Uchaguzi 2020 Napinga viongozi wa dini kukutana kwa lengo la kuelezea kinachoitwa mafanikio ya Rais Magufuli, hii ni kampeni na haikubaliki

Haya mafanikio ya Rais hayaonekani kwa macho mpaka yanadiwe?
Jukumu la viongozi wa dini kukosoa tu na sio kusifia???

Kwanini mnapenda kusikia tu yale yanayoifurahisha nasfi zenu !!!!?

Hiyo ni demokrasia ni ipi ambayo mnaipigania ikiwa mnashindwa kustahimili mawazo na fikra hasi za wenzenu!!??

Au demokrasia ni kukosoa tu!!?
 
umesikia wapi Bagoza kaitisha kikao cha kumpongeza Mbowe
 
Lini wamewahi kosoa,labda tu Kama wangekuwa si wanufaika.
Shehe baada ya kuona mirija imekatika kamtosa na kumnanga swahiba wake.
 
Wakikosoa wataambiwa wasichanganye siasa na dini,huku msajili keshaagizwa kuzifuta taasisi
 
Pingapinga Fc at work.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Ni shetani tu ndie asiyependa ukweli usemwe! Viongozi wa dini wameamua kumkataa shetani kwa kuamua kipongeza awamu ya tano waziwazi ili kuondoa upotoshaji wa shetani ambaye anamakengeza au ni kipofu anapotazama ukweli!
 
Viongozi wa dini ndio chanzo cha kuendelea kwa udikteta Afrika kwa kuacha wajibu wao mafundisho yapo wazi haki na batili udhalimu havichangamani,hata mitume awakushirikiana na tawala dhalimu ili kupata shibe,Bali walizipinga waziwazi hata kupelekea vifo vyao walisimama na Jamii kupinga dhuluma.Watu waovu majahili yafaa watengwe na Jamii,watengwe au wafutwe na dini zao bila kujali ukuu wao hii itawafanya waache watambue uovu wao na kurudi kwenye mstahili, udikteta ni zao la ukosefu wa malezi bora utotoni na utapiamlo wa kimalezi yenye maadili ya kutambua utu.
Viongozi wa dini wa kizazi hiki wanamkosea Mungu kwa kuwaalika na kuwapandisha Hadi madhabauni watu waovu,wanukao damu za watu,ole wenu mtakinywea kikombe cha damu za watu zilizomwagwa,cheki mfano Burundi Nkurunziza anapanda Hadi madhabauni anaimba kwaya,anapewa nafasi anahubiri akitoka kanisani anaenda mwaga damu za watu hapa viongozi wa dini wanakosa vipi kuwa kuni maana wameshiriki dhuluma kwwa unafiki wa kushindwa kusimamia kweli.
Ukimtenga mtu muovu ataujua uovu wake maana wengine ni barbaric, uncivilized bila action hawawezi badilika.
 
Hakuna nguvu hapo inatumika, maana wasiposema wao hata barabara, na nawe yatasema! Lengo ni kuondoa upotoshaji unaofanywa kwa makusudi na baadhi ya watz wasio Italian mema Tz yetu! Hongereni saana viongozi wa kiislam kwa kuliona Hilo!
 
Povu lote Hili la Nini! Kila mtu sio mlisema apewe haki ya Uhuru wa kujieleza! Sasa Uhuru si ndio huu, au mie sijui maana yake!? Ninyi mnaojiita wapinzani ni wanafiki kuliko maelezo, na Kama mngepewa mamlaka naona hakuna ambaye angeruhusiwa kufanya myafanyayo! Aibu yenu!
 

Wako hatua ya Nne ya sheria ya kumshughulikia Chama pinzani na Shindani katika sheria 11 za kumaliza upinzani. Sheria hizi hufanya kazi mara baada ya kushinda uchaguzi. Hufanya kwa kidodo kidodo ili mahasimu wasichanganyikwe. (sababu mkifanya haraka na wakachanganyikiwa wanaweza kusababisha kupotea kwa amani na utulivu katika nchi )


1) Adui yako wa kisiasa unatakiwa umpige sana achakaye kiasi ambacho hata atakapo pata nafasi ya kujibu mapigo, mapigo yake yawe dhaifu sana kiasi yasiwe na madhara kwako.

2) Wakati wa mashambulizi ya kisiasa, hakikisha Magenerali ( wakuu wa vyombo vingine vya utendaji wako imara na wakiendeleza mashambulizi na kutoa kipigo maeneo yote ambayo hasimu wako wa kisiasa anaweza kupata usaidizi, au kukimbia au kuepuka mapigo kabla hajapigwa sana na kuchakazwa.

3) Hakikisha unavunja nguvu za hasimu kwa kiasi kikubwa sana kupitia kunyong'onyesha Viongozi wake ambao wana nafasi ya kungundua mapambano , na wanachama watenganishwe na viongozi wanao weza kugundua mapambano kijikusanya tena. Ondoa akili bakiza makapi ili waendelee kupoteana.

4) Tumia vyombo vyote vya imani ( faith based) kwa kupitia kivuli na sio moja kwa moja ilI wakapigike kwenye nyoyo zao ili wawe waumini na pia watiifu kwa mamlaka.


5)

6)

7)

8)

9)

10)

11)

NITAWAPA SHERIA ZILIZO BAKI AU NYUNDO KIDOGO KIDOGO KUHUSU ( THE ART OF POLITICAL WAR AGAINST THE VANGUISHED).
 
Hakuna mahali popote katika dunia hii ambapo Shetani aliwahi kumshinda Mungu
 
Umemaliza
 

Utateseka saana, anza kuwatukana ili upunguze hasira,
Unajua munga na bagonza na askofu mkuu wa kkt hawataenda najua hao utawasifia kwamba wanajitambua, ila wakiwachoma kasindano kadogo kuwa Chadema mjitafakari mnaanza kuwashushia mawe.
 
Utateseka saana, anza kuwatukana ili upunguze hasira,
Unajua munga na bagonza na askofu mkuu wa kkt hawataenda najua hao utawasifia kwamba wanajitambua, ila wakiwachoma kasindano kadogo kuwa Chadema mjitafakari mnaanza kuwashushia mawe.
uko nje ya mada
 
Ndugu zangu mimi sioni shida viongozi wa dini wakieleza mazuri yaliyofanyika. Ikifika kipindi cha uchaguzi tunafanya maombi ili kupata kiongozi mzuri. Je, ni dhambi kuyashuhudia matendo makuu ya Mungu kwa kuonesha jinsi maombi yetu yalivyojibiwa?

Aaagh jamani hebu tuacheni chuki binafsi. Nadhani mngesubiri waongee halafu mseme wapi wamedanganya

Viva viongozi wetu wa dini viva
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…