Dadakidoti
JF-Expert Member
- Jul 26, 2024
- 399
- 1,409
Bila shaka familia ya JF, wote mko salama.
Nisiwachoshe, naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Mimi ni miongoni mwa wale wa "pangu pakavu," lakini namshukuru Mungu kwa kunijalia uhai na afya njema.
Najua humu ndani wengi wenu ni wenye vipato vikubwa, lakini naomba msisahau kuwa hata sisi walala store bado tumo. Kama ilivyo katika safari ya mamba, hata kenge wapo, hivyo msitubague.
Nije kwenye hoja: kwa kazi yangu hii yenye mshahara mdogo, nimejinyima sana na kufanikiwa kuweka akiba ya shilingi milioni 1.5. Naomba ushauri wenu, ni biashara gani naweza kuanzisha kwa kiasi hiki?
Tafadhali nisaidieni, jamani.
Muwe na siku njema!
Nisiwachoshe, naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Mimi ni miongoni mwa wale wa "pangu pakavu," lakini namshukuru Mungu kwa kunijalia uhai na afya njema.
Najua humu ndani wengi wenu ni wenye vipato vikubwa, lakini naomba msisahau kuwa hata sisi walala store bado tumo. Kama ilivyo katika safari ya mamba, hata kenge wapo, hivyo msitubague.
Nije kwenye hoja: kwa kazi yangu hii yenye mshahara mdogo, nimejinyima sana na kufanikiwa kuweka akiba ya shilingi milioni 1.5. Naomba ushauri wenu, ni biashara gani naweza kuanzisha kwa kiasi hiki?
Tafadhali nisaidieni, jamani.
Muwe na siku njema!