Napenda sana kula pweza, ila wauza pweza wa Dar asilimia 99 ni Wachafu na wala hawajui usafi ni nini

Napenda sana kula pweza, ila wauza pweza wa Dar asilimia 99 ni Wachafu na wala hawajui usafi ni nini

Ukifika ferry nina hakika hautokula samaki au hao wadudu
Mzee Usichokijua mimi mzawa wa mikoa ya mwambao, pweza nimeanza kumla niko mdogo, baada ya kujitegemea nimeishi, maeneo ya kunduchi jirani kabisa na kijiji cha kundichi pwani au, Kunduchi Beach hotel au chuo cha madini, hivyo mazingira ya bahari nayajua, pweza namjua tangu anapigwa mchangani, nakula chaza, mtamuonea kinyaa pweza.
 
Unapajua pale kariakoo wanapouza supu ya mangozi ya Ng"ombe au bugiruni pale wanauza mapupu? Nenda saizi ukaone nyomi lake
Ni bora ukaeleza kuna nini, unajua tunatofautiana majukumu, wengine kariakoo tunafika ila kufika maeneo hayo ni ngumu kulingana na jambo lilio nifikisha huko.
 
Ni kweli kabisa, ila Sio wauza pweza tu...kwa Dsm wafanyabiashara wengi ni WACHAFU, hata mama Ntilie na watu wa magengeni pamoja na wauza miwa

Sio kama Wafanyabiashara wa Moshi na Arusha

Chukieni mpaka mpasuke, ninyi ni wachafu
Moshi ? Una taka kusema wale wauza pweza,mihogo na vitu vingine pale karbu na mawezi primary chini ya stand mida ya jioni ni wasafi ? Usha waona vzuri lakini na ile population ya pale mida io
 
Ni bora ukaeleza kuna nini, unajua tunatofautiana majukumu, wengine kariakoo tunafika ila kufika maeneo hayo ni ngumu kulingana na jambo lilio nifikisha huko.
Mji una mambo mengi sana huu. Ulishawahi kuona chips zikimwagwa! Tuseme hazibaki! Zinapelekwa wapi???
 
Poleni sana, kwa mimi kuna level ya uchafu ikifika ndo itanishinda ila huo mdogo mdogo haunisumbui.
 
Nashauri kula uchafu mtaani si kitu kizuri japo hata huko nyumbani mkeo anaweza kukulisha uchafu pia!!
Asante 😳😳😳
 
Mimi ni mteja, nanunua kwa fedha ambazo wao, wanashida nazo, Sijalalamikia eti wanapunja mpaka nivue, usafi tu, kwa kuwa hawanawi wakishika pweza kwa kutumia uma kuna shida gani.
Nimetoa maoni yangu huku kama mteja samahani.
Nani kasema wanashida na pesa yako?

Ww unaye nunua ndiyo unashida na pweza zao ww kama unaona uchafu ni bora usinunue kuliko kuharibu biashara za watu.
 
Kanunue pweza mwenyewe ujitengeneze

Ova
 
Yapo maeneo baadhi ambayo wauzaji wamestaarabika usafi unazingatiwa at least.

Ila maeneo mengi hata mimi niliyoyaona wauzaji asilimia kubwa wako rough mno, nadhani hiyo inatokana na wateja wake alio watageti eneo hilo wengi wana falsafa za "we don't care"
Naomba hayo maeneo niwe naenda maana chef asili wananipiga sana

Ef sita kipande
 
Watanzania kiujumla wanapenda maeneo machafu,watu wengi waliofungua migahawa mizuri yenye mazingira masafi na mazuri wameishia kufunga biashara zao kwa kukosa wateja!! Ila ile migahawa michafu iliyopo kwenye mazingira machafu ndio watu wanajazana kupata huduma!! Watanzania wengi wanaamini sehemu nzuri ni kwa ajili ya wazungu na wageni wengine kutoka nje!! Mfano hayo majuice ya miwa, ukifungua ofisi nzuri ya kuuza juice ya miwa yenye mazingira safi na vifaa bora hakuna mtanzania atasogea hapo! labda kama ni diaspora au mzungu.
Hapana shida Bei nazo zinakua juu mnoo,chakula Cha 2500 atauza 6000,chips yai 2500,wanauza elf ,4
Hizo za kwenye vioo ndo shida ilipo hapo
 
Kwani wamekulazimisha ununue pweza wao?
Kwahiyo hawa wengine wanaotoa maoni juu ya bidha fulani, huwa wanalazimishwa kununua, ila siyo mbaya unajua hata umri unaongeza uweo wa fikra.
 
Nani kasema wanashida na pesa yako?

Ww unaye nunua ndiyo unashida na pweza zao ww kama unaona uchafu ni bora usinunue kuliko kuharibu biashara za watu.
Umri wa mtu pia huongeza uwezo wa kifikiri, basi sawa.
 
Nimekua mpenzi sana wa kula pweza, ila kula pweza Dar, kwa hawa wauzaji wetu barabarani, inataka uwe unafanana nao, usijue uchafu ni nini.

Unaona mtu amechagua mkia wa pweza, anaomba akatie vipande, jamaa anashika kwa mkono tu bila kunawa, akili ya kutumia uma, kushikia pweza anaekatwa hawana, mkono huo huo anashika pweza, anapokelea hela, anashikia stick anayojichokonolea kwenye meno.

Bakuli sasa ya kuwekea Supu, ni za plastick mpaka zimeingia rangi ya mchuzi wa pweza, jiulize maji wanayooshea baada ya mteja wa kwanza kuitumia, je vijiko vinanavyoingia ndani ya mdomo, wa kila mteja anekunywa supu, vinaoshwaje.

Ndugu zangu wauza pweza mjipende kwanza nyie ili muwapende wateja wenu pia, Pweza tunapenda ila.
Toka nimeumwa typhoid mwaka 2021 kutokana na kunywa michuzi na misupu ya pweza wa barabani sitamani kabisa kula pweza barabarani nitaenda feri kununua pweza fresh niende kupika nyumbani. mambo mengine tunajitakia kuyavaa magonjwa
 
Back
Top Bottom