Nape hajatania wala kukosea, huo ndiyo ukweli wenyewe

Nape hajatania wala kukosea, huo ndiyo ukweli wenyewe

Nape yupo sahihi hili pia alimjibu mtu twitter mwaka 2020
20240717_175736.jpg
 
Ingekuwa kwenye nchi ya kidemokrasia na inayoiishi demokrasia, Waziri Nape Nnauye angeshapoteza uwaziri na ubunge wake muda huu. Angepoteza kwa shinikizo la wananchi au kuondolewa na Rais aliyemteuwa. Lakini hapa kwetu, Nape bado anadunda na anakejeli kwa kusema eti amechakachuliwa video yake ya kule Bukoba.

Nape Nnauye amewahi kushika nafasi nyeti chamani-Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Taifa. Anajua kila jambo analolisema. Viongozi wa CCM hufundwa na kupikwa juu ya nini cha kusema; wapi pa kusema; lini useme; kwa jinsi gani useme na kwanini useme. Nape amesema akijua fika kuwa huo ndiyo ukweli wenyewe.

Nape anajua kuwa tunaelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa na ule mkuu mwakani. Ameanza, kwa kulewa madaraka na kujisahau kulikopitiliza, kuahidi kumpa ubunge Byabato wa Bukoba Mjini. Anaamini kuwa yeye anaweza kusema na kutenda lolote popote. Madaraka ya kulevya!

Waziri wa mgombea mtarajiwa wa Urais wa CCM-Mama Samia kusema vile kuna maana kubwa. Waziri wa tasnia ya habari akiisambaza habari kama ile ni jambo kubwa na la kuogofya. Kwamba, CCM hushinda kwakuwa ndiyo wanaohesabu kura na kutangaza matokeo. Hawashindi kwa kukubalika kwao na sera zao. Mambo mazito!

Mama Samia anafanya juhudi kubwa za kujipambanua kiutendaji na kikauli ili achaguliwe mwaka 2025 kama Rais wa Tanzania kupitia CCM. Nape anataka watanzania waamini kuwa juhudi zote za Mama Samia ni maigizo kwakuwa ana uhakika wa kutangazwa mshindi? Huu si uchochezi utoao machozi?

Nape amedhihirisha kwa umma wa watanzania mbinu chafu zinazoanzia kwenye chumba cha kuhesabu kura na wakati wa kutangazwa kwa matokeo. Wakati yeye akiwa Katibu wa Itikadi na Uenezi, mwaka 2012, mimi nilikuwa 'active' chamani na serikalini. Kwa uzalendo wangu, niliripoti jambo lifananalo na lake likitokea chamani mwaka huo: KIZOTA-Chumbani kuhesabu kura

Nape ameianika CCM yetu. Amekuwa mchochezi. Awajibishwe!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Nyegezi, Mwanza)

Pia soma

Huyu ni mpumbavu sana,kiukweli ni Bora ajiuzulu kuliko kusubiri afukuzwe ni aibu sana.
 
Watanzania tumezoea uongo uongo,ulaghai na utapeli kiasi kwamba mtu akisema ukweli, hatukubaliani naye.

Nape ni msemakweli (kwenye goli la mkono na uchaguzi) na kwa hili nampa kongole nyingi sana.

Ni nani asiyejua kuwa yaliyosemwa na Nape ndiyo yanayotokea!!??

Tunaomshambulia Nape maana yake tunaamini CCM wanashinda kihalali au tunaamini kuwa CCM hawaibi kura!

Mh. Rais aliposema kuwa hata wananchi wakipiga kura kwa vyama vingine, CCM ndiye atakayeunda serikali ni ukweli usio na hata chembe ya uongo.

Nape aliposema CCM itashinda kwa goli la mkono ni ukweli usio na shaka.

Nape anaposema kuna mbinu nyingi za kushinda uchaguzi, huu ni ukweli usio na chembe ya mashaka.

Kwa nini tunamlaumu kwa kuwa mkweli!!?
Kuwa mkweli ni dhambi ama kosa la jinai!!??

Mimi nilidhani kwa kauli hizi za ukweli kutoka kwa Samia na Nape, kama taifa, tulipaswa kukaa chini na kutafakari ni nini madhara ya ukweli huu kwenye mustakabali wa taifa na demokrasia.
Huyo unayemtetea keshaomba ladhi. Sasa wewe na Nepi nani MPUMBAVU?
 
Back
Top Bottom