demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
- Thread starter
-
- #21
Chico Ushindi anaelekea Al Hilal Sudan na Yacouba anatolewa mkopo kama haitabadilika itakuwa ni Geita Gold. Kwa Yacouba kutolewa kwa mkopo ni sawa ili Yanga ijiridhishe kama atakuwa amepona kabisa na vile vile apate mechi "fitness" kwa kucheza mara kwa mara akiwa timu ndogo. Kumbuka kuwa akibaki Yanga hatapata nafasi ya kucheza mara kwa mara kwa hiyo ni vigumu sana kurudisha kiwango chake kwa muda mfupi. Na Yanga kumtoa kwa mkopo ni faida kwao kwani wanaweza kumrudisha wakati wa dirisha dogo iwapo atakuwa ameimarika kifya na kiwango kimerudi na hasa iwapo kutakuwa na mchezaji wa kigeni aliyeshuka kiwango kuelekea dirisha dogo.
Yacouba awezi kosa nafasi mara kwa mara kwani Wakili Msomi na yeye wanafanana uwezo.