Naongea na mwenye mbwa siongei na mbwa

Naongea na mwenye mbwa siongei na mbwa

Visasi vipo mpaka kwenye ikulu ya Donald Trump kule Marekani. Au unasahau kuwa mwenye visasi ni mkristo au pengine muislam, mtu ambaye hukumbushwa kutubu dhambi zake?.

Nitajie kiongozi yoyote yule wa kitanzania kuanzia Mwalimu JKN mpaka hivi leo ambaye hana chembe ya ushahidi wa uwepo wa visasi kwenye hulka zake.
Mkuu kwani mie nimezungumzia viongozi? Wewe ndiye uliyeleta mfano wa mbwa kawa mwenye mbwa na sasa ana wapiga hata wale waliomwita mbwa. Ndio nikakukumbusha kuwa,kama mbwa imewezekana kugeuka kuwa mwenye mbwa basi uwezekano wa kurudi tena kuwa mbwa upo! Na sio mbwa bora bali mbwa koko anayejitafutia ridhiki jalalani.
 
Mkuu kwani mie nimezungumzia viongozi? Wewe ndiye uliyeleta mfano wa mbwa kawa mwenye mbwa na sasa ana wapiga hata wale waliomwita mbwa. Ndio nikakukumbusha kuwa,kama mbwa imewezekana kugeuka kuwa mwenye mbwa basi uwezekano wa kurudi tena kuwa mbwa upo! Na sio mbwa bora bali mbwa koko anayejitafutia ridhiki jalalani.
Kwa uzoefu jinsi ulivyo, wanaporudi kwenye maisha ya kawaida, hakuna anayewagusa. Walipiga kelele wakasema BWM apandishwe kizimbani, mpaka leo hii kiko wapi?.

Walipiga kelele wakasema Mkwere apandishwe kizimbani, mpaka leo kiko wapi?. Mwache mwenye mbwa wa sasa ainyooshe nchi, awatumikie wanyonge. Hivi vinyongo kaeni navyo mioyoni mwenu.
 
Kwa uzoefu jinsi ulivyo, wanaporudi kwenye maisha ya kawaida, hakuna anayewagusa. Walipiga kelele wakasema BWM apandishwe kizimbani, mpaka leo hii kiko wapi?.

Walipiga kelele wakasema Mkwere apandishwe kizimbani, mpaka leo kiko wapi?. Mwache mwenye mbwa wa sasa ainyooshe nchi, awatumikie wanyonge. Hivi vinyongo kaeni navyo mioyoni mwenu.
Ni swala la wakati tuu, hivi unadhani BWM na huku kuwaita wengine wapumbavu mabadiliko yakitokea ambaye siye akawa ndiye atapona? tusiweke akilini kuwa ccm itakuwepo daima.
Mfano mzuri ni election ya 2015, angalia pamoja na nguvu ya dola, media kubanwa na msaada wa NEC na Returning officers nini kilitokea?
 
Ni swala la wakati tuu, hivi unadhani BWM na huku kuwaita wengine wapumbavu mabadiliko yakitokea ambaye siye akawa ndiye atapona? tusiweke akilini kuwa ccm itakuwepo daima.
Mfano mzuri ni election ya 2015, angalia pamoja na nguvu ya dola, media kubanwa na msaada wa NEC na Returning officers nini kilitokea?
Mkuu kwa nchi hii ccm wanapopoteza majimbo ujue ni ujinga wao wenyewe. Wanapojipanga ipasavyo na kutimiza majukumu yao, basi kwa kizazi cha tulio duniani, ni vigumu sana kupingana na wanachokifanya.

CCM haundwi na malaika, lakini ni chama ambacho watu wake wanapoongea huwa wanasikilizwa kwa umakini licha ya kashfa chafu zilizoikumba serikali haswa enzi za JK na huyo BWM.

Bado CCM inahesabiwa na wengi wenye kujielewa kama ni kitovu cha maadili na rejea ya masuala ya kiuongozi.
 
