Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 22, nimezaliwa Mwanza. Mama alifariki nikiwa na miaka 5 na baba yeye hata simjui maana niliye kuwa nimeambiwa kuwa ni baba nilipomfuata aliiataa na kusema mimi siyo mwanawe.
Nimeishi na mimi kizaa mama, licha ya ugumu wa maisha kwa bibi lakini bibi alinipeleka shule. Nimesoma kwa shida hadi nikamaliza shule ya msingi.
Nilipofaulu kuingia kidato cha kwanza, nyumbani tulikuwa na mbuzi watatu tuliwauza na kuanza shule,mwaka wa pili ulipowadia nilianza kulima busitani ya mbogamboga, nilifanikiwa nikawa nimelipia ada ya shule.
Nilienda hivyohivyo hadi kidato cha tatu, lakini ilipofika mwenzi wa tisa 2010 nikiwa kidato cha tatu bibi aliamua kuolewa akaniambia niache shule kutokana na ugumu wa maisha. Nilikataa nikamwambia bibi nitabaki pale pale aliniachia kiasi kidogo cha chakula nikawa natoka shule nakuja kupika lakini kiliisha nikaamua nihame nikahamia kwa ndugu napo pakawa matatizo! Lakini nilijikaza na kukomaa na shughuli zangu za mbogamboga.
Ilipofika mwezi wa sita 2011 hali ikazidi kuwa tete maana nilikuwa naenda shule lakini nikirudi sipati chakula hadi jioni ndo nakula lakini nilivumilia tu
Nilipomaliza shule nililazimika kurejea pale tulipokuwa tukiishi na bibi nikaishi huku nikiendeleza shughuli zangu za mbogamboga, baada ya matokeo ya kidato cha nne nilituma maombi ya kujiunga na chuo cha ualimu sikuchaguliwa nikaenda kufanya interview Kolandoto chuo cha nursing nikachaguliwa kujiunga na diploma in Laboratory Technology lakini kutoka na ada kuwa kubwa sikufanikiwa kujiunga.
Ilipofika mwezi wa 12/12/2012 alikuja ngugu yake na bibi kutoka Dar akaniambia atanisaidia kuweza kupata chuo na kunisaidia kunilipia mahitaji ya chuo, nikaona inafaa nikaondoka nae hadi dar nilikuwa na pesa kidogo kama laki tatu nikamkabidhi ili nikitaka kwenda chuo nazo zitasaidia kuongezea.
Nilikaa kwake hiyo 2013 , alinikabizi shughuli zake kufanya pasipo malipo nilifanya kwa nguvu zote. Pia ulipofika wakati wa kutuma maombi nilituma lakini kwa bahati mbaya ilipofika mwezi wa 8 ,2013 nilipata ajali nikavunjika mguu sehemu ya paja.
Nilitibiwa Muhimbili hadi leo naendele vizuri.
Mwaka jana nilituma maombi nikachaguliwa chuo cha St. BAKHITA, NA SITY COLLEGE OF HEALTH AND ALIAD SCEINCE lakini mufadhili wangu akaniambia hayuko vizuri nisubiri mwaka huu lakini nimeongea nae ananiambia tena hatakuwa vyema, kutokana na kuwa atakuwa na wanafunzi wengi wa kusomesha.
Ndg zangu nimeishi hata vya kusema, na hapa nilipo mguu bado unaniuma kwa mbali.
JAMANI kwa yoyote anaeguswa naomba msaada!!! Nimehitimu kidato cha nne 2011,na kufanikiwa kupata division IV ya 26.
Matokeo yangu ni kama ifutavyo :-
Physics "C "
Chemistry "C "
Biology "C "
B /maths "D "
English "F "
Naombeni msaada wa ufadhili ili nijiunge na chuo. Nitashukuru sana kama nitasaidiwa kwa namna yoyote ile.
Wenu,, Marco Yohana.
Nimeishi na mimi kizaa mama, licha ya ugumu wa maisha kwa bibi lakini bibi alinipeleka shule. Nimesoma kwa shida hadi nikamaliza shule ya msingi.
Nilipofaulu kuingia kidato cha kwanza, nyumbani tulikuwa na mbuzi watatu tuliwauza na kuanza shule,mwaka wa pili ulipowadia nilianza kulima busitani ya mbogamboga, nilifanikiwa nikawa nimelipia ada ya shule.
Nilienda hivyohivyo hadi kidato cha tatu, lakini ilipofika mwenzi wa tisa 2010 nikiwa kidato cha tatu bibi aliamua kuolewa akaniambia niache shule kutokana na ugumu wa maisha. Nilikataa nikamwambia bibi nitabaki pale pale aliniachia kiasi kidogo cha chakula nikawa natoka shule nakuja kupika lakini kiliisha nikaamua nihame nikahamia kwa ndugu napo pakawa matatizo! Lakini nilijikaza na kukomaa na shughuli zangu za mbogamboga.
Ilipofika mwezi wa sita 2011 hali ikazidi kuwa tete maana nilikuwa naenda shule lakini nikirudi sipati chakula hadi jioni ndo nakula lakini nilivumilia tu
Nilipomaliza shule nililazimika kurejea pale tulipokuwa tukiishi na bibi nikaishi huku nikiendeleza shughuli zangu za mbogamboga, baada ya matokeo ya kidato cha nne nilituma maombi ya kujiunga na chuo cha ualimu sikuchaguliwa nikaenda kufanya interview Kolandoto chuo cha nursing nikachaguliwa kujiunga na diploma in Laboratory Technology lakini kutoka na ada kuwa kubwa sikufanikiwa kujiunga.
Ilipofika mwezi wa 12/12/2012 alikuja ngugu yake na bibi kutoka Dar akaniambia atanisaidia kuweza kupata chuo na kunisaidia kunilipia mahitaji ya chuo, nikaona inafaa nikaondoka nae hadi dar nilikuwa na pesa kidogo kama laki tatu nikamkabidhi ili nikitaka kwenda chuo nazo zitasaidia kuongezea.
Nilikaa kwake hiyo 2013 , alinikabizi shughuli zake kufanya pasipo malipo nilifanya kwa nguvu zote. Pia ulipofika wakati wa kutuma maombi nilituma lakini kwa bahati mbaya ilipofika mwezi wa 8 ,2013 nilipata ajali nikavunjika mguu sehemu ya paja.
Nilitibiwa Muhimbili hadi leo naendele vizuri.
Mwaka jana nilituma maombi nikachaguliwa chuo cha St. BAKHITA, NA SITY COLLEGE OF HEALTH AND ALIAD SCEINCE lakini mufadhili wangu akaniambia hayuko vizuri nisubiri mwaka huu lakini nimeongea nae ananiambia tena hatakuwa vyema, kutokana na kuwa atakuwa na wanafunzi wengi wa kusomesha.
Ndg zangu nimeishi hata vya kusema, na hapa nilipo mguu bado unaniuma kwa mbali.
JAMANI kwa yoyote anaeguswa naomba msaada!!! Nimehitimu kidato cha nne 2011,na kufanikiwa kupata division IV ya 26.
Matokeo yangu ni kama ifutavyo :-
Physics "C "
Chemistry "C "
Biology "C "
B /maths "D "
English "F "
Naombeni msaada wa ufadhili ili nijiunge na chuo. Nitashukuru sana kama nitasaidiwa kwa namna yoyote ile.
Wenu,, Marco Yohana.