Course Coordinator
JF-Expert Member
- Jul 27, 2019
- 1,742
- 3,224
Ndio rais ni mtu Mkubwa Sana kumtusi ni sawa na kuhujumu uchumi, au wewe hujui? Au unajitoa ufaham? Unadani kumtukana rais wa nchi ni Jambo Dogo Kama unavyoweza kumtus jirani yako, kumtusi rais ni kuitus nchi mkuuu ndio maaana unaona kiongoz yoyote wa nchi nyingne akitusi nchi nyingne au kuikashfu anaambiwa aombe msamaha kwa nchi husika
x,Nape karibu tena kwenye kale kakikundi ketu ka kumsifu na kumuabudu Jiwe, tuliku-miss sana! Sasa ujitokeze hadhari kuunga mkono ile kauli ya kuwapiga mashangazi zetu ambayo enzi zile umetengwa kwenye haka ka kikundi ketu ka majuha tunaosifu na kuabudu uchizi wote wa awamu ya 5 kalikuumiza sana! Karibu sana comrade, majuha wenzako wa Lumumba tuliku-miss sana!
Jumba bovu limemuangukiaWanasiasa sio watu wa kuwaamini, alivyokua anaongea vile kwenye simu sijategemea kumuona akiomba msamaha
Wakudadavua huyu alisema mshamba kasamehewa, lakini yule aliyesema dictator uchwara, alininginizwa na kutupwa nje kabisa . Duniani kuna mamboMbunge wa Mtama Nape Nnauye amefika Ikulu jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kuomba msamaha. Ameomba msamaha na kusamehewa kosa aliliofanya miezi michache iliyopita.
Akizungumza akiwa nje ya Ikulu baada ya kuzungumza na Rais Magufuli, Nape Nnauye amesema "Kwanza nimekuja kumuona baba yangu lakini Mwenyekiti wa Chama changu, Rais wangu kwasababu wote mnajua mambo yaliyopita au kutokea hapo katikati na mimi kama mtoto wa CCM, kama mwanae, nimeona ni vizuri nije niongee na Baba yangu.
Nashukuru kwamba amenipa fursa ya kuja kumuona na ameniambia amenisamehe na amenipa ushauri na kwakweli kwa dhati ya moyo wangu nishukuru sana amenipa fursa kubwa sana."
Mbunge Nape anaendelea kusema "Kwa kweli Muheshimiwa Rais kama Baba yangu, kama mzazi wangu nashukuru sana kwa fursa uliyonipa kwa kunisikiliza, kwa kunisamehe, kunishauri, kunielekeza nifanye nini huko mbele ninapokenda."
Rais Magufuli amesma "Mimi nimeshamsamehe kwa dhati Nape, amekuwa akiandika 'message' nyingi sana za kuomba msamaha hata saa nane za usiku nimemuona huyu mtu akiomba msamaha'"
"Leo ameniomba hapa aje anione na kabla, amejaribu sana, ameenda kwa Mzee Mangula amefika hadi kwa Mzee Opson na Mama Nyerere, amehangaika kweli. Na kwamba sisi tumeumbwa kusamehe, na wewe umemuona asubuhi amekuja hapa nikasema siwezi kumzuia kumuona ngoja nimuone kwanza japo nilikuwa na kikao kingine na kikubwa" ameongeza Rais Magufuli
"Anachozungumza ni kwamba naomba Baba unisamehe, najua kusamehe kunaumiza lakini nasema kwa dhati kabisa nimemsamehe kabisa na anaeleza yaliyokuwa yanamsibu na baadhi ya watu waliokuwa wanamrubuni. Wengine wapo kwenye chama lakini nasema yote tumesamehe kwa sababu bado ni kijana mdogo na ana 'future' nzuri kwenye maisha yake."
"Nikiendelea kumshikilia kwenye moyo wangu, kwanza ni dhambi kubwa kwa mwenyezi Mungu na imeandikwa tusamehe saba mara sabini na Mungu amtangulie katika shughuli zake, akalee mke wake na familia yake, akakitumikie chama na akawatumikie wananchi wa jimbo lake." Amemalizia Rais Magufuli
Wakimalizia katika maongezi yao nje ya Ikulu, Rais Magufuli alimuuliza Nape "Kwa hiyo ulikuwa huna amani?"
Nape: Sana
Rais Magufuli: Uwe na amani na Mungu akusaidie
Pia soma;
Imevuja sauti inayodaiwa ni Maongezi ya Simu ya Nape Nnauye na Abdulrahman Kinana kuhusu njama za kuichafua CCM
Ni kuhusu barua iliyotolewa na Makamba na Kinana kuhusu kuchafuliwa na Musiba. Ni Maelekezo ya Kinana Kumtaka Nape aisambaza barua kwenye vyombo vya habari. Kinana: Mwambie bwana hawa jamaa wanatoa statement leo, Unafikiri tumpe nakala? [Nape: Hapana] Mwambie wanaiandaa Mzee wataitoa leo...www.jamiiforums.com
Kamanda kula limau tu hakuna namna!Kwani si aombe kimya kimya kwani ni lazima ipewe coverage kuubwa.
Pengine ndio adhabu yenyewe hiyoMbona ameshukia mbali na makaz ya Rais akaanza kutembea kwa miguu? Uku tunaonaga wageni wengine wanashushwa mbaka karibia na ngazi za kuingia ndani ikulu.
