Naombeni msaada: Nakosa usingizi usiku lakini mchana nalala sana!

TRIPLE H

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2013
Posts
651
Reaction score
349
Wakuu,
Tatizo langu ndo hilo kwamba usiku kucha sipati kabisa usingizi, lakini kukishapambazuka ndio nahisi kulala. Sana mida kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi jioni saa 12 nakuwa na usingizi wa ajabu kiasi kwamba popote niwapo napitiwa kabisa najikuta nakoroma. Tatizo ni nini? Nina kama miezi minne sasa nikiwa kwenye hali hii.
Naombeni ushauri na msaada wenu wakuu.
Ahsanteni.
 
Kunywa mlonge/au uwatu ni mzuri sana kwa wenye tatizo kama lako
 
Mzungu bana hapa ndio alitupiga Bao, utakuta akiingia kitandani kwa pembeni anavuta "Novel" Au "Journal" Ana soma.. Lengo ni nini? Kuutafuta usingizi... Una weza kudhani wana penda kusoma vitabu kumbe hamna lolote....
 
Ukiwa na majukumu huo usingizi utaisha wote ni suala la muda tu.
 
Mi usingizi wangu kuanzia saa sita daah! Naangusha gari ofisini

Majanga!
 
Reactions: BAK
Huna mwenza wako? Piga viwili vya afya na usingizi utakuja tu.

Usipokuja Wahi hospital
 
Mzungu bana hapa ndio alitupiga Bao, utakuta akiingia kitandani kwa pembeni anavuta "Novel" Au "Journal" Ana soma.. Lengo ni nini? Kuutafuta usingizi... Una weza kudhani wana penda kusoma vitabu kumbe hamna lolote....
Barabara huwa unavuka mwenyewe?
 
1. Jitahidi kutwa 1 ipite bila kulala mchana, lazima usiku utalala. Unachokifanya sasa ni kuuzoesha mwili kulala mchana na ndio maana usiku unakosa usingizi. Mwili wako umeanza anza kuzoea hiyo classical conditioning. Pindua hiyo ratiba.

2. Epuka msongo wa mawazo kama unao coz inaweza kuwa sababu pia. Usiku kuna utulivu so labda mwenzetu muda huo ndio unaanza kuwaza na kuwazua yanayokusonga tofauti na mchana kunapokuwa na pilika na hekaheka unajikuta huwezi kuzama mawazoni na ndio maana unalala.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…