Nape Nnauye kama January Makamba, maji ya shingo yamfika. Amuangukia Rais Magufuli baada ya kumnanga

Nape Nnauye kama January Makamba, maji ya shingo yamfika. Amuangukia Rais Magufuli baada ya kumnanga

Mwaka huu hautaisha ataulamba tena uwaziri, kuna mtu amechuja sana kwenye wizara moja hivi ,wale wapumbavu wa katibu wa CCM wote wanaenda kuomba msamaha,MAGUFULI KURA ZAKE 25% ZIPO MTWARA NA LINDI ,AMEONA WAOMBANE MSAMAHA YAISHE AENDELEE KUKUBARIKA ,NAPE NAE 2020 KAONA ASIISHIE TU UBUNGE WA MSIMU MMOJA ....
 
Ndio rais ni mtu Mkubwa Sana kumtusi ni sawa na kuhujumu uchumi, au wewe hujui? Au unajitoa ufaham? Unadani kumtukana rais wa nchi ni Jambo Dogo Kama unavyoweza kumtus jirani yako, kumtusi rais ni kuitus nchi mkuuu ndio maaana unaona kiongoz yoyote wa nchi nyingne akitusi nchi nyingne au kuikashfu anaambiwa aombe msamaha kwa nchi husika

Kwa Africa mtawala ni mungu MTU nchi zilizoendelea kiongozi ni mtumishi wa watu
 
Nape karibu tena kwenye kale kakikundi ketu ka kumsifu na kumuabudu Jiwe, tuliku-miss sana! Sasa ujitokeze hadhari kuunga mkono ile kauli ya kuwapiga mashangazi zetu ambayo enzi zile umetengwa kwenye haka ka kikundi ketu ka majuha tunaosifu na kuabudu uchizi wote wa awamu ya 5 kalikuumiza sana! Karibu sana comrade, majuha wenzako wa Lumumba tuliku-miss sana!
x,
Mwenye final say Kwenye Chama chetu ni chairperson .
 
Kwani si aombe kimya kimya kwani ni lazima ipewe coverage kuubwa.
 
Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye amemuomba msamaha Rais John Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam kwa kile alichoeleza kuwa siku za hivi karibuni yametokea mambo mengi.

Waziri huyu wa zamani wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amefunga safari hadi Ikulu Dar es Salaam kuonana na Rais Magufuli ambapo leo ndipo wamekutana na kuzungumza.

"Nimekuja kumuona kwa sababu mnajua mambo yaliyopita, hapa katikati kumetokea mambo mengi. Mimi kama mtoto wa CCM nimeona ni vizuri nije niongee na Baba yangu na nina shukuru amenisamehe na amenipa ushauri," amesema.

Kwa upande wake Rais Magufuli amesema, "Na mimi nimeshamsamehe kwa dhati, Nape amekuwa akiandika hata meseji nyingi hata usiku wa manane akiomba msamaha, unamuona kabisa huyu mtu anaomba msamaha".

 
Mbunge wa Mtama Nape Nnauye amefika Ikulu jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kuomba msamaha. Ameomba msamaha na kusamehewa kosa aliliofanya miezi michache iliyopita.


Akizungumza akiwa nje ya Ikulu baada ya kuzungumza na Rais Magufuli, Nape Nnauye amesema "Kwanza nimekuja kumuona baba yangu lakini Mwenyekiti wa Chama changu, Rais wangu kwasababu wote mnajua mambo yaliyopita au kutokea hapo katikati na mimi kama mtoto wa CCM, kama mwanae, nimeona ni vizuri nije niongee na Baba yangu.

Nashukuru kwamba amenipa fursa ya kuja kumuona na ameniambia amenisamehe na amenipa ushauri na kwakweli kwa dhati ya moyo wangu nishukuru sana amenipa fursa kubwa sana."



Mbunge Nape anaendelea kusema "Kwa kweli Muheshimiwa Rais kama Baba yangu, kama mzazi wangu nashukuru sana kwa fursa uliyonipa kwa kunisikiliza, kwa kunisamehe, kunishauri, kunielekeza nifanye nini huko mbele ninapokenda."

