Nape ataka "faili" la Rose Muhando

Nape ataka "faili" la Rose Muhando

Khaaaaaa !!!!!! Rose atapata dhambi hataki kumuimbia Mungu ???
 
Hawa Msama ndio watakuwa matapeli
wenyewe haiwezekani kitu cha aina moja kinajirudia Mara kwa Mara.

A
Nape.jpg


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametaka kupewa maelezo maalum ya kimaandishi juu ya mwenendo wa mwimbaji wa nyimbo za Injili, Rose Muhando ili aweze kuchunguza madai ya utapeli yanayosemwa juu yake.

Nape alitoa kauli hiyo baada ya kuulizwa endapo atafanyia kazi tuhuma zilizotolewa na waandaaji wa Tamasha la Pasaka la kila mwaka, Msama Promotions, waliodai mwimbaji huyo hakutokea jukwaani, licha ya kupewa malipo yake na stahiki zingine zilizostahili.

rose_muhando.jpg


“Kwanza ieleweke kuwa mimi sikuambiwa, ila nilisikia wakiwatangazia watu waliokuwepo uwanjani juu ya kutokuwepo kwa Rose kwenye tamasha hilo. Sasa mimi siwezi kufanya kazi kwa maneno ya mtaani, kama kuna wasanii wanatapeli, niletewe maelezo kimaandishi yakiwa na ushahidi wa tuhuma zao, hapo ndipo nitaweza kujua hatua za kuchukua,” alisema.

Awali, ofisa mmoja wa Msama Promotions aliyeomba hifadhi ya jina lake kwa kuwa siyo msemaji, alisema Rose alikuwa amepewa malipo yote, ikiwa ni pamoja na usafiri wa gari la kumtoa Dodoma hadi Mwanza, lakini hakuweza kutokea katika onesho hilo.

“Tulishamalizana na Rose na kila mmoja alijua atakuwepo, lakini tunashangaa mara ya mwisho hapatikani kwenye simu na hatujui kapatwa na masaibu gani,” alisema ofisa huyo.

Source: Naniliu
 
Maskini huyu mama sijui anayo yapitia, alikuwa anaeleweka ila sijui dhoruba gani imemkumba. Mungu amsaidie aione njia tena
Hamna cha dhoruba Bali Ni kiburi chake tu usiweke maslahi mbele kwenye Kazi ya Mungu. Kiburi hiki shetani kawateka watumishi wengi Sana hasa waimbaji na baadhi ya wahubiri ukimsikia mwimbaji wa injili anadai milioni kadhaa ndio atokee kwenye kuinjilisha huyo ujue Ana pepo
 
Hamna cha dhoruba Bali Ni kiburi chake tu usiweke maslahi mbele kwenye Kazi ya Mungu. Kiburi hiki shetani kawateka watumishi wengi Sana hasa waimbaji na baadhi ya wahubiri ukimsikia mwimbaji wa injili anadai milioni kadhaa ndio atokee kwenye kuinjilisha huyo ujue Ana pepo
Ongea polepole mi nitakuelewa
 
Na huyu muheshimiwa akileta za kuleta mzingue vilevile....

Hajui kua uko kwy game toka kitambo......wanyoroshe hao Dada Rose hadi wakae sawa!
 
Tatizo ni kuifanya inayoitwa huduma ya Mungu biashara.
 
We Nape huyo Msama asikuzingue, mtumbue yeye anatumia jina la Rose kukusanya watu, si bure
 
We msama unamtafutia nini Rose muhando??hii sio mara moja kumchafua huyu dada halafu unamuharibia huku nthen mkikutana mnayamaliza kimya kimya jaribu kuwa na utu homeboy.
 
Huko kwenye hiyo Sanaa yapo mengi makubwa Zaidi ya huyo Rozi Mhando, labda aseme anataka amsogeze karibu yake zaid.
 
Nape awe makini na Msama Production, ni opportunists wakubwa hawa watu. Kama Rose Mhando ni tapeli kwanini wasitoe taarifa polisi? Waziri anahusikaje na kesi za utapeli? Kila mtu anatafuta ulaji na Rose Mhando inaelekea amechoka kuwa ngombe wa maziwa.

Msama kwa kugundua rais Magufuli anatoka Geita haraka haraka kapeleka tamasha la Pasaka Geita akitegemea Magufuli angekuwa huko wakati wa Pasaka ili ahudhurie.
 
Back
Top Bottom