Napinga hoja ya RC Makalla ya kulazimisha Mabasi yote ya Mikoani kupakia na kushusha abiria Stendi ya Magufuli pekee

Napinga hoja ya RC Makalla ya kulazimisha Mabasi yote ya Mikoani kupakia na kushusha abiria Stendi ya Magufuli pekee

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Amos Makalla ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na Mfadhili wa zamani wa bendi ya FM ACADEMIA ya Kinondoni, bila kufanya utafiti wowote ule leo ametoa amri ya kulazimisha mabasi yote ya mikoani kuanzia safari zao kwenye kituo kikuu cha mabasi ya mikoani cha Mbezi Luis, kinachoitwa kituo cha mabasi cha Magufuli na kushushia abiria wake hapohapo.

Lengo kuu la kauli yake hii ni kujaribu kukusanya watu ili kuneemesha wafanyabiashara waliojazana kwenye stendi hiyo bila mpangilio wowote, Makalla anaamini kwamba abiria wote wakishushwa ama kuanzia safari zao hapo basi watanunua bidhaa za wamachinga waliojazana hapo, hivi ndivyo akili yake ilivyomtuma, kwamba abiria wakomeshwe ili kufurahisha wafanyabiashara, amesahau kwamba abiria ni bora kuliko wamachinga kwenye mustakabhali wa Safari, hata hivyo sikubaliani naye.

Mbezi Luis eneo ilikojengwa Stendi ya Mabasi ya Mikoani ni nje kabisa ya jiji la DSM , kulazimisha Mabasi yaliyokuwa yanaanzia safari zake Mbagala, Tandika au Kigamboni kuacha kazi hiyo na kulazimisha sasa lazima yote yaanzie Nje ya jiji ni sawa na unyama , kwamba sasa aliyekuwa anapandia basi Mbagala akodi teksi kwa zaidi ya gharama ya tsh elfu 30 ili kulifuata basi Mbezi Luis, kwa vile tu Amos Makalla kajisikia hivyo haikubaliki na ni lazima ipingwe kwa nguvu zote.

Alichotakiwa kufanya Mh RC ni kuhakikisha kwamba basi lolote kutoka kwenye yard yoyote ile binafsi linakoanzia safari lisiondoke DSM bila ya kupita Stendi kuu ama lishushe litakako ila ni lazima lije stendi kuu, Vinginevyo Mh Makalla atamke hadharami Maslahi yake binafsi atakayopata kwa kuwatesa abiria wa Kigamboni, Vikindu , Chamanzi, Mbagala, Tandika na kwingineko waliokuwa wanapata ahueni ya kuanzia safari kwenye maeneo yao ya karibu.

Naomba kuwasilisha.
 
Siku zote huwezi kujenga Bar bila kuwashirikisha walevi hiyo stend wadau wa secta ya usafiri hawakushirikishwa ipasavyo

NB: Baada ya miaka 10 ijayo hiyo stand itafanya kazi vizuri kama wataboresha usafiri wa kufika sehwm husika
 
Lazima niseme, hii ni ngumu mkuu Erythro.

Pamoja na pendekezo lako la mabasi hayo lazima yapitie Stendi kuu, bado naona Makalla yumo ndani ya mstari, hata kama yeye atakuwa na msukumo wa maslahi tofauti na matakwa ya mabasi hayo kuanzia na kuishia stendi kuu.

Stendi kuwa mbali na mjini siyo hoja, kwa sababu stendi kuu ni lazima ihudumiwe na usafiri toka sehemu zote za mji, kwa hiyo hiyo ni fursa kwa wenye biashara zao za usafirishaji mjini.

Ni sawa na uwanja wa ndege, ambako ukitaka kusafiri, kama unatokea Kawe, ni lazima utafute usafiri wa kukufikisha JKNIA, na hivyo hivyo, kama unaingia, utapata usafiri toka hapo kukupeleka Kawe.

Mimi naona la msingi zaidi ni Makala kuhakikisha sehemu zote za mji wake zipo huduma za kuwafikisha wananchi Stendi kuu ya mabasi, Mbezi Luis.

Lakini pia inabidi niulize swali hapa: kuna ubaya wowote kwa mfano kuwepo kwa vituo kadhaa vya mabasi mjini Dar, kwa mfano kituo cha mabasi yanayoelekea kusini mwa nchi kikawepo Mbagala; kituo cha mabasi yaendayo Nyanda za juu yakaanzia, tuseme Gongo La Mboto, n'k.?

Vipi, mbona hujachangamkia fursa ya Hotel/Guest maeneo hayo mkuu Erythrocyte!
 
Lazima niseme, hii ni ngumu mkuu Erythro.

