Nimefuatilia kikao cha waziri mkuu leo na wafanyabishara kuhusu mgogoro wa kariakoo nimesikitika sana. Licha ya kwenda na Mawaziri na Timu ya wataalamu wa Wizara mbalimbali ameshindwa kutatua matatizo ya wafanyabiashara wa Kariakoo. Amepata fursa ya kuwasikiliza wafanyabiashara siku nzima ya...
Mapato ya milioni 4 kwa mwaka ni sawa na kama 11000 tu kwa siku, kumlipisha kodi mtu kama huyu ni kumfanya aendele kubaki kwenye kuganga njaa maisha yake yote biashara yake ikue mwendo wa kobe. Serikali waoneeni huruma wafanyabiashara wadogo katika masuala ya kodi kwa maslahi mapana ya ukuaji...
Kamati ya watu 14 ya kushugulikia changamoto za wafanyabiashara nchini imeanza kazi kwa kukutana na makundi tofauti ya wafanyabiashara. Kamati hiyo ilisema Dar es Salaam jana kuwa itafanya kazi kwa weledi, itasikiliza maoni yote na itazunguka katika masoko nchini. Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dk...
Wako wafanyabiashara kadhaa EFD zao zimezimwa na TRA na zinaonyesha ujumbe mzuri kabisa DEVICE BLOCKED BY TRA bila kusema sababu. Hii inawezekanaje wakati ambao TRA inahamasisha toa risiti dai risiti?!
Hivi karibuni kumeibuka Hoja nyingi juu ya uhalali wa Risiti za EFD, kwa sasa EFD ndio risiti maalumu ya Bidhaa kuuza na kununua popote pale Nchini. Lakini risiti hizi zina utata kutokana na uhalali wake. TRA wana tovuti ya kuhakiki risiti hizi za EFD ambayo ni TRA RISITI lakini asilimia 80% ya...
TRA Tanzania
Tanzania tuna mfumo wa kodi ambao naweza kuuita ni 'Tax chain system'. Yaani ni kwamba bidhaa moja inaweza ikapigwa kodi hata mara kumi halafu wale watu walioilipia kodi mara ya 2 hadi ya 10 wanatakiwa wapeleke mahesabu TRA ili warudishiwe kodi yao;kivipi?
Mfano bidhaa imezalishwa kiwandani, mnunuzi wa kwanza atakayenunua atalipa 18% Vat, na hii tu ndio halali ya TRA kwa bidhaa hiyo, lakini kama huyu mnunuzi wa kwanza ataenda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD na atamlipisha tena mteja 18% Vat ambayo TRA itamdai, huyu nae akienda kuiuza itabidi atoe risiti ya EFD ambapo atamchaji tena mteja 18% VAT ambayo nayo itatakiwa kupelekwa TRA, and so on hata mara 10.
Ili kuepuka kulipa VAT mara mbili kila mfanyabiashara atapeleka mahesabu na risiti za VAT (kwa waliounganishwa na VAT) ili kujua kiwango cha ziada cha kile ambacho ameshalipa, na hicho tu ndicho atapaswa kulipa; hii process inaleta mlolongo mgumu na very complicated, yaani ni mfumo mgumu sana bila sababu, nadhani wote mnofuatilia haya masuala mtajua.
Lengo la TRA kung'ang'ania huu mfumo ni ili kupata 18% ya faida ya kila hatua ya uuzaji wa bidhaa, hata ikiuzwa mara 10 TRA hawajali, wanataka 18% ya ile faida (gross profit) ya kila mfanyabiashara katika kila chain link ya uuzaji wa bidhaa husika, hadi kwa final consumer, yule wa mwisho kabisa. (Wanakaba hadi penalti).
Hii inaweza kuonekana ni nzuri ukiitazama kwa juu juu, lakini in reality hii ni sawa na kutumia risasi kuwinda smaki baharini, unatumia 10shs. kukusanya shs.8, yeees, ukweli ndio huu. Badala ya kusababisha such an expensive practical complexity ni kwanini TRA isiwekeze instead kuhakikisha kodi yote ya kila bidhaa inalipwa palepale kiwandani bidhaa inapozalishwa au bandarini mzigo unapoingizwa, hata kama kodi ikiongezwa sio mbaya lakini ilipwe yote infull palepale kiwandani / bandarini.
