Naombeni kujua vitu vya msingi na gharama kufungua radio ya kidini inayoshika wilaya au mkoa tu

Naombeni kujua vitu vya msingi na gharama kufungua radio ya kidini inayoshika wilaya au mkoa tu

matunduizi

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2018
Posts
7,968
Reaction score
19,368
Rejea kichwa cha habati hapo juu.

Baada ya kuona upotoshaji unaongezeka na watu wakizidi kudanganywa. Mwenyezi Mungu amenielekeza kufungua radio na baadae TV ambayo itasambaa dunia nzima kwa lugha zote kutokea Tanzania.

Hapa nitakuwa nafundisha neno tu, hakuna ujanjaujanja wala upigaji wala maigizo ya miujiza. Lengo ni kuwaconnect watu na Mungu sio na mimi ili wabarikiwe hapa duniani kimungu na waende mbinguni baadae.

Naombeni mawazo na ushauri.

Kwa haraka nataka kuanza na Radio inayoshika kuanzia ukubwa wa eneo la wilaya.

Sina wasiwasi na gharama maana Mungu hawezi kukupa wazo asikupe na vyanzo vya kutekelezea.

Karibuni kwa mawazo zaidi. Maana naamini Mungu huwa anawapa watu ideas kwa ajili ya watu wake.

Mfano Yethro kwa Musa.
 
Nenda kwenye kituo chochote cha Radio watakupatia maelezo husika na taratibu zake. Au kama ni mvivu funga kwa sala na maombi utajulishwa hivyo vitu kwenye maombi kabisa
 
Back
Top Bottom