Pamoja na pendekezo lako la mabasi hayo lazima yapitie Stendi kuu, bado naona Makalla yumo ndani ya mstari, hata kama yeye atakuwa na msukumo wa maslahi tofauti na matakwa ya mabasi hayo kuanzia na kuishia stendi kuu.
Sisi tulioanzia safari zetu Tandika tumesababisha hasara gani? Kuhusu kuwekeza pale kwangu ingekuwa aibu sana, mpangisha vyumba alikuwa Sipora Liana.
 
sisi tulioanzia safari zetu Tandika tumesababisha hasara gani
Sina hakika kama Bima za hayo magari zitakuwa zinahusiana na mpango huo; hilo ni jibu moja la harakaharaka. Nina hakika zipo sababu nyingine nyingi, tena za kisheria zinazowabana wasafirishaji hao, na hata kwa usalama wa wasafiri wao.
kuhusu kuwekeza pale kwangu ingekuwa aibu sana
Hata hotel yenye hadhi ingekuwa ni "aibu"?

Hiyo ya 'Sipora' naona imenikalia pembeni kabisa, maanake sielewi kitu!

Lakini niseme tu ninayoyajua kwa uzoefu: Miji mikubwa yote duniani, kuna vituo kama hicho cha Magufuli, na utaratibu huo ni wakawaida kabisa. Sasa kama kwa Tanzania utakuwa haufai, hilo litakuwa ni jambo jingine.
 
Juzi nime-experience something very strange.

Hajui ni kwa jinsi gani hayo mabasi yanawasaidia abiria hasa wale wanaotoka safari za mbali, na wanaishi mbali na mji.

Chukulia kwa mfano, juzi nimetoka Kahama kuja DSM, njiani tulipofika Dodoma tumekutana na msafara wa makamu wa Rais tukawekwa pembeni saa zima, baada ya hapo safari ikaendelea.

Tulipofika karibia na Morogoro, tairi ya gari (bus) ikapasuka, pale napo tukasubiri tairi libadilishwe tukasubiri karibia dakika 45 mpaka giza likaingia, baada ya hapo tumetoka pale tukaja kufika Dsm saa 6 usiku, kule ndani palikuwepo na abiria wanaoenda Mbagala, wakamuomba dereva wa lile bus waende nalo Mbagala, dereva akakubali.

Hawa watu wameshachoshwa na uchovu wa safari, wana mizigo, watoto, na wengine ni wazee, hivi Makalla anayajua haya mambo? anataka mtu alietoka safarini amechoshwa na safari bado akifika Dar aanze kugombania daladala tena akiwa na uchovu wa safari?

Kuwalazimisha hawa abiria kupanda daladala maana yake watatakiwa kulipa tena nauli zao na watoto, na kulipia mizigo kama watakuwa nayo, hapo bado kupata siti nayo ni bahati, Makalla anataka hawa abiria wapitie mateso yote haya ili tu kuhamasisha biashara ya mamalishe stand ya Magufuli!.

Hata hivyo, sababu aliyoitoa Makalla kuwa abiria wale kwa mamalishe stand ya Magufuli nayo ni option, wapo watakaokula na wasiokula, kwanza usiku huo wanapofika wengi wanaelekea majumbani kwao kula na kupumzika, kwangu hii sio sababu ya kujitosheleza kulazimisha wenye mabasi washushe abiria wote stand ya Magufuli.
 
Naunga mkono hoja. Baadhi ta wenye mabasi wenye stendi zao pale Sinza Shekilango kama Kilimanjaro, Dar Lux, Marangu Coach na mengine, wenye mabasi zaidi ya moja kwa route ya Moshi Arusha, njia rahisi kwao ni route ya Bagamoyo Msata, na sio njia ya Chalinze, kuwalazimisha lazima waanzie Stendi mpya ni kuwatesa tuu bure abiria, after all, wengi wa abiria wa mabasi hayo, haswa wale abiria wa 1st Class, sio wa type ya kununua vitu kwa machinga au kula kwa Mama Ntilie! Hivyo kama nia ni kuwasaidia Machinga na mama ntilie, then, hizo ni sababu alizotoa Mkuu wa Mkoa ni sababu za kijinga sana!.

Hatuwezi kuendelea kuendesha nchi kijinga jinga hivi halafu utegemee tutapata mafanikio. Il tuendelee , la kupata maendeleo ya kweli de must stop such nonsense!.

p
 
Ni sawa na uwanja wa ndege, ambako ukitaka kusafiri, kama unatokea Kawe, ni lazima utafute usafiri wa kukufikisha JKNIA, na hivyo hivyo, kama unaingia, utapata usafiri toka hapo kukupeleka Kawe.
Usilinganishe air transport logistics na mabasi ya walalahoi/masikini. Anayepanda ndege ana uwezo wa kulipa taxi mpaka airport. mtu anakwenda Mtwara. Yuko Mbagala, apande gari aje Mbezi kupanda gari la Mtwara kweli? Fikiri tena na tena! Basi lianzie Mbezi, wa Mbagala limkute Mbagala limpakie safari iendelee.
 
Sio magufuli stand tu ni mikoa yote.

Ukibisha tafta usafiri wako huko uendako.
 
