John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Waziri wa Habari, Nape Nnauye akiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam Media, Tindo Mhando, jana usiku walifika Hospitali ya Taifa Muhimbili Dar es Salaam kuwajulia hali waandishi wa habari wanne wa Azam waliopata ajali ya gari Mlima wa Kitonga, Iringa wakiwa safarini kwenda Mbeya.
Awali, majeruhi hao walipokelewa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuendelea na matibabu na wote hali zao zinaendelea vizuri.
Uwanjani hapo majeruhi hao walipokewa na viongozi waandamizi wa Azam Media Limited, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye na Mbunge wa Buchosa, Erick Shigongo.
Awali, majeruhi hao walipokelewa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kuendelea na matibabu na wote hali zao zinaendelea vizuri.
Uwanjani hapo majeruhi hao walipokewa na viongozi waandamizi wa Azam Media Limited, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye na Mbunge wa Buchosa, Erick Shigongo.