Sio mamlaka makubwa, bali anatumia vibaya mamlaka. Hamna asiye pingwa dunia hii, ila unapowakomoa kwa kuwaua kisiasa/ kimwili unayetofautiana naye kimtazamo ni kosa.Juzi nilicomment kwenye Uzi flani nikawaambia Rais ana mamlaka makubwa na hilo liko wazi, wengi mliwananga akina ngeleja kuomba msamaha Leo nape kwenda wazi wazi, nawambia tena Rais ana mamlaka makubwa kumtukana na kumsengenya ni kosa kubwa sn
Zamani nilwahi kuskia ya kutoka kwa askari Polisi ya kuwa ukitaka kummaliza nguvu mtu tajiri ni kumpiga pingu mbele ya hadhara.Polisi huyu alinihakikishia ya kuwa mtu huyo hata awe tajiri vipi nguvu zinamuishia.Mbunge wa Mtama Nape Nnauye amefika Ikulu jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kuomba msamaha. Ameomba msamaha na kusamehewa kosa aliliofanya miezi michache iliyopita.
Akizungumza akiwa nje ya Ikulu baada ya kuzungumza na Rais Magufuli, Nape Nnauye amesema "Kwanza nimekuja kumuona baba yangu lakini Mwenyekiti wa Chama changu, Rais wangu kwasababu wote mnajua mambo yaliyopita au kutokea hapo katikati na mimi kama mtoto wa CCM, kama mwanae, nimeona ni vizuri nije niongee na Baba yangu.
Nashukuru kwamba amenipa fursa ya kuja kumuona na ameniambia amenisamehe na amenipa ushauri na kwakweli kwa dhati ya moyo wangu nishukuru sana amenipa fursa kubwa sana."
Mbunge Nape anaendelea kusema "Kwa kweli Muheshimiwa Rais kama Baba yangu, kama mzazi wangu nashukuru sana kwa fursa uliyonipa kwa kunisikiliza, kwa kunisamehe, kunishauri, kunielekeza nifanye nini huko mbele ninapokenda."
Rais Magufuli amesma "Mimi nimeshamsamehe kwa dhati Nape, amekuwa akiandika 'message' nyingi sana za kuomba msamaha hata saa nane za usiku nimemuona huyu mtu akiomba msamaha'"
"Leo ameniomba hapa aje anione na kabla, amejaribu sana, ameenda kwa Mzee Mangula amefika hadi kwa Mzee Opson na Mama Nyerere, amehangaika kweli. Na kwamba sisi tumeumbwa kusamehe, na wewe umemuona asubuhi amekuja hapa nikasema siwezi kumzuia kumuona ngoja nimuone kwanza japo nilikuwa na kikao kingine na kikubwa" ameongeza Rais Magufuli
"Anachozungumza ni kwamba naomba Baba unisamehe, najua kusamehe kunaumiza lakini nasema kwa dhati kabisa nimemsamehe kabisa na anaeleza yaliyokuwa yanamsibu na baadhi ya watu waliokuwa wanamrubuni. Wengine wapo kwenye chama lakini nasema yote tumesamehe kwa sababu bado ni kijana mdogo na ana 'future' nzuri kwenye maisha yake."
"Nikiendelea kumshikilia kwenye moyo wangu, kwanza ni dhambi kubwa kwa mwenyezi Mungu na imeandikwa tusamehe saba mara sabini na Mungu amtangulie katika shughuli zake, akalee mke wake na familia yake, akakitumikie chama na akawatumikie wananchi wa jimbo lake." Amemalizia Rais Magufuli
Wakimalizia katika maongezi yao nje ya Ikulu, Rais Magufuli alimuuliza Nape "Kwa hiyo ulikuwa huna amani?"
Nape: Sana
Rais Magufuli: Uwe na amani na Mungu akusaidie
Pia soma;
Imevuja sauti inayodaiwa ni Maongezi ya Simu ya Nape Nnauye na Abdulrahman Kinana kuhusu njama za kuichafua CCM
Ni kuhusu barua iliyotolewa na Makamba na Kinana kuhusu kuchafuliwa na Musiba. Ni Maelekezo ya Kinana Kumtaka Nape aisambaza barua kwenye vyombo vya habari. Kinana: Mwambie bwana hawa jamaa wanatoa statement leo, Unafikiri tumpe nakala? [Nape: Hapana] Mwambie wanaiandaa Mzee wataitoa leo...www.jamiiforums.com
Umenena mkuu! nyuma ya keyboard wakiwa wameshiba ni mashujaa na watetezi wetu....njaa ikiyauma yanatembelea magoti na mikono vifuani kama wanaomba kazi kwa mhindi!Tweet za kujifanya shujaa nyingi na hatimaye matapishi yamekuwa chakula tena.
Maneno yako mazito japo umegusia aina moja ya "utekaji"Zamani nilwahi kuskia ya kutoka kwa askari Polisi ya kuwa ukitaka kummaliza nguvu mtu tajiri ni kumpiga pingu mbele ya hadhara.Polisi huyu alinihakikishia ya kuwa mtu huyo hata awe tajiri vipi nguvu zinamuishia.
Nikaja kusikia kwamba njia mojawapo ya kuvunja mtu kisaikolojia ni kumvua nguo zote abaki uchi wa mnyama.
Miaka ya karibuni tukasikia tena ya kuwa ukirekodiwa ukifanya jambo baya unakuwa mateka wa aliyeku rekodi.
Juzi juzi nikasikia kuwa njia mojawapo ya kumfanya mtu akose amani ni kumuonyesha kuwa unamfuatilia kwa kila jambo.
Kwa udukuzi uliofanyika na kuvujisha sauti ni lazima wote waishiwe nguvu na hakuna atakayeweza kusimama tena,wamekuwa mateka wataimba na kucheza kama itakavyoamriwa.
Hii ndiyo na hizo ndio siasa.