Naomba ushauri


Thanks kwa kunitoa tongotongo kaka!!!
 
Nina ndugu yangu alipigania watoto wake wawili hivohivo na mapaka sasa anao tamwa ni mwisho wa matatizo, huyo anataka tu kukukomoa na wivu pia, unafikiri wanapotuacha hawatupendi? hapo kashaona wivu fulani hivi kuona umeshapata mwandani wako na unaishi kwa amani, wanaume wengine wanapenda wakiachana na wake zao wapate shida sana wao ndio furaha. embu jiulize, kwa nini hakuwataka hao watoto kabla hujaolewa? Yaaani hayo maelezo ukieleza tu tamwa wala hana chake.na bado atabanwa awe analeta pesa za matumizi. na hiyo nyumba anayokaa itauzwa au itapangishwa watoto wapate pesa zao za shule
 
Nawachukia Wababa kama hao! Akafilie mbele uko kwani nani alimwambia watoto ni kuweka mimba tu? ****** kweli huyo, i hate such kind of men maana nafahamu shida wanazopata wanawake kulelea watoto pasipo usaidizi wa mmoja wapo wa wazazi. ila pia watoto wanaathirika kisaikolojia sana....mwambie nimemtukana sana tu
 
wanaume wanachosha jamani..sasa maam wa watoto yupo na hukuhudumia watoto kuanzia huko leo ndio unakumbuka wanao,dada pambania watoto hao coz kasheshe za kulelewa na step ma wengi tunazijua yeye apambane kumweka mbegu mkewe huko....chaa, hivi hiyo sheria ya miaka 7 haijabadilikaga tu? jamani wanawake tuna kazi kweli kweli.
 

yaani ndio hapo ukifikiria kuanza moja na mtu shida, ukimkuta anvyo shida cjui watu tuishije sasa....kwa wanaume wengi wanapenda kuona kakuacha halafu unaaibika ili aonekane bila yeye maisha yamekushinda, tutauza mpaka mchicha haki ya nani.
 
Asante RIWA kwa ushauri , ila ninawasiwasi pia hata mm kuhusu ndoa niliyonayo, maana kwa sasa ananisaidia je akichoka ? sasa hayo ndiyo yanayoniogopesha sana na sielewi ni kwa nn wanaume hawapendi kumuona x wake anamaendeleo yeye anataka akimwacha mwanamke ateseke mpk. na huwa wanasahau kuwa wao si Mungu.
 

watoto wana umri gani mdada?
 
Wamekushauri wapwa vya kutosha..........fanyia kazi.........mimi yangu ni pole kwa masahibu yote!
 
watoto wana umri gani mdada?

Hata mimi natamani kujua hilo.
halafu dada simama kwa miguu yako,
Neema ya Mungu inakutosha kabisaaa.
Mi naona anachotafuta huyo mshamba ni kukuharibia ndoa yako ya sasa tu,
Hana lolote, na Ashinde kabisa na alegeeeeeeeeee!!!!!

Kama wengine wanavyosema hapo juu, Sheria ipo,
Tena muache yeye awahi mahakamani, asipojikamatisha mwenyewe.
Tulia, mshirikishe Mume wako, na wazazi wako, na marafiki wale unaowamini,
na wenye uwezo wa kukusaidia kwa namna yoyote ile kuhusu hilo.
Utaona mwenyewe kiburi chake kinamuisha. Hana lilote wala usimuogope,
Hebu muone kama CRAP. Dah mi mtu aliyeniharibia maisha yangu bwana,

Simama songa mbele, huyo anayemuona mwanamke si akae naye, amzalie watoto.
Kwani leo hao watoto wamebadilika nini, hadi ajifanye anawapenda. Fukuzia mbali,
Kwanza una roho manake sidhani hata kama ningekutana naye, labda akiwepo mume wangu,
na watu wengine, lakini sio peke yetu. SIO SIRI NAWACHUKIA WANAUME WA HIVI.
Wakati ukifika watoto watamjua baba yao ni huyu, na wataaamua, kwa akili zao.
Khaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!
 
watoto wana umri gani mdada?


wa kwanza yupo darasa la sita ana miaka 11

wa pili ana miaka 9 yupo darasa la nne


nyamayao nawapenda sana wanangu na nitapigana mpk damu ya mwisho kwa ajili yao. nilipokwa nakwenda kwenye maombi nilikuwa naomba mungu anibariki nilee watoto wangu wakue ili waje wanisaidie.
 

Chukua ushauri huo wa riwa dada, ni kweli mahakama inaangalia kipindi chote hicho alikua anawatunza? sasa kama alishindwa kuwatunza kipindi hicho sasa ndio ataweza? na lazima atoe sababu za msingi zilizomfanya asitunze watoto wake kwa kipindi chote hicho. Na pia ongea na wanao tena uwafundishe na kuwaeleza athari za kukaa na mama wa kambo ili mahakamani wakatae kukaa na baba yao labda kwenda kumuona tu. Tena kumuona kama atakua anatoa matunzo.

Huyo mbaba hana lolote anachotaka ni kukuletea migogoro katika ndoa yako ya sasa kwani wanaume huwa wanapenda akikuacha uendelee kuteseka kazana maombi na usiwe na uwoga hata chembe wala usijihangaishe kuumia moyo kwani hicho ni kitu kidogo sana watoto uwalee wewe halafu ye aje achkue kiulani? hicho kitu hakuna labda watoto wenyewe wakikua waamue.

