Nape Nnauye: Hakuna Mtanzania amekamatwa kwa kukosoa Mkataba wa Bandari

Nape Nnauye: Hakuna Mtanzania amekamatwa kwa kukosoa Mkataba wa Bandari

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1692199116331.png

Waziri wa Nape Nnauye amesema kwamba hakuna Mtanzania yeyote aliyekamatwa ama anyeshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa sababu tu ya kukosoa mkataba wa uwekezaji wa bandari kati ya serikali ya Tanzania na Dubai kama ambavyo imekuwa ikitajwa na mashirika ya Kitaifa na Kimataifa.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Agosti 16, 2023, kufuatia kukamatwa kwa Balozi Dkt Willbrod Slaa, Mdude Nyagali pamoja na Wakili Boniface Mwabukusi, ambapo Waziri Nape amesema watu hao wamekamatwa kutokana na kauli zao zinazoashiria vitendo vya uvunjifu wa amani pamoja na kupanga maandamano ya kuiondoa serikali madarakani.
 
Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) limeshindwa kwenye kesi yake IPTL -Independent Power Tanzania Limited.

Hukumu hiyo imefikiwa mwisho wa wiki iliyopita ambapo World Bank tribunal (international centre for settlement of investment disputes.

ICSID imeamuru TANESCO kuilipa Standard Chartered Bank Hong Kong (SCB HK) kiasi cha dola za kimarekani milioni 148.40 pamoja na tozo riba.

SCB HK ndio walionunua mkopo wa IPTL kutoka bank ya Malaysia Danaharta kwa gharama ya dola za kimarekani milioni 76.1

Kwa habari zaidi soma the Guardian la leo:

My take.
Muda si mrefu tutasikia Tanzania yashindwa kesi na DP world yatakiwa kulipa trillioni 15.

Njia mpya iliyobuniwa na wajibu ndani ya serikali kuchota kodi za walala hoi, unasaini mkataba wa kijinga ambao ni kichaa tu anayeweza kuuvumilia alafu ukiulizwa unasema tumeshindwa kesi tulipeni tu.
 
Kunya anye kuku, akinya bata kaharisha....😕
 

Waziri wa Nape Nnauye amesema kwamba hakuna Mtanzania yeyote aliyekamatwa ama anyeshikiliwa na Jeshi la Polisi kwa sababu tu ya kukosoa mkataba...
Nape tumbo tumbo halina akili,mkuu wa mkoa Chalamila anasema wamekamatwa kwa kukosoa bandari,yeye anakuja na kipeperushi cha kujitetea na kumsagia kunguni utawala wa JPM.
 
Polisi wawakazie wanasiasa,kua kazi yao haihusiani na siasa,wao kazi yao ni kulinda raia na mali zao tu.
 
Back
Top Bottom