Mimi si mtaalamu wa masuala ya biashara na ili kupata ushauri wa kitaalam unaweza kukutana na wataalam waliosajiliwa. Ila naweza kusema haya nilisikia watu wakisema hii biashara sio nikajifariji kwamba control yangu ni nzuri na tofauti na wanaofanyia mazoea kilichonikuta ni siri yangu hadi sasa nimebaki na baadhi ya pikpik nimefungia ndani. hii ni aina ya biashara ambayo ili uifanye itakubidi muda wote uwekeze hapo huwezi kufanya mambo mengine. vijana wanaoendesha vyombo hivyo ndo watakukwamisha ile hujuwahi ona. tena wewe unaanza na kumi.. jiangalie vizuri mkuu.. ni rahisi kusimamia fulo moja ya kubeba mawe,mchanga etc kuliko toyo 10. ila akili kichwani mwako kama unaamini kwenye mipango yako basi kila la heri.