Nape amkana Kinana

Nape amkana Kinana

Kinana alichosema ni kuwa si rahisi kutengeneza Katiba itakayo mridhisha kila mtu hivyo CCM kama chama yatakuwepo tunayoyaunga mkono na mengine tunaweza kuwa na ushauri tofauti lakini tusibiri kikao cha Kamati Kuu kinakutana jtatu tutakuwa na msimamo wa taasisi. Namimi nikarudia hapo hapo. Nilichosahihisha ni dhana kuwa CCM inapinga rasimu mia kwa mia, sio sahihi! CCM haipingi rasimu ya Katiba bali inaweza kuwa na maoni tofauti kwa baadhi ya mambo!
Nape

mheshimiwa kuna thread moja kuhusu mbinga umeipitia?
Japo nakushauri umalize kwanza shughuli zako zote humu ndani maana ukiisoma tu lazima ulog out!
 
kamati kuu ya ccm kukutana kujadili rasimu ndo nini! ina maana inataka kuwa influence wanachi kuhusu hiyo rasimu? ninachojua katiba itajadiliwa kwenye mabaraza ya katiba haiwezekani chama kikurupuke na kusema hadharani kuwa haikubali rasimu. ingawa huwa nampinga Nape wakati fulani hapa yuko sahihi na Kinana kakurupuka. kinana angetoa maoni yake binafsi kama alivyofanya Sumaye
Wewe nawe uko biased, mmoja kasema haiungi mkono asilimia 100 (Kinana) mwingine kasema anaikubali (Nape). Wote wameyatamka haya hadharani, iweje mmoja awe sahihi na mwingine asiwe sahihi kwa mujibu wako? KCCM wameshaitaarifu Tume kwamba wataunda Baraza la Katiba ili watoe maoni yao, na nijuavyo maoni hayo hayapaswi kuwa siri. Ndiyo maana wanakutana.
 
Nahisi anakaugonjwa kanaitwa chademanism hivyo,kila akiitwa au kuulizwa swali huhisi kama vile cdm wamemwiliza!
 
nilisha tabiri kuwa ccm watakua kama kanu ya kenya kipindi moi alikuwa anamaliza muda wake pale ambapo tulishuudia wana kanu wengine walipoungana na kuunda narc,hili nalo naona kwa ccm watagawanyika vikundi vikundi ndo itakuwa mwisho wa ccm.RIP CCM.
 
Kinana alichosema ni kuwa si rahisi kutengeneza Katiba itakayo mridhisha kila mtu hivyo CCM kama chama yatakuwepo tunayoyaunga mkono na mengine tunaweza kuwa na ushauri tofauti lakini tusibiri kikao cha Kamati Kuu kinakutana jtatu tutakuwa na msimamo wa taasisi. Namimi nikarudia hapo hapo. Nilichosahihisha ni dhana kuwa CCM inapinga rasimu mia kwa mia, sio sahihi! CCM haipingi rasimu ya Katiba bali inaweza kuwa na maoni tofauti kwa baadhi ya mambo!
Nape
Nape, chonde chonde hakikisha aidha ni serikali moja au tatu. Ni uhaini wa Tanzania Bara kukubali kuwa na serikali mbili. Tunasubiri kwa hamu tamko la jumatatu. Naona Wazeanji wamesituka na sasa hawataki serikali tatu. Mtoto akililia wembe mpe, walilikoroga acha walinywe ila CCM yetu unafiki na kuwakumbatia wazenji. Mkipitisha serikali mbili, jua CCM tutaonekana majuha
 
Kati ya Kinana na Nape nani kiongozi wa mwenzake. I thought Nape was answerable to Kinana? If that is the case how dare Nape utter those words. Chama kinapoteza mwelekeo.

Kama baraza la mawaziri linaweza kutofautiana kauli, hicho ni kituko kidogo sana.
 
KATIBA SIO MALI YA CCM WALA CHADEMA NI MALI YA WATANZANIA,MBONA MNATAKA TUTUKANE TUPIGWE BAN NYIE WANA SIASA?.KUWENI SERIOUS YEYOTE AMBAYE A TAPINGA RASIMU HII KWA LENGO LA KUIBOMOA TUTAPAMBANA NAE HATA KAMA NI CHADEMA ..a
mbona mnagombaniana kitu cha kwetu wote.. tafuteni katiba yenu watanganyikaaaaaaaaaaaaaa.. hamna nyumba mnatapa tapa...
 
Tunawataka wanasiasa wasitusemee sisi wananchi, watuache tutoe maoni yetu wenyewe bila kushawishiwa!
 
Katika mahojiano na Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Nape kapingana na katibu wake ambaye hapo awali alidai kuwa wanaitisha kikao cha dharura kuijadili rasimu ya katiba mpya kwa maana hawajakubaliana nayo kama chama. Lakini Nape kadai yeye alishasema kuwa anakubaliana na rasimu hiyo na alishawapongeza kina Jaji Warioba kamalizia kuwa hayo maneno ya kutokubaliana nayo ni ya mitaani kwa vile yeye ndo msemaji wa chama chao.

Source: BBC

--------------------- Ufafanuzi wa Ndg Nape Nnauye.

Nape kazi yako sasa ni kukanusha kilichosemwa na wakuu wako.
 
Back
Top Bottom