Rais Magufuli amesma "Mimi nimeshamsamehe kwa dhati Nape, amekuwa akiandika 'message' nyingi sana za kuomba msamaha hata saa nane za usiku nimemuona huyu mtu akiomba msamaha'"

"Leo ameniomba hapa aje anione na kabla, amejaribu sana, ameenda kwa Mzee Mangula amefika hadi kwa Mzee Opson na Mama Nyerere, amehangaika kweli. Na kwamba sisi tumeumbwa kusamehe, na wewe umemuona asubuhi amekuja hapa nikasema siwezi kumzuia kumuona ngoja nimuone kwanza japo nilikuwa na kikao kingine na kikubwa"
ameongeza Rais Magufuli

"Anachozungumza ni kwamba naomba Baba unisamehe, najua kusamehe kunaumiza lakini nasema kwa dhati kabisa nimemsamehe kabisa na anaeleza yaliyokuwa yanamsibu na baadhi ya watu waliokuwa wanamrubuni. Wengine wapo kwenye chama lakini nasema yote tumesamehe kwa sababu bado ni kijana mdogo na ana 'future' nzuri kwenye maisha yake."

"Nikiendelea kumshikilia kwenye moyo wangu, kwanza ni dhambi kubwa kwa mwenyezi Mungu na imeandikwa tusamehe saba mara sabini na Mungu amtangulie katika shughuli zake, akalee mke wake na familia yake, akakitumikie chama na akawatumikie wananchi wa jimbo lake."
Amemalizia Rais Magufuli

Wakimalizia katika maongezi yao nje ya Ikulu, Rais Magufuli alimuuliza Nape "Kwa hiyo ulikuwa huna amani?"

Nape: Sana

Rais Magufuli: Uwe na amani na Mungu akusaidie

Pia soma;
Wakudadavua huyu alisema mshamba kasamehewa, lakini yule aliyesema dictator uchwara, alininginizwa na kutupwa nje kabisa . Duniani kuna mambo
 
Mbona ameshukia mbali na makaz ya Rais akaanza kutembea kwa miguu? Uku tunaonaga wageni wengine wanashushwa mbaka karibia na ngazi za kuingia ndani ikulu.
Pengine ndio adhabu yenyewe hiyo
 
Kupambana na utawala si kitu mchezo.

Walikuwa wanafikiri sisi tunaonyanyaswa na chama tawala tunaraha!

Lazima ujitoe muanga kutetea wananchi hasa utawala huu.

Kwa hiyo korosho sasa zinakosa watetezi, bado Mwantumu.

Kutetea watu ambao hawajitambui siyo kitu mchezo.

POLENI SANA KWA KUJARIBU KAZI ZETU,
 
Juzi nilicomment kwenye Uzi flani nikawaambia Rais ana mamlaka makubwa na hilo liko wazi, wengi mliwananga akina ngeleja kuomba msamaha Leo nape kwenda wazi wazi, nawambia tena Rais ana mamlaka makubwa kumtukana na kumsengenya ni kosa kubwa sn
Sio mamlaka makubwa, bali anatumia vibaya mamlaka. Hamna asiye pingwa dunia hii, ila unapowakomoa kwa kuwaua kisiasa/ kimwili unayetofautiana naye kimtazamo ni kosa.
 
Mbunge wa Mtama Nape Nnauye amefika Ikulu jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kuomba msamaha. Ameomba msamaha na kusamehewa kosa aliliofanya miezi michache iliyopita.


Akizungumza akiwa nje ya Ikulu baada ya kuzungumza na Rais Magufuli, Nape Nnauye amesema "Kwanza nimekuja kumuona baba yangu lakini Mwenyekiti wa Chama changu, Rais wangu kwasababu wote mnajua mambo yaliyopita au kutokea hapo katikati na mimi kama mtoto wa CCM, kama mwanae, nimeona ni vizuri nije niongee na Baba yangu.

Nashukuru kwamba amenipa fursa ya kuja kumuona na ameniambia amenisamehe na amenipa ushauri na kwakweli kwa dhati ya moyo wangu nishukuru sana amenipa fursa kubwa sana."



Mbunge Nape anaendelea kusema "Kwa kweli Muheshimiwa Rais kama Baba yangu, kama mzazi wangu nashukuru sana kwa fursa uliyonipa kwa kunisikiliza, kwa kunisamehe, kunishauri, kunielekeza nifanye nini huko mbele ninapokenda."

