Naombeni ushauri: Je, ninunue simtank nihifadhie maji au nijenge Kalo?

Naombeni ushauri: Je, ninunue simtank nihifadhie maji au nijenge Kalo?

Kwann amekuwa mchaw?
Mkuu vijana hawa tuwaache kama walivyo , hata hakuelewa mantiki yangu , alichofanya ni kukumbuka shughuli zake za kichawi na babu yake shamba huko , honestly sijaelewa maana zaidi ya hiyo
Ukiachana na hayo ujenzi pia una raha yake ndo Mana napenda kushauri lolote ninalolijua kuhusu ujenzi , I'm not the best at it Ila kwenye ku save nipo vzr , hapa nina ujenzi darasa kongowe huko target yangu nataka nihamie kwenye nyumba bila kuspend 10 million. Nikifanikiwa naleta mrejesho
 
Mkuu vijana hawa tuwaache kama walivyo , hata hakuelewa mantiki yangu , alichofanya ni kukumbuka shughuli zake na babu yake shamba huko , honestly sijaelewa maana ya kuniita mi mchawi
Ukiachana na hayo ujenzi pia una raha yake ndo Mana napenda kushauri lolote ninalolijua kuhusu ujenzi , I'm not the best at it Ila kwenye ku save nipo vzr , hapa nina ujenzi darasa kongowe huko target yangu nataka nihamie kwenye nyumba bila kuspend 10 million. Nilifanikiwa naleta mrejesho
Sawa
 
Kutokana na kipind hch maji changamoto nikuleta boza na kuniwekea maji na mvua ikinyesha itasaidia pia
Nashauri kama una eneo la kutosha bora ujenge underground tank la ukubwa utakaotosheleza matumizi ya muda unaotaka , niliwahi kuishi kwenye nyumba yenye tank la kujengewa ardhini nilisahau kabisa shida ya maji kwa kipindi nilichoishi hapo, ukivuna msimu mmoja unatumia mda mrefu kulingana na ukubwa wa tank utakalojenga.
 
Nashauri kama una eneo la kutosha bora ujenge underground tank la ukubwa utakaotosheleza matumizi ya muda unaotaka , niliwahi kuishi kwenye nyumba yenye tank la kujengewa ardhini nilisahau kabisa shida ya maji kwa kipindi nilichoishi hapo, ukivuna msimu mmoja unatumia mda mrefu kulingana na ukubwa wa tank utakalojenga.
Nachukua ushau wako
 
Ushauri wangu ajenge kisima (sijui ndo amemaanisha karo?),mimi nilijenga cha kuingia litre 5,000 mpaka sasa nimekifunika juu kinatumika kuvuna maji mvua.

Hakikuwa na gharama kubwa maana tofali nusu zilifukiwa na nusu zikapanda juu gharama ilikuwa labda kwenye cement tu na siyo ya kutisha,ukisema ununue tank kwa litakaloingia lita elf5 siyo chini ya 700K ila kisima hakitakost zaidi ya laki5 na utakuwa huna wasiwasi wa kuibiwa still utakitumia kuhifadhia maji ukihamia.
 
Mie ujenzi wangu wa kwanza nilifanya kuchimba chemba ndogo ya choo (maji taka) kwanza kisha ndio nikawa nahifadhia maji kipindi chote cha ujenzi nilipomaliza ndio nikanunua matenki ya juu baada ya kuanza kufunga mifumo ya maji na shimo nikalitumia kwa kazi yake husika

Mpk leo mradi wowote wa ujenzi natumia kanuni hiyo hiyo
Fuata ushauri huu. Hii kanuni bora kabisa kama unataka kusave gharama zisizokuwa na ulazima
 
Ushauri mwingine jamani! Eti septic tank utumie kuhifadhi maji ya kujenga! Khaaaaa! Hiyo nyumba si itanuka hadi Kenya huko wapate harufu.
 
Ushauri mwingine jamani! Eti septic tank utumie kuhifadhi maji ya kujenga! Khaaaaa! Hiyo nyumba si itanuka hadi Kenya huko wapate harufu.
Hujaelewa. Lile septic tank unalijenga kabla ya nyumba wala kuliunganisha na mfumo wa maji taka. Unalitumia kama hifadhi ya maji mpk hapo unapomaliza ujenzi ndio unaliunga na mfumo wa majitaka

Sijui nini hujakielewa hapo
 
Ushauri,unapoanza ujenzi ni muhimu sana kuanza kujenga kisima cha maji au karo tena karo hilo au kisima hicho kiwe kikubwa cha kutosha kuhifadhi maji kisi cha malori yasiyopungua matatu.Kiwe cha chini ya ardhi kwa maana hiyo utahitaji kuchimba na kujenga. Faida mojawapo ni kwamba kifusi kitakacho tokana na kisima hicho kitatumika kwenye msingi wa nyumba unayotegemea kuijenga sambamba pia utakuwa na tanki la maji ya kutosha hata kana itakubidi kununua maji kwa lorry aka boozer basi utakuwa na uhakika kuwa maji yatatosha. Sambamba pia tanki hilo linaweza kuendele kutumika kuhifadhi maji pindi ujenzi utakapo kamilika au pia kutumika kama mojswapo ya mashimo ya choo.
 
Mie ujenzi wangu wa kwanza nilifanya kuchimba chemba ndogo ya choo (maji taka) kwanza kisha ndio nikawa nahifadhia maji kipindi chote cha ujenzi nilipomaliza ndio nikanunua matenki ya juu baada ya kuanza kufunga mifumo ya maji na shimo nikalitumia kwa kazi yake husika

Mpk leo mradi wowote wa ujenzi natumia kanuni hiyo hiyo
smart. Unaua ndege wawili kwa jiwe moja,sim tank pia ni risk kama eneo halina usalamawahuni wanabeba. I did the same.
 
Uzuri wa simtank linahamishika, ama kuliuza.. karo je?


Nunua la lita 2000 ama 3000, au yale ya migodini ya lita 1000 ya pembe 4, i think laki mbili bei yake
 
Gharama za simtank
Screenshot_20210513-182335.jpg
 
Nunua simtank, baada ya ujenzi litakusaidia kuifadhia maji ya familia, ushauri wangu nunua simtank ambalo hata kwa baadae litasaida kwenye familia, usinunue dogo sana angalau mil 5000 au 3000
Ubora je
 
Gharama za kuchimba na kujenga shimo
1. Tofali 300-400 = 400,000/=
2. Kuchimba shimo 150k -200k
3. Cementi mifuko 10 x 18,000 = 180,000
4. Fundi kujenga tofali 150,000
5. Hupiga plasta 60,000
6. Water proof cement 10x5000
7. Wire mesh 8 x 20,00p
Bado kufunika juu
Nondo sinaona ufafanuz nzuri
 
Back
Top Bottom