Alichotakiwa kufanya Mh RC ni kuhakikisha kwamba basi lolote kutoka kwenye yard yoyote ile binafsi linakoanzia safari lisiondoke DSM bila ya kupita Stendi kuu ama lishushe litakako ila ni lazima lije stendi kuu , Vinginevyo Mh Makalla atamke hadharami Maslahi yake binafsi atakayopata kwa kuwatesa abiria wa Kigamboni , Vikindu , Chamanzi , Mbagala , Tandika na kwingineko waliokuwa wanapata ahueni ya kuanzia safari kwenye maeneo yao ya karibu .
Naafikiana nawe 100% ila napingana nawe 100% kumwita mtu mwenye akili za Makala mheshimiwa, Makala hastahili kuheshimiwa kwa lolote, kwa mtazamo huo ipo siku hata vibaka watapewa heshima, kitendo alichofanya Makala ni economic rapping, na hii huenda ina agenda ya siri nyuma yake kwa manufaa yake binafsi. He is stupid!!
 
Mama tunampenda sana, lakini kuna watendaji wake baadhi wanatulazimisha tumchukie Madame. Hili alitengue!
 
Lakini kweli najaribu kufikiria kwa mfano mtu kapitia njia ya bagamoyo stendi ya mwenye gari kama kilimanjaro pale shekilango anapitia mwenge alafu abiria wake wengi wanakuja hadi shekikango alafu eti arudi nao hadi mbezi wakashukie huko alafu gari sasa litoke mbezi lije shekilango tena wakati huo huo kuna abiria wanahitaji kuja kushukua tena shekilango wao sasa inabidi wapande tena daladala. Hapana hapo kakosea sana kwa kweli huu ni usumbufu mkubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anataka kusababisha usumbufu usio na tija.
  • Wale wa kusini stand zao zipo Mbagala na Tandika siyo sawa waje mpaka mbezi mwisho.
  • Wale wa Mwanza, kilimanjaro wapo stand zao zipo Shekilango siyo sawa waje mpaka Mbezi mwisho.
 
Ah hapo MAkala kachemsha
Aisee usiombe ukasafiri uende mle ndan yaan ni kero mara 10 ya ilivyo kuwa pale Ubungo buss terminal ..madeiwaka wana kung'ang'ania utazan nzi kaona kinyesi yaan utajuta kwann una safiri
 
Naafikiana nawe 100% ila napingana nawe 100% kumwita mtu mwenye akili za Makala mheshimiwa, Makala hastahili kuheshimiwa kwa lolote, kwa mtazamo huo ipo siku hata vibaka watapewa heshima, kitendo alichofanya Makala ni economic rapping, na hii huenda ina agenda ya siri nyuma yake kwa manufaa yake binafsi. He is stupid!!
Hivi haoni Kama atasababisha msongamano wa magari na watu bila sababu ya msingi? Huyu jamaa sijui katumia akili gani
 
Dar es Salaam haihitaji kuwa na stendi kuu ya mabasi.Ukosefu wa uelewa wa biashara ya usafiri na akili ndogo za wapanga mji zinazopenda centralization na kuona majengo makubwa makubwa ndizo zimetufikisha katika matatizo kama haya.
Lazima niseme, hii ni ngumu mkuu Erythro.

Pamoja na pendekezo lako la mabasi hayo lazima yapitie Stendi kuu, bado naona Makalla yumo ndani ya mstari, hata kama yeye atakuwa na msukumo wa maslahi tofauti na matakwa ya mabasi hayo kuanzia na kuishia stendi kuu.

Stendi kuwa mbali na mjini siyo hoja, kwa sababu stendi kuu ni lazima ihudumiwe na usafiri toka sehemu zote za mji, kwa hiyo hiyo ni fursa kwa wenye biashara zao za usafirishaji mjini.

Ni sawa na uwanja wa ndege, ambako ukitaka kusafiri, kama unatokea Kawe, ni lazima utafute usafiri wa kukufikisha JKNIA, na hivyo hivyo, kama unaingia, utapata usafiri toka hapo kukupeleka Kawe.

Mimi naona la msingi zaidi ni Makala kuhakikisha sehemu zote za mji wake zipo huduma za kuwafikisha wananchi Stendi kuu ya mabasi, Mbezi Luis.

Lakini pia inabidi niulize swali hapa: kuna ubaya wowote kwa mfano kuwepo kwa vituo kadhaa vya mabasi mjini Dar, kwa mfano kituo cha mabasi yanayoelekea kusini mwa nchi kikawepo Mbagala; kituo cha mabasi yaendayo Nyanda za juu yakaanzia, tuseme Gongo La Mboto, n'k.?

Vipi, mbona hujachangamkia fursa ya Hotel/Guest maeneo hayo mkuu Erythrocyte!
 
Katika makosa makubwa Mama amefanya ni kumleta Makala Dar, alishindwa Mbeya akahamishiwa mkoa mdogo huko Rukwa/Katavi akashindwa, ataiwezaje Dar?

Badala ya kuja kutatua kero amekuja kuongeza kero, he is not for citizens
 
Back
Top Bottom