Nape Nnauye: Warioba haitendei CCM haki.

Nape Nnauye: Warioba haitendei CCM haki.

Waungwana si tuko kwenye mchakato wa katiba ya Taifa la Tanzania????????????? Mbona kuna CCM hapa???? Nakubaliana na yule mwanasiasa aliyesema "Watanzania tusidanganyike kwamba tutapata katiba mpya kupitia mchakato wa Chama Cha M...Hiki ni kiini macho kwetu"
 
Sasa naaanza kuelewa yale maoni ya yule mgombea, aliye enguliwa wakati wa uchaguzi wa mabaraza haya, kusema CCM wamepanga wapeleke watu wao!! nia ilikuwa ndo hii, kufanya maoni mengi ya chama, ili ionekane kuwa wajumbe wa mabaraza wengi (mfano) walitaka serikali tatu n.k kumbe behind the scene ni maoni ya CCM.

Kama hii katiba ni ya nchi na vyama vya siasa vinapaswa kuifuata, kwa nini wawatume wanachama wao na maoni ya chama? mimi nilifikiri ni bora waache wananchi waende na maoni yao, ili hata wao kama chama wajue nini wananchi wanataka, iwe hata rahisi kuandaa sera kulingana na maoni ya wananchi, hata kubari kura za reforandam ( vingine tutapiga maktaim)
NAPE na viongozi wote wa vyama vya siasa acheni kwanza watu wajadaili maoni yao, kisha ya chama mtapeleka wakati wenu ukifika
my 0.5cts
SP
 
Warioba na tume yake kiukweli inabidi itege sikio lake kwa umakini.
Kuna maoni mengi hayakuingizwa kwenye rasimu hii iliyoandaliwa.
Mchakato bado sana

Lakini sio hayo ya MACCM, kwani MACCM walishayatuma ofisini kwa Jaji, Na Inakera ukizunguka nchi nzima kila mjumbe akija hoja ni hiyohiyo tena, Copy and Paste.

Na hivi ndivyo walivyofanya wakati wa kura za kukubali vyama vingi, wakatuma mabalozi wa chama baada ya kuwapa maelekezo mwisho wake wakachakachua White Paper.
 
Kawakaririsha wajumbe kusoma barua aliyoitawanya tanzania nzima -- Barua ambayo hata tume ina-copy yake; huku ni kupoteza muda.

Jaji warioba umewakamata vilivyo.
 
CCM tumezoea sana kubebwa siku tusipobebwa tunalalamika sana.
Maoni yetu CCM (tena mabovu kabisa) tumeshampa Warioba sasa tuwaache wananchi nao watoe maoni yao.
CCM tunaogopa nini?
 
Nape juzi tu umemtukana mzee Warioba kuwa anaweka maoni ya Serikali tatu wakati anasubiri kufa,

Leo tena unalia na Warioba huyohuyo kuwa anakuoneeni,

Mwacheni mzee afanye kazi ya Watanzania salama na amalize na kulinda heshima yake na ya Taifa letu pia!
 
Dar es Salaam. Katibu wa Itikadi na Uenezi (Nec-CCM), Nape Nnauye, ametuhumu Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa haitendi haki kwa kuwazuia wajumbe wa Baraza la Katiba kusoma waraka wa chama hicho unaopinga baadhi ya mambo yaliyopo kwenye rasimu.

Nape alitoa shutuma hizo jana alipozungumza kwa njia ya simu, alibainisha kuwa viongozi wa Jukwaa la Katiba akiwamo Mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba, wanataka mapendekezo yaliyopo kwenye rasimu yapite yalivyo.

“Kwani kufanya hivyo wanazuia maoni ya wananchi, ingawa hatujawatuma kuusoma kwenye mapendekezo, lakini wana haki ya kuutumia wanavyojisikia,” alisema Nape.

Alisema wanajua wapo watu wachache wanaoupinga waraka huo wa CCM, lakini hawaelewi kwa sababu unahusu wanachama wao.

“Tume itende haki isikilize mawazo ya kila mtu, inachofanya sasa ni ubaguzi, wao wanatakiwa kusikiliza maoni siyo kutetea rasimu,” alisema.

Hivi karibuni vyombo vya habari viliripoti jinsi Jaji Warioba alivyokosoa wajumbe wa Mabaraza ya Katiba wanaokwenda na matamko au nyaraka za vyama, badala ya maoni ya wananchi waliowachagua.

