Naombeni ushauri wa Biashara ya vitenge kutoka Zambia

Naombeni ushauri wa Biashara ya vitenge kutoka Zambia

Yohimbe bark

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2019
Posts
2,160
Reaction score
5,728
Habari wakuu,

Nataka kuanza kufanya hii biashara ya vitenge kutoka Zambia, kuna Jamaa anaifanya biashara hii aliniambia ina faida yeye alianza na mtaji wa milioni 1.5 mpaka sasa mtaji umefikia milioni 8 na ana miezi 9 kwenye game, aliniambia nitafute mtaji then anipe connection ila toka nimwambie mtaji nishapata hanipi ushirikiano kabisa na simu hapokei kwa sasa.

Wateja nishatafuta nimewapata, ombi langu kama kuna mtu ashaifanya hii biashara anipe abc kuanzia issue za TRA na mengine, nawaza niende mwenyewe Zambia nikafanye research kwanza ila nikaona sio mbaya kuwashirikisha wanajukwaa naweza kupata ushauri wowote mzuri.
 
Sio kila mwanadamu anapenda kuona hatua zako kimaendeleo hivyo usiumize kichwa fanya survey mwenyewe, jilipue nenda kafanye biashara huko hakika mola mlezi atakujalia hitaji lako pia usikate tamaa kwa maana changamoto ni kawaida katika maisha.
 
Mkuu
Isanga family nishauri chochote kaka mkubwa.
Hiyo biashara ina kodi kubwa sana ili kuzuia watu wasilete Tanzania ingawaje vingi vinatoka China.

Ukienda kuchukua vitenge Zambia ina maana itakua biashara ya kukwepa kodi kitu ambacho ukikamatwa na TRA watachukua mzigo wako wote huko Tunduma, Songwe ni kweli ni biashara yenye faida kubwa na mzunguko upo ila hatari yake ndio hiyo kodi yake ni 100% kitu ambacho ukinyooka pale Customs utaacha mzigo wako kwa makadirio utakayopewa.

Mimi binafsi huwa sishauri mtu afanye bisahara ya kukwepa Kodi kama unaanza maana ukiipoteza hiyo pesa utachanganyikiwa zaidi na pia hiyo bisahara inahusu sana kukopesha na wateja wengi sio walipaji mkuu ukitaka upate pesa kaa na mali yako uza kwa kulipwa shilingi yako.

Zambia na DRC au kasumbalesa Vitenge vingi.

Ukiweza nenda pale Kasumbalesa mpaka wa Zambia na DRC wanauza TV bei ndogo sana utakuja kuwauzia Watanzania panoja na Friji kubwa na ndogo utasafirisha kwa maroli yanayorudi bila mzigo mpaka Nakonde...TV zinauzwa bei ndogo ukiweza waulize hao madereva wa magari yanayokwenda DRC na ukiwa naza kadhaa nyooka hapo TRA wape pesa zao unalipa kutokana na Receipt ya Kasumbaresa...2m pale unaenda na TV unapata kadhaa kwa kujibana ndio Life hiyo.
 
uliwezaje kupata wateja kwa bidhaa ambayo hauna?

uliwaonesha Sample gani?
Kwanza aliniambia niende mjini nikatafute wateja then aongee nao ila nisiwambie kama mzigo unatoka zambia niwadanganye hata mbeya au sehemu yoyote ile ili wasije kufata wenyewe zambia basi nikafanya hivyo nikaenda duka la kwanza nikajieleza jamaa kasema haina shida ila nimuoneshe sample ikabidi nimpigie jamaa akaniambia mpe simu nikampa wakaongea mteja akataka kutumiwa sample jamaa akamtumia through whatsapp basi mteja akavipenda akasema yupo tayari kuchukua 1000pcs kila week.

Nikaenda kwenye duka la pili nikafanya hivyo hivyo mteja akasema atachukua 500pcs kila week basi jamaa akasema hao wateja wawili wanatosha kwa kuanzia mimi nikaondoka, ila toka siku hiyo nikimcheki chenga nyingi inaonekana kanizunguka wale wateja kachukua yeye.
 
Mkuu

Hiyo biashara ina kodi kubwa sana ili kuzuia watu wasilete Tanzania ingawaje vingi vinatoka China.
Ukienda kuchukua vitenge Zambia ina maana itakua biashara ya kukwepa kodi kitu ambacho ukikamatwa na TRA watachukua mzigo wako wote huko Tunduma, Songwe ni kweli ni biashara yenye faida kubwa na mzunguko upo ila hatari yake ndio hiyo kodi yake ni 100% kitu ambacho ukinyooka pale Customs utaacha mzigo wako kwa makadirio utakayopewa..
Mimi binafsi huwa sishauri mtu afanye bisahara ya kukwepa Kodi kama unaanza maana ukiipoteza hiyo pesa utachanganyikiwa zaidi na pia hiyo bisahara inahusu sana kukopesha na wateja wengi sio walipaji mkuu ukitaka upate pesa kaa na mali yako uza kwa kulipwa shilingi yako...
Zambia na DRC au kasumbalesa Vitenge vingi...
Ukiweza nenda pale Kasumbalesa mpaka wa Zambia na DRC wanauza TV bei ndogo sana utakuja kuwauzia Watanzania panoja na Friji kubwa na ndogo utasafirisha kwa maroli yanayorudi bila mzigo mpaka Nakonde...TV zinauzwa bei ndogo ukiweza waulize hao madereva wa magari yanayokwenda DRC na ukiwa naza kadhaa nyooka hapo TRA wape pesa zao unalipa kutokana na Receipt ya Kasumbaresa...2m pale unaenda na TV unapata kadhaa kwa kujibana ndio Life hiyo..
Nimekupata kaka.
 
Nimekupata kaka.
Huyo jamaa anakukimbia shukuru sana maana hiyo kazi ni kama kuuza madawa ya kulevya Tanzania wanaoweza kufanya ni wale walio mikoa ya mpakani kama Mbeya na Iringa kupeleka hiyo bidhaa sio kazi ila ukizidi hapo jua umepoteza ingawaje mapapa wanafanya wakipoteza mara moja anapata mara tano baadae...
 
Huyo jamaa anakukimbia shukuru sana maana hiyo kazi ni kama kuuza madawa ya kulevya Tanzania wanaoweza kufanya ni wale walio mikoa ya mpakani kama Mbeya na Iringa kupeleka hiyo bidhaa sio kazi ila ukizidi hapo jua umepoteza ingawaje mapapa wanafanya wakipoteza mara moja anapata mara tano baadae...
Kweli mkuu mara ya mwisho nilimpigia akaniambia mzigo wake umekamatwa na tra nikamuuliza lakini si uliniambia unasafirisha kihalali akaniambia ngoja kidogo nitakutafuta akakata simu.
 
Back
Top Bottom