Kila la kheri nakuombe mwenyezi Mungu akutie nguvu
 

Nashukuru kwa ushauri wako.
hata mm nafikiri ni hilo la kutaka kuniharibia ndoa yangu ndilo analo kichwani kwake.

maana nilipoachana naye nilikwenda kupanga mbali kidigo naye lkn eneo ni hilohilo tegeta, basi siku moja alikuw anapita na agri mm nimebeba mtoto mgongoni asubuhi nampeleka hospitali. akaniona lkn hata kuniuliza hakuniuliza wala kunipa lift ili niwahi walaaaaa, akapita kama hanijui ihali mtoto ni wakwake, nililia sana asikuambie mtu, na sitakagi kukumbuka maana nahisi simanzi. lkn nashukuru akapita msamalia akanipa lift na pesa za matibabu. yaani nilipata shida mm anayejua ni mungu.

nitapigana na nitasimama kwa miguu yangu I PROMISE THAT.
 
Tena ana roho ya ajabu mimi asingepata nafasi ya kuzungumza na mimi tungekutana huko huko mahakamani natamani kama iyo kesi ingekua yangu yaani dada umewatunza watoto muda wote peke yako na bado unao uwezo unaanza kutishwa na hiyo CRAP ngoja niishie hapa
 
Pole sana dada agu!ushauri wangu ni huu.
Kwanza nakupongeza kwa kuto wahusisha watoto ktk huo mugogoro kwa sasa.
Na nitatofautiana kidogo na wana JF wengine walio kushauri kuwamanipulate watoto.
Mueleze mmeo wa sasa kila kitu alafu ongea na huo x wako ninyi wenyewe labda kwa kuwashirikisha tu mmeo na huyo mkewe.

Maswala ya kupelekana mahakamani na ugomvi usio na sababu kwa sasa si jambo la busara kwa sababu mwisho wa siku hao watoto watakuja jua na kisaikolajia wata athiriwa na huo ugomvi wa baba na mama. Mkubaliane tu na huo mzazi mwenzio kwa faida ya watoto kwamba watamtembelea nae ajaribu kufuta makosa ya hapo nyuma kwa kuwaonesha upendo na si kuonesha kwamba nae ana watoto au kua yeye ni baba kwa kuonea wivu baba yao wa sasa (mmeo wa sasa).

Kupelekana mahakamani ni last option na matokeo huwa mara zote si mazuri maana jibu la mahakama litakua na mwelekeo wa nani zaidi jambo ambalo kwako sikuona likiwa kipaumbele. kipaumbele kwako ni well-being ya watoto wako nakusifia kwa hilo.

Kushindwana tabia si uadui, ni mwelekeo tu mwingine wa maisha. kila la kheri
 
Reactions: Mbu
JF leo especially MMU Full Huzuni kwa thread. Mie hii imenigusa sana naondoka bila kusema au kutoa ushauri because I can feel it.

The only word I can say is "POLE SANA"
 
Mwehu tu huyo anahaha huyo mkewe hana kizazi? si alimuona wa maana mpaka akakutoa ndani Mungu huyu tunayemuabudu na huwa anawapa pigo watu wasio na utu kama hawa. Hivi mwanaume mwenye akili atampita x na mtoto wake bila kujua hali yake? ushamba tu unamsumbua. Usiwatoe watoto wako wakaanze kwenda kuishi kama wakiwa wakati wewe upo. kama alishindwa kuwaonyesha mapenzi hapo nyuma mlipoachana atawapenda sasa hivi kweli? si ndio atawanyanyasa mpaka basi.
 

Umeona eeeee! yani mwehu kwani kidogo, mahakamani tu ila anzia tamwa
 
Lisa na hao watoto wa mzee vipi wana access na mama yao? mama yao mnaelewana ? binafsi naona watu kama wameachana bado ni muhimu watoto wawe na access na wazazi wao wote wawili.Jaribuni kupata namna nzuri ya watoto kuwa wanakutana na baba yao,wanamhitaji pia hata kama alikunyanyasa maana hayo ni ya kwako na yeye na si ya watoto,kwao yeye ni baba tu.Ikibidi jenga pia mawasiliano na mkewe ili watoto wakienda kumsalimia baba yao uweze kuwa unapiga simu na kuongea nao.By the way kitu gani kinakufanya uone kwamba watoto wakiishi na baba yao watakuwa machangu?mbona kuna mababa wengi tu single fathers na wanalea vizuri watoto wao?
 
Usichanganyikiwe hata kidogo bidada, nina uhakika hawezi kuwachukua hao watoto hata siku moja, nina uhakika watoto watagoma na atawaacha na hata hiyo sheria yenyewe itachemka
 

Kama aliweza kuwapita huku wanatembea na miguu na mtoto anaumwa leo atawapa umuhimu wowote? anataka kuwafungia tu misaada kwa baba yao mpya ndio maana wababa kama hawa huko nchi za mbele mtoto anakataa kabisa kuhusika nae. wamtambue na awaombe msamaha,ingekuwaa ugomvi ni between baba na mama angewapa wale watoto priorities zao ila baad ya kuona wako kivulini ndio anabana mambupu yake. apeleke huko kwa huyo anayeishi nae
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…