Napenda sana kula pweza, ila wauza pweza wa Dar asilimia 99 ni Wachafu na wala hawajui usafi ni nini

Ukifika ferry nina hakika hautokula samaki au hao wadudu
Mzee Usichokijua mimi mzawa wa mikoa ya mwambao, pweza nimeanza kumla niko mdogo, baada ya kujitegemea nimeishi, maeneo ya kunduchi jirani kabisa na kijiji cha kundichi pwani au, Kunduchi Beach hotel au chuo cha madini, hivyo mazingira ya bahari nayajua, pweza namjua tangu anapigwa mchangani, nakula chaza, mtamuonea kinyaa pweza.
 
Unapajua pale kariakoo wanapouza supu ya mangozi ya Ng"ombe au bugiruni pale wanauza mapupu? Nenda saizi ukaone nyomi lake
Ni bora ukaeleza kuna nini, unajua tunatofautiana majukumu, wengine kariakoo tunafika ila kufika maeneo hayo ni ngumu kulingana na jambo lilio nifikisha huko.
 
Ni kweli kabisa, ila Sio wauza pweza tu...kwa Dsm wafanyabiashara wengi ni WACHAFU, hata mama Ntilie na watu wa magengeni pamoja na wauza miwa

Sio kama Wafanyabiashara wa Moshi na Arusha

Chukieni mpaka mpasuke, ninyi ni wachafu
Moshi ? Una taka kusema wale wauza pweza,mihogo na vitu vingine pale karbu na mawezi primary chini ya stand mida ya jioni ni wasafi ? Usha waona vzuri lakini na ile population ya pale mida io
 
Ni bora ukaeleza kuna nini, unajua tunatofautiana majukumu, wengine kariakoo tunafika ila kufika maeneo hayo ni ngumu kulingana na jambo lilio nifikisha huko.
Mji una mambo mengi sana huu. Ulishawahi kuona chips zikimwagwa! Tuseme hazibaki! Zinapelekwa wapi???
 
Poleni sana, kwa mimi kuna level ya uchafu ikifika ndo itanishinda ila huo mdogo mdogo haunisumbui.
 
Nashauri kula uchafu mtaani si kitu kizuri japo hata huko nyumbani mkeo anaweza kukulisha uchafu pia!!
Asante 😳😳😳
 
Mimi ni mteja, nanunua kwa fedha ambazo wao, wanashida nazo, Sijalalamikia eti wanapunja mpaka nivue, usafi tu, kwa kuwa hawanawi wakishika pweza kwa kutumia uma kuna shida gani.
Nimetoa maoni yangu huku kama mteja samahani.
Nani kasema wanashida na pesa yako?

Ww unaye nunua ndiyo unashida na pweza zao ww kama unaona uchafu ni bora usinunue kuliko kuharibu biashara za watu.
 
Kanunue pweza mwenyewe ujitengeneze

Ova
 
Naomba hayo maeneo niwe naenda maana chef asili wananipiga sana

Ef sita kipande
 
Hapana shida Bei nazo zinakua juu mnoo,chakula Cha 2500 atauza 6000,chips yai 2500,wanauza elf ,4
Hizo za kwenye vioo ndo shida ilipo hapo
 
Kwani wamekulazimisha ununue pweza wao?
Kwahiyo hawa wengine wanaotoa maoni juu ya bidha fulani, huwa wanalazimishwa kununua, ila siyo mbaya unajua hata umri unaongeza uweo wa fikra.
 
Nani kasema wanashida na pesa yako?

Ww unaye nunua ndiyo unashida na pweza zao ww kama unaona uchafu ni bora usinunue kuliko kuharibu biashara za watu.
Umri wa mtu pia huongeza uwezo wa kifikiri, basi sawa.
 
Toka nimeumwa typhoid mwaka 2021 kutokana na kunywa michuzi na misupu ya pweza wa barabani sitamani kabisa kula pweza barabarani nitaenda feri kununua pweza fresh niende kupika nyumbani. mambo mengine tunajitakia kuyavaa magonjwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…