Napenda kufahamu maneno haya kwa Kisukuma na Nyamwezi

Sijawahi kusikia "Ntogwimasangu" ila "Ntogwiisangu".

Hapo naona kuna habari za wingi na umoja.

With isangu being umoja na masangu being wingi.

Imalamaseko I denotes umoja

Maganiko ma denote wingi.


Umukizungu: This Kiranga at his best! Umukisuma: Kiranga! Pamoja na kuwa katika Kisukuma hakuna "r" hivyo ilitakiwa kuwa Kilanga (Shilanga?)🙂
 

Muhya wane ... Demu Wangu (katika Kiswahili)!
Banhya bane ... Mademu wangu (Katika Kiswahili)!!
Banhya .... Totoz, hasa za porini, n.k
 
Sijawahi kusikia "Ntogwimasangu" ila "Ntogwiisangu".

Hapo naona kuna habari za wingi na umoja.

With isangu being umoja na masangu being wingi.

Imalamaseko I denotes umoja

Maganiko ma denote wingi.

Kama unataka kuunda neno moja basi itakuwa 'ntogwamasangu' ikimaanisha 'mpenda makande'.

Lakini kwenye Kisukuma hakuna umoja katika neno la makande.

Makande (kwenye Kisukuma) ni mass noun/ noncount noun.
 
Kama unataka kuunda neno moja basi itakuwa 'ntogwamasangu' ikimaanisha 'mpenda makande'.

Lakini kwenye Kisukuma hakuna umoja katika neno la makande.

Makande (kwenye Kisukuma) ni mass noun/ noncount noun.

Ninaungana na wewe. Hakuna umoja wa Makende katika Kisukuma. Kuna wingi "Masangu". Na hasa kwa kuwa Masangu ni chakula kinachotokana baada na mkusanyiko wa Vyakula/nfaka mbalimbali zikipikwa pamoja Mf. Mandege (Mahindi), Nshiili (Choroko), Ng'halanga (Karanga), Ndulu (Kwa kiswahili ???), n.k. na vikorombezwo vongonevyo kutegemea na uwepo. Hakuna umoja wa makande!
 

Yup, upo sahihi.

Ila hapo nilipopakoleza na rangi nyekundu pana utata kidogo:smile-big:.
 
Mwabeja nho bhagalu na bhagika, bhacheye na bhagobhobho, hiphop na wote!
nimefurahishwa na ushirik wenu. ama kweli Jf ni kisima cha burudani, shule na kuongeza maarifa.
KOMEJAGI BHADUGU BHANE.
 
Kama unataka kuunda neno moja basi itakuwa 'ntogwamasangu' ikimaanisha 'mpenda makande'.

Lakini kwenye Kisukuma hakuna umoja katika neno la makande.

Makande (kwenye Kisukuma) ni mass noun/ noncount noun.

Hilo "Ntogwiisangu" ni neno la kisukuma. Kulikkuwa na Daktari maarufu Muhimbili akiitwa Dr. Ntogwiisangu. Watoto.zake kina Makoye Ntogwiisangu na Fred "Saganda" Ntogwiisangu aliyeimba wimbo wa wimbo wa "Rafaeli" uliopata umaarufu kwa kuwa wimbo wa kwanza qa bongoflava kwa kuimbwa kwa Kiswahili cha lafudhi ya Kichagga.

Kumbuka pia Kisukuma kimegawanyika, Wanyantuzu mnaweza kuwa hamna maneno mengine yetu Wasukuma.

Sikiliza Rafaeli kwanza. Mtoto wa Kisukuma alivyofoji Uchagga mpaka unataka kuamini ni Mchagga.

https://ia600303.us.archive.org/24/items/Rafaeli/01-Raphael.mp3

Google "Ntogwisangu" uone majina kibao.

Duh, halafu madaktari wa Kisukuma siku hizo walikuwa wamejaa Muhimbili, ukitoka kwa Dr. Nyamageni juu unashuka chini kwa Dr. Ntogwiisangu.

Ukipinda kona kwa Dr. Masale.

I am just realizing that.
 

Inawezekana kweli ni neno la Kisukuma maana Kisukuma nacho kina lahaja zake. Kama mtu anatokea Mwanza au Shinyanga mjini au Kahama huko anaweza asiwaelewe kabisa Wanyantuzu wa Bariadi.

Hapa ndo nam-miss mshua maana aliandika vitabu kadhaa juu ya historia ya Wasukuma hususan Bakwimba. Enkwimba ndo 'lwimbo' wetu huo kwa upande wa mshua.

Sasa sijui hao Bakwimba walitokea pande za Mwanza ndo wakaenda mpaka huko Bariadi au sijui Wanyantuzu ndo walitawanyika wakaenda mpaka huko Kwimba.

Itabidi nirudie tena kuvisoma hivyo vitabu.
 

Kuna hadi kamusi kadhaa za Kiingereza na Kisukuma na Kiswahili na Kisukuma.

Najua wale Maryknoll Fathers walijitahidi sana katika kusaidia kutengeneza hizo kamusi.

Ila bongo ndo hivyo tena, watu wenye interest na mambo kama hayo ni wachache mno kiasi cha kupelekea kazi kama hizo kukusanya mavumbi tu kwenye library za wazee wetu.
 

Nasikiliza hiyo link ya audio niliyoitia hapo juu, it has a gospel slant, lakini kusikia wanaongea Kisukuma authentic tu kumenirudisha mbali sana.

If you get a min give it listen.

Najiona kama nimerudi nyumbani halafu kuna mami fulani anahubiri hivi.

Badogo bane, degelekagi....
 
Nyani Ngabu Shetani kisukuma anaitwaje?

Kwa kweli najua jina la shetani ila sasa hivi limenitoka!

Mungu ni sebha au liwelelo (hili pia linaweza kutafsirika kama dunia/ ulimwengu...katika muktadha wa mungu ndo inakuwa kama lidunia au liulimwengu lenye nguvu juu yetu sote)
 
Kwa kweli najua jina la shetani ila sasa hivi limenitoka!

Mungu ni sebha, liwelelo (hili pia linaweza kutafsirika kama dunia/ ulimwengu...katika muktadha wa mungu ndo inakuwa kama lidunia au liulimwengu lenye nguvu juu yetu sote)

Nimekuuliza kwa sababu nawasikiliza hawa watu wanamuita shetani "shetani".

Kitu kinachoweza kumaanisha kwamba katika kisukuma hakuna neno la shetani per se.

Kitu kinachoweza kumaanisha kwamba concept ya shetani ni foreign kwa Wasukuma. Kwa sababu kama ingekuwa indigenous ingekuwa na an indigenous name.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…