Napendeza Kamati ya Wataalamu kwenda kumuona Mo Dewji

Napendeza Kamati ya Wataalamu kwenda kumuona Mo Dewji

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Soka ni pesa, bila pesa soka inaweweseka. Mohamed Dewji amekuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya Simba Sc kiuchumi na hivyo kufanikisha pia usajili mzuri wa Wachezaji na benchi la ufundi.

Lakini amekuwa akiibua sintofahamu Kwa maneno yake ya chini chini kuhusu uwezezaji wake ndani ya Simba Sc na maneno yake yanawaka wapinzani wa Simba nafasi ya kuwakejeli. Yawezekana maneno yake yana ukweli lakini amekuwa aliyatoa Kwa mpangilio unaoonyesha timu haimsaidii kitu yeye ndo anaibeba.

Hata kama ndo ukweli, lakini hupaswi kumsimanga Mtu hadharani Kwa msaada unaompa. Alianza Kwa kusema hajawekeza 20B pekee Bali ni zaidi ya 85b hivyo wanaohoji 20b wajue ametoa msaada zaidi ya kiwango alichotakiwa. Akafuatia na kauli iliyowakera Sana wengi wa mashabiki wa Simba ya "Napata hasara kuwekeza Simba.

Jana kabutua tena Kwa kusema Kwa vile Mchakato unachelewa yeye ANAKATA TAMAA, Kwa maana nyingine yeye kama mwanasimba hana Muda wa kusukuma Mchakato huo usonge mbele Ila ameaachia wanaomhitaji wakamilishe Kila kitu halafu wamfuate, "Mkuu Tayari".

Kwa Hali hiyo napendekeza kuundwa Kwa Kamati ya Wataalamu toka JF kwenda kumuona TAJIRI na kumrai awe na subira wakati Mambo mengine yanashughulikiwa. Jambo jingine la kumweleza kama adidu za rejea Kwa Kamati ni kumtaka apunguze maneno ambayo mara nyingi anayatoa pale timu inapoonekana imeanza kutengeneza furaha.

WAJUMBE WA KAMATI
1.Scars - M/Kiti
2.
3.
4.
5.
 
[emoji38]
Screenshot_20230711-155735.jpg
 
Hapo wangehusika hawa wafuatao kwenda kumuona na kumbembeleza ili asikate tamaa:-

1. Hamis Kigwangala (MB)
2. Mzee Kilomoni
3..........
4.........
5..........

Wajumbe 5 tu wanatosha. Jazieni hao 3 wengine waliobakia.
 
Unatakiwa kujua kitu kimoja, timu inapoanza kuwa na furaha yeye pochi lake linaanza kuwa na huzuni maana ili nyinyi muwe na furaha ni lazima yeye aingiliwe pakubwa ndio maana anaongeaga ili kupunguza machungu ya pesa zake kifuani!

Yeye anaamini Transformation itafanya timu ijiendeshe yenyewe bila kuingilia kibubu chake.

Ukitaka ku experience anachofeel tajiri MO, wewe anzisha united kids FC ya mtaani kwako then invest pesa yako ili uwape furaha mashabiki wa hiyo timu as return wewe uweke matangazo ya shughuli zako za kibiashara!

Aliyevaa kiatu ndo anajua msumali unachomea wapi"- Maalim Seif
 
Hapo wangehusika hawa wafuatao kwenda kumuona na kumbembeleza ili asikate tamaa:-

1. Hamis Kigwangala (MB)
2. Mzee Kilomoni
3..........
4.........
5..........

Wajumbe 5 tu wanatosha. Jazieni hao 3 wengine waliobakia.
Kigwangala akamuone Mo?? We jamaa wewe!!!
 
Unatakiwa kujua kitu kimoja, timu inapoanza kuwa na furaha yeye pochi lake linaanza kuwa na huzuni maana ili nyinyi muwe na furaha ni lazima yeye aingiliwe pakubwa ndio maana anaongeaga ili kupunguza machungu ya pesa zake kifuani!

Yeye anaamini Transformation itafanya timu ijiendeshe yenyewe bila kuingilia kibubu chake.

Ukitaka ku experience anachofeel tajiri MO, wewe anzisha united kids FC ya mtaani kwako then invest pesa yako ili uwape furaha mashabiki wa hiyo timu as return wewe uweke matangazo ya shughuli zako za kibiashara!

Aliyevaa kiatu ndo anajua msumali unachomea wapi"- Maalim Seif
Ni kama kuna ukweli kwenye maneno yako!!! Ngoja nichimbe zaidi.
 
Unatakiwa kujua kitu kimoja, timu inapoanza kuwa na furaha yeye pochi lake linaanza kuwa na huzuni maana ili nyinyi muwe na furaha ni lazima yeye aingiliwe pakubwa ndio maana anaongeaga ili kupunguza machungu ya pesa zake kifuani!

Yeye anaamini Transformation itafanya timu ijiendeshe yenyewe bila kuingilia kibubu chake.

Ukitaka ku experience anachofeel tajiri MO, wewe anzisha united kids FC ya mtaani kwako then invest pesa yako ili uwape furaha mashabiki wa hiyo timu as return wewe uweke matangazo ya shughuli zako za kibiashara!

Aliyevaa kiatu ndo anajua msumali unachomea wapi"- Maalim Seif
Simba na yanga zina mvuto mkubwa, yeye alianza na african lyon zikamshinda ila si\kama aliona hasara kitu gani kilimshawishi awekeze kwenye timu kubwa nchini.
kama anaona hasara aache kama alivyoacha kwenye timu nyingine
 
Ujinga hiu kumpigia binadamu magoti siyo haijawai kuwa ya kwanza kuporomoka kiuchumi
 
Back
Top Bottom