Naombeni msaada tatizo la figo

Keben

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
725
Reaction score
175
Mzee wangu ana miaka 52. Tangu 2007 amekuwa akisumbuliwa na FIGO ameenda kutibiwa hadi Seliani. tatizo hii bado lipo; dalili zinazo onekana ni kushindwa kula, kushindwa kutembea, maumivu makali ya pande za tumbo, mkojo mchafu wenye rangi tofautitofauti, siku anaumwa hucheua sana.

Natanguliza shukrani
NB: Hanywi pombe ila anavuta sigara
 
Pole kiongozi keben. ngoja waje matabibu.
 
Mpe Pole Mzee wako mimi Dawa ya kumtibu mzee wako maradhi ya figo ninayo na akitumia dawa yangu atapona ukihitaji nitafute kwa kubonyeza hapa.Mawasiliano
 

pole sana mkuu kwa matatizo ya mzee wetu na post yako kwa kiasi fulani imenilengesha machozi kwani hao wazee ndiyo hazina yetu vijana.
 
Tenda wema mkuu MziziMkavu, uwezalo saidia, saidia tu wala usichoke, vinywa vinavyokushukuru ni rehema na baraka kwako, Mungu ndiye atakayekulipa, c kila bnadam anaweza toa shukran.... Mungu azidi kukujalia Afya bora


Ndugu Keben pole kwa kuuguza, Mungu ampe nguvu mzee watu, atapona tu.
 
Huo mkojo ni vizuri ukaspecify wa rangi gani...maana rangi fulani ya mkojo huelezea tatizo fulani..kwa mfano mkojo rangi ya chai unaindicate tatizo tunaliita kitaalam acaptonuria ni tatizo la kibiokemia zaid linalohusu metabolism ya amino acids, mkojo mzito wenye rangi inayotaka kufanana na maji ya mchele huindicate chyluria.

kwa hiyo mkuu ili tukusaidie inabidi uspecify vizuri hizo dalili maana kunamatatizo mengi na kila tatizo uja na dalili zake specific...huwezisema mkojo wa rangi mbalimbali, inabidi utaje hiyo rangi japo kwa kufananisha kama haunauhakika....funguka vizuri tukusaidie madaktari tupo
 

Nashukuru kiongozi. Anakojoa rangi tofauti, yaani kama chai ya rangi, njano, maji ya mchele(mazito) na hukojoa harakaharaka sana(kila baada ya dakika 5), hushindwa kitembea, huumwa zaidi na hucheua sana hasa anapokula vitu vyenye mafuta kama nyama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…