Napinga kauli za kusema "Mwisho wa mwaka ajali na vifo ni vingi

Napinga kauli za kusema "Mwisho wa mwaka ajali na vifo ni vingi

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Mtu anatoa kauli hii bila kutoa takwimu za vifo au ajali za miezi mingine huku akilinganisha na Desemba.

Kwakuwa watu wengi wako likizo basi habari husambaa haraka na kwa wingi. Tukio moja likitokea hupambwa kwenye media zote.

Pia ili upige hesabu sawia ya takwimu ya ajali barabarani usisahau kupiga hesabu ya magari yanayofanya movement katika hiyo barabara.

Kama mwezi April barabara ya Dar - Arusha kwa siku hupita magari 1000, ajali 4-7 . December kama yanapita magari 2500 kwa siku ajali zikiwa 7- 13 hapo ukimwona mtu anakesha kanisani kufunga roho ya ajali basi akili yake si timamu.

Hii ni sawa na kusema shule hii siku hizi inafaulisha sana. Ukiangalia waliofaulu kwenda kidato cha 5 ni 40, huku waliohitimu kidato cha 4 ni 200.

Zamani walikuwa wakifaulu 15-20, huku waliohitimu kidato cha 4 ni 60.

Pia lazima tufahamu kuwa watu wengi ambao hawajazoea masafa marefu ndipo hujifunza kushika usukani kwa muda mwingi kwenda kwao kuringishia harrier zao.

Hamna cha roho za ajali mwezi Desemba. Kama zipo rohi za ajali basi hazihusiani na mwisho wa mwaka.

Hakuna cha sijui roho ya ajali, mara roho ya umwagaji damu kwaajili ya kafara . No.

Kama wapo watu hutoa kafara basi hawawezi kusubiria Desemba. Watafanya muda wowote kwa kadri ya uhitaji wao.
 
Hayo matukio uliyoyataja ya kuongezeka kwa safari ndizo haswa roho za ajali zenyewe. Shetani hupenda ku-take advantage ya matukio kama haya.
 
Binafsi naona kuna vitu vingi vinachangia hili kabla ya watu kuanza kukimbilia kafara, Mtoa mada Nakubaliana na wewe kabisaaa

1. Madereva hua wanachoka sana maana Safari nyingi Inakua Go and return
2. Speed ya Gari inakua kubwa hasa gari za abira ili kwendana na mda na kasi ya abiria.
3. Ongezeko kubwa la Gari barabarani, hii sasa ni kama mtoa mada alivyo elezea vzr
4. Gari nyingi kua bussy sana, hii inafanya hata mda wa kutosha kwa ajili ya service usiwepo, au hata check-up haipo, hivyo gari inasafiri ikiwa na defects,
5. Kujaza/pakia kupita kiwango/uwezo wa gari(hili sitazungumzia, kila mtu anajua kila kitu kina limiting point),
6. Umakini wa Traffic na mfumo mzima wa ukaguzi unakua chini sababu ya work load kubwa,

Maombi yenu, nina afari ndefu kuanzia Asubuhi hii saa 12
 
Binafsi naona kuna vitu vingi vinachangia hili kabla ya watu kuanza kukimbilia kafara, Mtoa mada Nakubaliana na wewe kabisaaa

1.Madereva hua wanachoka sana maana Safari nyingi Inakua Go and return,
2. Speed ya Gari inakua kubwa hasa gari za abira ili kwendana na mda na kasi ya abiria.
3. Ongezeko kubwa la Gari barabarani, hii sasa ni kama mtoa mada alivyo elezea vzr,
4. Gari nyingi kua bussy sana, hii inafanya hata mda wa kutosha kwa ajili ya service usiwepo, au hata check-up haipo, hivyo gari inasafiri ikiwa na defects,
5. Kujaza/pakia kupita kiwango/uwezo wa gari(hili sitazungumzia, kila mtu anajua kila kitu kina limiting point,
6. Umakini wa Traffic na mfumo mzima wa ukaguzi unakua chini sababu ya work load kubwa,
Yes.
Kukimbilia kusema kafara ni ulofa kabisa
 
Back
Top Bottom