Hebu fikiria tu harassment wanayopata wateja wanaposafirisha mizigo barabarani, watu husimamishwa hovyo hovyo na mapolisi 'Tigo' wale wenye silaha za kivita as if wanasimamisha jambazi, kumbe umebeba T.V tu ndio imekuwa nongwa, kwani hii T.V si imepitia bandarini??! Si mchukue kodi yenu yote huko huko muache wananchi waishi kwa amani?
Mateso kama haya walikuwa wanayapata wamiliki wa magari ambapo kila mwaka walipanga foleni TRA na office za MXMALIPO kulipia road license, tena barabarani TRA walipoteza nguvu kazi kubwa ya wasomi wenye madegree kusimamabarabarani eti kukagua sticker za road license, as if hizo gari hazitumii mafuta ambayo tayari yana kodi lukuki, binafsi nilianzisha uzi wa kupendekeza kodi hiyo nayo iunganishwe tu humo humo kwenye mafuta(Hivi ni kwanini road license isilipiwe kwenye mafuta?) watu waligoma goma ili mwishowe logic and common sense emerged victourious, serikali ikahamishia kodi hiyo kwenye mafuta na sasa hii kero imeisha
Muda mwingine umasikini tunajitafutia wenyewe kwa kukariri vitu vilivyopitwa na wakati, technolojia imekuwa, ni rahisi sana kukata kodi yote in full kwenye viwanda / bandarini, tubadilike bwana; nakaribisha maoni.
=================================
Update: 04/04/2021
Waziri wa Fedha na Mipango, Mwigulu Nchemba, amesema wanaangalia namna ya kutumia mfumo mpya wa ukusanyaji kodi
Mama Samiah ana lipi la kutuambia juu ya kauli yake kwamba akipata nafasi ya kukopa atakopa tena. Tumsikilize mwamba akiwafundisha wanafunzi wake, na endapo Rais wetu anaweza kuirudia ile kauli yake juu ya mikopo? ================================ Update: 15/02/2022...
Kuna tetesi ya mgomo wa wafanyabiashara eneo la Kariakoo. Sababu za kuitisha mgomo; 1. Urasimu bandarini 2. Usajili wa stoo 3. Kamata kamata hovyo ya wateja kwa ukuguzi wa risiti Wao wapo tayari kufanya biashara kwa uhuru na kulipa kodi bila mambo ya rushwa rushwa na maonezi. Rai kwa...
Hadi Sasa ni saa 2:24 asubuhi maduka mengi hayajafunguliwa. ======== Pia, soma MGOMO: Wafanyabiashara Kariakoo kufunga biashara zao kuanzia 24/6/2024 mpaka changamoto zao zitakapotatuliwa RC Chalamila: Wafanyabiashara wa Kariakoo wajitafakari, migomo siyo suluhisho
Leo 25 june kuna mgomo mkubwa wa wafanyabiashara ,maduka yafungwa,oneway,mahengo mitaa haina watu kabisa hali tete wananchi wanahaha ,ccm imechoka kwa kweli
Licha ya kuripotiwa kuwepo kwa suluhu kwenye baadhi ya madai ya Wafanyabiashara waliyowasilisha Serikalini na kufanyika kikao cha pamoja lakini mpaka kufikia Saa tatu Asubuhi hali ya mgomo inaonekana kuendelea maeneo ya Kariakoo ambapo maduka mengi yameendelea kufungwa. Itakumbukwa kwamba jana...
Maduka yote Mjini Kyela leo 25/06/2024 yamefungwa, ikiwa ni muendelezo wa Mgomo wa wafanyabiasha nchi nzima kupinga dhuluma za serikali kupitia TRA, kuwakamua Wafanyabiashara hadi watoke damu. Wengi waliofuata mahitaji ya watoto wao hasa kipindi hiki kuelekea kufunguliwa kwa Shule, Wamepigwa...
Siongezi neno wala mimi si mkalimani === Alichozungumza kwenye video hiyo, ni kuhusu Africa kutoza kodi kubwa ambazo zinaua uwezekano wa maendeleo kwa kuwa zinaua hata uwekezaji. Suala hilo linaongeza umasikini na kufanya nchi kuwa tegemezi wa mikopo na misaada. Mzungumzaji huyo amesema hiyo...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.