Napendezwa sana na utulivu alionao Freeman Mbowe

Gulio Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Jan 30, 2018
Posts
3,325
Reaction score
7,807
Nampongeza sana kiongozi wa CHADEMA Freeman Mbowe kuonesha ukomavu wa kisiasa kuhimili misukosuko kila inapojitokeza amekuwa na utulivu sana mwenye hekima hasa kunapotokea chama kinapitia hali ngumu.

Wapo viongozi walihama lakini chama kilizidi kuimarika zaidi hata sasa nimejifunza zaidi yaliyotokea kwa mch msigwa yeye alikaribishwa chadema akapewa platform akajulikana sasa msigwa amehama chama amesahau yote mazuri aliyofanyiwa anazunguka katika majukwaa ya ccm kumchafua mwamba Mbowe amebaki kuwa kimya sio kwamba hajui madhaifu ya mch Msigwa kukaa kimya ni jibu tosha anamambo mengine ya msingi zaidi.

Mwamba unastahili kabisa kuendelea kuwepo katika kiti cha uongozi.
 
Mr Zero ataongea nini?
 
Mbowe kijana wa saigon, sifa Ile ndio sifa ya vijana wa saigon, utulivu na kuendesha game from behind the scene.

mfano wa kijana mwingine wa saigon ni Jk wa msoga, hao wote ni vijana wa saigon ambao wanarun hii game hapa bongo.

Utulivu, tolerance, uvumilivu, umafia nk ni sifa ya vijana waliokomaa wa saigon.
 
Mbowe anafaa sana kuiongoza nchi hii tuondokane na utumwa wa CCM.
 
Mkuu The Boss aliwahi kuwaeleza Yeye na JK kama ni Vijana wa Mjini, yaani born town miaka ile JPM akiwabana kinamna
 
Kabisa, Mbowe ana utulivu wa hali ya juu. Angekuwa na wenge, angeuvaa mkenge wa Mchungaji Msigwa. Badala yake Lissu ndiye akauvaa mkenge, akaanza ziara na Msigwa, akaenda mpaka Iringa akamshambulia Mbowe, muda kidogo Msigwa kijani.

Hapo Lissu ndio alijua kwamba Mbowe ni master wa siasa za mageuzi aliyedumu katika mfumo kwa kipindi kirefu zaidi, ukiondoa Maalim Seif Sharrif Hamad
 
Mbowe ni kijana!
JK ni kijana!

Nyie ndio mnafanya vijana halisi wa nchi wasithaminiwe
 
Utulivu au hana namna?
 
Ukipigwa kwenye mshono lazima utulie Kwanza
 
Elewa neno "kijana wa Saigon"

Hata akiwa Mzee wa miaka 1000 bado atakuwa tu kijana wa Saigon.
Kwa nini usiseme mtu wa Saigon, kutumia neno kijana kwa muktadha huo ni kama kuwadogosha vijana waliopo sasa. Wazee hamtaki kuzeeka manina
 
WEWE ENDELEA KUPONGEZA MWENZAKO ANAVUTA ZAKE HELA MAISHA YANAENDELEA,WAJINGA KAMA NYINYI KWAKE NI MTAJI MKUBWA SANA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…