MWANANCHI GAZETI

KWA SWALA LA KATIBA MPYA HALIKUWA SEHEMU YA ILANI YAO HIVYO LAZIMA WATAPINGA MENGI!!!! Hii inathibitishwa na kauli mbalimbali za viongozi wao kabla ya raisi kuwasikiliza cdm.
Hebu Tuone chache hapa :::::

Waziri Kombani adai wanaodai Katiba mpya ni watu 'wa barabarani'

Kauli ya Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani, kwamba wale wanaodai katiba mpya ni watu wa barabarani wasiokuwa na uelewa juu ya masuala hayo.
Akizungumza na gazeti dada la The Citizen, waziri huyo pia alisema hakuna umuhimu wa kuwapo katiba mpya na kwamba Serikali inaridhika na utaratibu uliopo wa kuifanyia katiba hiyo marekebisho ya mara kwa mara pindi umuhimu wa kufanya hivyo unapokuwapo. Alisema kuwa Serikali haiko tayari kuanzisha mchakato wa kuandika katiba mpya kwa sababu wanaodai kuwapo kwa katiba hiyo hawajapeleka maombi yao serikalini kwa maandishi.
Refer:www.ippmedia.com › Home › News

Mwanasheria mkuu apinga katiba mpya:::
WAKATI Mbunge wa Jimbo la Ubungo, Bw. John Mnyika akiwasilisha hoja binafsi ya mabadiliko ya katiba mpya, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema amesema kuwa haiwezekani kuandikwa upya na badala yake
kinachowezekana ni kuifanyia marekebisho iliyopo....by http://majira-hall.blogspot.com/2010/12/mwanasheria mkuu-apinga-katiba mpya

Kuna wengi zaidi walipinga nikiweka hapa hata kusoma itachosha. Niseme nimeamua kuweka hizo hapo za watu muhimu ili tuone wenyewe jinsi swala hili lisivyokubalika nao
Sasa kwa mantiki hii lazima zitatumiwa mbinu nyingi kuidhoofisha rasimu yenyewe.
Kibaya zaidi wajumbe waliopo kwenye manaraza wengi elimu ndogo kwa hiyo wanatoa maoni kama wamemezeshwa vile.
 
Dar es Salaam. Katibu wa Itikadi na Uenezi (Nec-CCM), Nape Nnauye, ametuhumu Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa haitendi haki kwa kuwazuia wajumbe wa Baraza la Katiba kusoma waraka wa chama hicho unaopinga baadhi ya mambo yaliyopo kwenye rasimu.

Nape alitoa shutuma hizo jana alipozungumza kwa njia ya simu, alibainisha kuwa viongozi wa Jukwaa la Katiba akiwamo Mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba, wanataka mapendekezo yaliyopo kwenye rasimu yapite yalivyo.

“Kwani kufanya hivyo wanazuia maoni ya wananchi, ingawa hatujawatuma kuusoma kwenye mapendekezo, lakini wana haki ya kuutumia wanavyojisikia,” alisema Nape.

Alisema wanajua wapo watu wachache wanaoupinga waraka huo wa CCM, lakini hawaelewi kwa sababu unahusu wanachama wao.

“Tume itende haki isikilize mawazo ya kila mtu, inachofanya sasa ni ubaguzi, wao wanatakiwa kusikiliza maoni siyo kutetea rasimu,” alisema.

Hivi karibuni vyombo vya habari viliripoti jinsi Jaji Warioba alivyokosoa wajumbe wa Mabaraza ya Katiba wanaokwenda na matamko au nyaraka za vyama, badala ya maoni ya wananchi waliowachagua.

MWANANCHI GAZETI
Kwenye RED “Tume itende haki isikilize mawazo ya kila mtu, lkn mh. Nape waraka wa CCM sio mawazo ya wanachama wa CCM, mmewapa waraka na kwa sababu ni vilaza wameingia nayo madesa(waraka) kwenye mabaraza. Na m/kiti wa tume alishasema mapema waacheni wananchi watoe maoni yao na si maoni ya vyama vya siasa.Mwanaccm huyu, sijui anaitwa Mateo Qaresi, "alieleza kuwa Serikali tatu haziwezi kuepukika na kuwataka wanasiasa wakiwamo wa CCM kuacha ushabiki".hii ni kutoka gazeti la mwananchi la leo. Watch out my friend, sio kila kitu ni siasa.
 
Tanzania kwanza sera za kushibisha matumbo yenu baadae. Nchi kwanza chama baadae.
 
MH. Nape angalia kikatuni hiki, ni aibu!!! Hivi wewe kwa busara yako unaona mlivyowafanyia wanachama wenu ni sahihi kweli? Kilicho hapo kwenye katuni ni reality. Acheni ujinga nyie watu.
toon.jpg
 
Back
Top Bottom