandalia schedule of materials bure, bei za materials ataweka kulingana na eneo anakoishi.
 
Mimi professional-wise ni QS (Quantity Surveyor) ninachotaka kusema ni hiki:
1. Vipimo vya kiwanja ulichosema vinakanganya. Mara unasema ukipima kwa miguu mara feet hueleweki
2. Vyumba sita (nikiamini una maanisha bedrooms maana ndio nomenclature - mtu akisema nyumba ya vyumba vitatu self-contained anamaanisha vyumba vitatu vya kulala) vinakataana na suala lako la ukubwa wa kiwanja ukuchukulia mahitaji ya nyumba ya vyumba sita vya kulala - corridors, sitting room,kitchen, bathrooms, utility etc etc.
3. Jambo la kwanza kabla ya kuamua utumie 'materials' gani unahitaji mchoro ili ujue nyumba yako ina ukubwa upi na mpangilio wa vyumba ukoje! After that kukokotoa mahitaji ya vifaa vya ujenzi inaweza kufuata hence kufikia kwenye makadirio ya gharama za ujenzi wa nyumba husika

Hitimisho ni kua taarifa yako na mahitaji yako yanakinzana, inahitaji majadiliano ya kina kati yako wewe mteja na mimi mtaalamu ili kufanikisha lile linalowezekana

Naomba kuwasilisha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…