Naomba uzoefu kuhusu Honda Fit

KABAKA28

JF-Expert Member
Joined
Jun 18, 2014
Posts
204
Reaction score
191

Habari wana Jf, natumai mu wazima.

Leo naomba kuuliza wataalam walio wahi kumiliki/Kutengeneza gari aina ya Honda Fit, naomba kujua yafuatayo:

1. Ustahimilovu wa miundombinu (Barabara za Tanzania).

2. Ulaji wa mafuta (Compared to IST, VITZ, RAUM-JAMII YA TOYOTA)

3. Upatikanaji wa spare zake na gharama za spea.

4. Kwanini sio nyingi mjini.

5. Je inafaa kufanyia biashara ya UBER?

Asante, naomba kuwasilisha.

MAONI NA MICHANGO YALIYOTOLEWA NA WADAU WA JF


Mrejesho
 
Kwa ufahamu wangu kuhusu hzo gari, nitakuelezea kama ifuatavyo
Declaration of interest;

- Nazipenda sana gari za Honda bila kujalisha ni aina gani. Na natumai ipo siku ntaacha kutumia Toyota na kuhamia Honda.

Maelezo kuhusu Honda fit kulingana na ufahamu wangu;

1)Honda ni moja ya gari ngumu sana zinazotengenezwa japan, hvyo ustahimilivu wa barabara zetu ni mkubwa sana.

2) Honda Fit ulaji wake ni mdogo sana kutegemeana na engines, wana engines za: 1.2L, 1.3L, 1.4L , 1.5L nimeweka kwenye hzo groups kuondoa confusion kwa maana zipo za 1198 cc, 1297cc, 1246cc na zote zinaangukia kwenye 1.2L. hvyohvyo kwa za 1.3, 1.4 na 1.5 .

Lakini nyingi za bongo zinaangukia kwenye 1.3L(1330cc na 1310cc).
Hvyo kwenye suala LA ulaji wa mafuta ni kidogo sana na haitatofautiana na IST au Vitz zenye 1.3L.

3) Upatikanaji wa spares ni mkubwa wala isihofi, na pia soku hizi mambo yamerahisishwa sana waweza kuagiza moja kwa moja.

4) Honda Fit ni nyingi ila inategemea unalinganisha na gari gani.

5) Unaweza kutumia kwa biashara, Honda fit zipo kwenye generations 3 kama ifuatavyo:
I. 2001 - 2008,

hizi ni kama kusema toleo kwanza na ndo zipo nyingi bongo.
II. 2009 - 2014,

hizi zipo chache na zinamuonekano mzuri sana waweza sema sio Honda fit, kama BMW
III. 2014 to present,

Kwa matoleo hayo ukichukua latest inaweza kupigia biashara na mteja wako akahisi kama upo kwenye Lamborghini au Maybach, kwa lugha nyepesi INAFAA KUFANYIA BIASHARA
 
Mdau hapo juu kaongea vizuri sana, ningependa kujazia nyama kidogo.

As a car dealer, ushaur wangu naweza kukupa kulingana na mwaka husika wa gari sababu hua zinatofautiana sifa kulingana na mwaka.
 
Asanteni sana kwa mrejesho, kulingana na kabajeti kangu, nilitaka kuchukua ya mwaka 2004. Ili kupunguza purukushani za TRA maana naona inavyozidi kuwa latest, na ushuru unaongezeka, sijui nyinyi kama wataalam mnanishaurije.
 
Kwa ufahamu wangu kuhusu hzo gari, nitakuelezea kama ifuatavyo
Declaration of interest;

- Nazipenda sana gari za Honda bila kujalisha ni aina gani. Na natumai ipo siku ntaacha kutumia Toyota na kuhamia Honda.
...
Mkuu uko fit sana kwenye nyanja hii ya magari!
 
Asanteni sana kwa mrejesho, kulingana na kabajeti kangu, nilitaka kuchukua ya mwaka 2004. Ili kupunguza purukushani za TRA maana naona inavyozidi kuwa latest, na ushuru unaongezeka, sijui nyinyi kama wataalam mnanishaurije.
Mkuu wangu chukua tu!! Honda ni gari nzuri na relatively ina bei ndogo kulinganisha na counter part zake za Toyota kama Vitz na ist!!!
Mimi nina Honda Fit Aria ya 2005 iko poa sana!!

Nizaidi ya mwaka mzima naitumia sijawahi kupata tatizo la kuifundi lililonihitaji kufunga spare/kifaa kipya!!! Labda kwa vile ni ya matumizi binafsi, kama ni ya biashara hapo sina experience.
 
Ngoja nikaiagize, asanteni sana kwa mrejesho. Kwakweli mm niliipenda imbo lake sio kama vitz na ni pana ndani pia. Nitawapeni mrejesho.
 
Vipi kuhusu sources kuna hawa watu wanajiita SBT Japani naona wanagharama ndogo relatively to trade car view na be forward... Any experience?
 
Exactly, na mimi huwa nawaza kwanini mtu ananunua vitz ambayo kwanza ni bei kubwa lkn mwonekano wake hata siyo classic kama Honda Fit!
Nafikiri ni dhana ya upatikanaji wa vipuli, watu wengi wanadai gari tofauti na Toyota vifaa vyake ni ghali sana, na hua havipatikani kiurahisi.
 
Vipi kuhusu sources kuna hawa watu wanajiita SBT Japani naona wanagharama ndogo relatively to trade car view na be forward... Any experience?
Mi nilichukuliaga Be forward!! Tradecarview huwa wanabei kubwa, sijui kwanini? Lkn hao SBT huwa ni wazuri na waaminifu kama befoward tu. Huna haja ya kuogopa
 
Kwa ufahamu wangu kuhusu hzo gari, nitakuelezea kama ifuatavyo
Declaration of interest...
Mkuu ngoja niinunue, nitakutafuta. Ulo vizuri sana kwenye magari, ubarikiwe zaidi.
 
Mdau hapo juu kaongea vizuri sana, ningependa kujazia nyama kidogo.

As a car dealer, ushaur wangu naweza kukupa kulingana na mwaka husika wa gari sababu hua zinatofautiana sifa kulingana na mwaka.
Nahitaji ya mwaka 2004 au 2005 ambayo haijatembea km zaidi ya 60k, vipi naweza kuipata kwa bei gani kwenu? Rangi iwe silver au nyeupe ya kupauka.
 
Wakuu nimerudi tena baada ya kimya kirefu. Nimeagiza honda Fit ya mwaka 2004 kupitua SBT Japan sasa n wiki ya pili.... Kila kitu kinaenda sawa.

Naomba kuuliza wazoefu wq clearing and forwarding, kama kuna mtu anafanya hii kitu au anamjua anaeweza kunifanyia kwa bei nafuu.
Nimesikia wale wa SBT wana bei kubwa sana, na vyuma vimekaza sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…