Naombeni Ushauri wenu please

Naombeni Ushauri wenu please

Joined
Sep 26, 2014
Posts
12
Reaction score
1
*Habari zenu wana Jf

*mimi ni kijana mdogo kabisa mwenye elimu ya form 4b ninaeishi Daressalaam..

*Nina mtaji wa milioni mbili ila nimeshindwa kupata Idea yoyote ya business ambayo itanilipa vizuri na kuendelea kuniweka mjini.

*Humu ndani najua kuna watu wana nia ya kusaidia,hivyo naombeni ushauri wenu kabla wazee wa boxer hawajanikwapua....!!
 
Kuwa wakala wa m pesa ama wa ges za mtungi kwa mtaj wako unatosha ama kama una eneo fanya ufugaj wa kuku unalipa ukizatia madawa, chango n.k
 
Kuwa wakala wa m pesa ama wa ges za mtungi kwa mtaj wako unatosha ama kama una eneo fanya ufugaj wa kuku unalipa ukizatia madawa, chango n.k

*mambo ya uwakala Big no,kutokana na uhalifu wa mitandaoni uko juu sana sasa na kuhusu ufugaji kuku naona wazo zuri ila eneo sina kabisa.

*Asante kwa ushauri.
 
Kijana nakushauri rudi kijijini kwenu ukaanzishe biashara ya vyakula ukusanye kwa jumla kisha utafute eneo uuze.Utatoka baada ya muda hutaamini!,na kama dar ndio kwenu kabisa basi nenda maeneo ya kawe ama mbagala fanya hiyo akili niliyokupa utatoka
 
Hongera kwa kuweza kukusanya na kuhifadhi hiyo kilo mbili. Nakushauri ununue vipande vya umoja 4400 kwa shs 2Mil kisha rudia njia ile ile iliyokuwezesha kupata hiyo 2Mil kwa mwaka au miwili hivi kwa vyovyote katika kipindi hicho utapata wazo zuri la kibiashara kuliko sasa wakati hiyo pesa bodo ya moto na wewe hujajua ufanye nini. Kila la kheri.
 
Kijana nakushauri rudi kijijini kwenu ukaanzishe biashara ya vyakula ukusanye kwa jumla kisha utafute eneo uuze.Utatoka baada ya muda hutaamini!,na kama dar ndio kwenu kabisa basi nenda maeneo ya kawe ama mbagala fanya hiyo akili niliyokupa utatoka

Mie sina kijiji,mwenyeji wa hapahapa dar...
Asante kwa ushauri wako ila wazo lako naona haliendani na mtaji wangu.
 
Hongera kwa kuweza kukusanya na kuhifadhi hiyo kilo mbili. Nakushauri ununue vipande vya umoja 4400 kwa shs 2Mil kisha rudia njia ile ile iliyokuwezesha kupata hiyo 2Mil kwa mwaka au miwili hivi kwa vyovyote katika kipindi hicho utapata wazo zuri la kibiashara kuliko sasa wakati hiyo pesa bodo ya moto na wewe hujajua ufanye nini. Kila la kheri.

Hii milioni mbili nmeipata baada ya kuuza kijishamba changu ambacho kilikua kina mgogoro...
kwa hio siwezi kupata 2m kwa njia ya mwanzo...
 
*Habari zenu wana Jf

*mimi ni kijana mdogo kabisa mwenye elimu ya form 4b ninaeishi Daressalaam..

*Nina mtaji wa milioni mbili ila nimeshindwa kupata Idea yoyote ya business ambayo itanilipa vizuri na kuendelea kuniweka mjini.

*Humu ndani najua kuna watu wana nia ya kusaidia,hivyo naombeni ushauri wenu kabla wazee wa boxer hawajanikwapua....!!

Nunua guta(tricycle) 3@600,000 tafuta vijana unao waamini, hesabu ni 10,000-15,000 ingawa yeye atakunja kama 40,000/siku,kwa hiyo
30-45/kwa siku =900,000-1350000/mwezi unaishi kabisa
 
Nunua guta(tricycle) 3@600,000 tafuta vijana unao waamini, hesabu ni 10,000-15,000 ingawa yeye atakunja kama 40,000/siku,kwa hiyo30-45/kwa siku =900,000-1350000/mwezi unaishi kabisa
Hii nimeipenda sana Unataka kuniambia Guta zile za Toyo ni shs Laki 600,000/- moja or cjaelewa?Na ahapa Dar naweza kwenda kununua kesho wapi?Maana nna kijana anafanyaga usafi tu ningepatia hilo ingefaa sanaa
 
Back
Top Bottom