Rais Magufuli amesma "Mimi nimeshamsamehe kwa dhati Nape, amekuwa akiandika 'message' nyingi sana za kuomba msamaha hata saa nane za usiku nimemuona huyu mtu akiomba msamaha'"

"Leo ameniomba hapa aje anione na kabla, amejaribu sana, ameenda kwa Mzee Mangula amefika hadi kwa Mzee Opson na Mama Nyerere, amehangaika kweli. Na kwamba sisi tumeumbwa kusamehe, na wewe umemuona asubuhi amekuja hapa nikasema siwezi kumzuia kumuona ngoja nimuone kwanza japo nilikuwa na kikao kingine na kikubwa"
ameongeza Rais Magufuli

"Anachozungumza ni kwamba naomba Baba unisamehe, najua kusamehe kunaumiza lakini nasema kwa dhati kabisa nimemsamehe kabisa na anaeleza yaliyokuwa yanamsibu na baadhi ya watu waliokuwa wanamrubuni. Wengine wapo kwenye chama lakini nasema yote tumesamehe kwa sababu bado ni kijana mdogo na ana 'future' nzuri kwenye maisha yake."

"Nikiendelea kumshikilia kwenye moyo wangu, kwanza ni dhambi kubwa kwa mwenyezi Mungu na imeandikwa tusamehe saba mara sabini na Mungu amtangulie katika shughuli zake, akalee mke wake na familia yake, akakitumikie chama na akawatumikie wananchi wa jimbo lake."
Amemalizia Rais Magufuli

Wakimalizia katika maongezi yao nje ya Ikulu, Rais Magufuli alimuuliza Nape "Kwa hiyo ulikuwa huna amani?"

Nape: Sana

Rais Magufuli: Uwe na amani na Mungu akusaidie

Pia soma;
Zamani nilwahi kuskia ya kutoka kwa askari Polisi ya kuwa ukitaka kummaliza nguvu mtu tajiri ni kumpiga pingu mbele ya hadhara.Polisi huyu alinihakikishia ya kuwa mtu huyo hata awe tajiri vipi nguvu zinamuishia.
Nikaja kusikia kwamba njia mojawapo ya kuvunja mtu kisaikolojia ni kumvua nguo zote abaki uchi wa mnyama.
Miaka ya karibuni tukasikia tena ya kuwa ukirekodiwa ukifanya jambo baya unakuwa mateka wa aliyeku rekodi.
Juzi juzi nikasikia kuwa njia mojawapo ya kumfanya mtu akose amani ni kumuonyesha kuwa unamfuatilia kwa kila jambo.
Kwa udukuzi uliofanyika na kuvujisha sauti ni lazima wote waishiwe nguvu na hakuna atakayeweza kusimama tena,wamekuwa mateka wataimba na kucheza kama itakavyoamriwa.
Hii ndiyo na hizo ndio siasa.
 
Nimetazama sana kwa jicho la tatu nimegundua yafuatayo
1. Nape amesoma siasa na ameelewa nyakati hizi ni pambio gani linafaa kuimbwa . Nape halisi tutanwona 2025 panapo majaliwa

2.Nape ameelewa kitakachofuata kwake ikiwa hatajishusha ni kufutwa katika historia ya siasa kwasababu utawala wa sasa hautaki mchezo mchezo maana yake amesoma nyakati

3.tumtazamie Nape akiwa mpole sana Bungeni na yawezekana akarudi kwenye baraza la mawaziri maana ametambua alichokuwa anakitenda na anaye mtendea sio wa kawaida na hataki utani.

4. Ni vema Nape abadilike kabisa isiwe season break tu



Je wewe umeona nini
 
Zamani nilwahi kuskia ya kutoka kwa askari Polisi ya kuwa ukitaka kummaliza nguvu mtu tajiri ni kumpiga pingu mbele ya hadhara.Polisi huyu alinihakikishia ya kuwa mtu huyo hata awe tajiri vipi nguvu zinamuishia.
Nikaja kusikia kwamba njia mojawapo ya kuvunja mtu kisaikolojia ni kumvua nguo zote abaki uchi wa mnyama.
Miaka ya karibuni tukasikia tena ya kuwa ukirekodiwa ukifanya jambo baya unakuwa mateka wa aliyeku rekodi.
Juzi juzi nikasikia kuwa njia mojawapo ya kumfanya mtu akose amani ni kumuonyesha kuwa unamfuatilia kwa kila jambo.
Kwa udukuzi uliofanyika na kuvujisha sauti ni lazima wote waishiwe nguvu na hakuna atakayeweza kusimama tena,wamekuwa mateka wataimba na kucheza kama itakavyoamriwa.
Hii ndiyo na hizo ndio siasa.
Maneno yako mazito japo umegusia aina moja ya "utekaji"
 
Back
Top Bottom