Naombeni ushauri wa dawa ya Mafua

Joined
Oct 27, 2017
Posts
91
Reaction score
94
Mimi nina ndugu yangu katokea jijini Dar kaja kuniona jijini mbeya lakini toka amefika baada tu yakukaa siku nne yalimuanza mafua mazito wakati mwingine ya maji maji pia kifua kina mbana na kikohozi hakiishi.

Tumeenda hospitali kucheki afya tumekuta hana tatizo dawa nyingi tumetumia ila wapi yote ayo ilikuwa ni kwa ushauri wa madaktari na wataalam wa afya Sasa imefikia hatua anakohoa usiku mzima mpaka mbavu zinauma,pua hazipitishi hewa na anashindwa kupumua anahangaika ufanyeje

Asante.
 
Epukeni pia kushea nae vitu vinavyotumika midomoni ili kuepusha maambukizi kwa wengine sababu haijajulikana kama ni bakteria au virus ndio chanzo,

Mazingira pia yanayomzunguka yawe safi na salama, mshauri abadili mswaki kama bado anatumia aliotoka nao Dar au tangu anunue huko bado anao tu,
 
Mkuu unafikiri mswaki ndo unaweza kuwa tatizo kweli
 
Achukue asali achanganye na karafuu pamoja na kitunguu maji (hicho kitunguu asikikate vipande vidogo vidogo sana na karafuu azitie kwenye asali zikiwa nzima) halafu awe anatumia hiyo asali kijiko kimoja cha chai mara 3 kwa siku,baada ya wiki moja ataona mabadiliko kwa uwezo wa Mungu.
 
Asante sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…