Hapana hapana hapana. Umekosea kabisa. Hata kama umeambiwa kutoka kwa malaika lakini kuna namna ungeweza ku-present thread yako na ikaeleweka. Wewe umeumba picha ya kuwa rais Magufuli yupo tayari kujibu mapigo kwa sababu aliambiwa msemo ambao haukumpendeza tena siku za nyuma! Hapa ni kama unamweka rais kwenye kundi la walipa kisasi. Ungeweza tu kusema jamaa ana kosa A na una fununu kuwa atatumbuliwa siku za karibuni. Na labda ungeweza kukumbushia mwishoni kuwa ''mnakumbuka huyu ndiye aliyekuwa na jeuri ya kusema blah blah blah siku za nyumba!

Jaribu kurudia tena maandishi yako:
Shombe shombe yupo kwenye wakati mgumu, kwani huyu mwenye mbwa wa sasa, anafahamu fika dharau aliyokutana nayo wakati akiwa kazini katika wizara ya barabara.

Nyeti zinahabarisha kwamba mwenye mbwa yupo njiani kuandaa mapigo yatakayorudisha heshima aliyoipoteza baada ya kudharauliwa mpaka kufananishwa na dogi.
Haya sasa raisi kampinga za chembe huyo kabachori wenu wa kihindi
 
Huyu anaezungumziwa si bwana YUSUPH MANJI au sio yeye

Sent from my TECNO L9 Plus using JamiiForums mobile app
 
Mwenyekiti wa kamati ya kuleta wachezaji klabuni

Hapa inabidi kuzungumzia sports, kwisha. Kuchanganya issue za personal record ambazo serikali makini ya Tanzania ilishamalizana naye na anafanya shughuli za maendeleo ni makosa. Kuna wengi waliokuwa na makosa na tuhuma zinafonana na hizo na leo hii ni raia wema na wanapewa heshima zao.

In other words hakuna urafiki au uadui wa kudumu kwenye siasa, ndiyo maana waliachiwa, na hata Zanzibar kulishakuwa na serikali ya CCM na CUF unless watu wamesahau. Wa Tz, tuwe juu ya level hizi! Huyo mnamwita mhaini mnajua Baba yake alipoteza maisha katika mazingira gani? na alifanya nini kwa taifa? Halafu mabo ya shombe n.k. si ya kitanzania.

Yaani mnataka kumchonganisha na viongozi wa juu! kisa nini! usajili wa 2017! si na ile timu ilisema inaweza kusajili mchezaji yeyote? tuzungumzie michezo hizo nyingine ni rafu na ni aibu.
 
Dharau mbaya sana, hata mtu usiyemfahamu huwezi kumwambia vile, acha apate habari yake, kwanza ni mkwepaji wa kodi mkubwa sana nchini, ataipata fresh...
 
Dharau mbaya sana, hata mtu usiyemfahamu huwezi kumwambia vile, acha apate habari yake, kwanza ni mkwepaji wa kodi mkubwa sana nchini, ataipata fresh...
Unamzungumzia Nani

Nahisi umeenda chaka
 
Kauli za kibaguzi hazifai, kwani ukimwandika jina lake unapungukiwa nini? Fuatilia huyo chotara miaka ya nyuma aliifanyia nini Tanzania,
Hans Pope
Pamoja na hayo ndio amwite mwingine mbwa?
 
Acheni kuandika kiumbembea, huyu mtu anaitwaa hance pope. Dini inatufundisha kusamehe saba mara sabini. Magufuli sii mjahaidina, magufuli ni mkristo safi.
Mawazo yenu nyinyi wachonganishi, hayapo kwa magufuli.
Hivi kosa la Manji walijua?
Kwanini asisamehewe?
 
Hivi hii ni habari ya michezo na burudani?naomba sample ya mkojo wako mleta thread hii!
 
Back
Top Bottom