Narudi tena kwenye Kilimo cha Nyanya. Mniombee

Narudi tena kwenye Kilimo cha Nyanya. Mniombee

Akili 09 Nguvu 01

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2015
Posts
695
Reaction score
1,377
Mnamo mwezi wa 12/2018 na Januari 2019 niliingia kwenye kilimo cha Nyanya. Nikiri kua nilikua sina maarifa wala uzoefu wowote kweny kilimo cha nyanya. Kuna rafiki yangu mmoja ndo alinishauri na kunishawishi kuingia kwenye kilimo cha nyanya(alinichukua na kunitembeza kweny mashamba ya nyanya na niliona jinsi watu walivyofanikiwa kupitia kilimo cha nyanya) hivyo nilishawishika vilivyo

Tulikubaliana tulime shamba la pamoja kwa kushirikiana na kushare gharama sawa kwa sawa. Tulikodi shamba na tukalima kwa trekta, baada ya wiki moja tu tangu kulima uyu rafiki yangu akapata kazi nyingne mkoa mwingine. Hivyo nikabaki peke yangu nikilisimamia shamba.

Nilienda vijijini nikatafuta vijana wa kazi nikawapeleka shamba shughuli iliendelea. Hapa nikiri kua gharama zote za shamba nilitoa mim uyu rafiki yangu ni kama alinisusia shamba(kumbuka tulilima shamba kubwa kama hekari 1.25 ivi kwa minajili ya kushare gharama)

Kufupisha stori
Katika kilimo hiki nyanya zilipofikia hatua ya kukomaa ziliingiliwa na ugonjwa wa wadudu na mnyauko hivyo mwisho wa siku sikuvuna hata ndoo moja ya nyanya. Pia vijana waliokua wanahudumia shamba wamenifelisha kwa kiasi kikubwa
Nilivopiga hesabu nilikua nimetumia zaidi ya Milioni 2 lakini sikuvuna kitu

Sijakata tamaa
Mwaka huu 2020 nimerudi tena kweny kilimo cha nyanya, saizi nna maarifa na uzoefu kidgo pia nmemtafuta mwenyej mzoefu nashirikiana nae, mim natoa gajarama yeye katoa shamba na nguvukazi yake. Kama mambo yakienda vizuri nategemea mwezi wa 4 nyanya zitakua tayari
Tukutane mwezi wa 4 kwa ajili ya mrejesho wa mavuno
 
Nzuri hiyo, wekeza sana kwenye utaalam kabla hujaanza kulima, uliza bwanakilimo best popote alipo aje akuongoze na kukupa muongozo kuanzia kuandaa shamba, kupanda mpaka kuvuna. Epuka mabwanakilimo wa bei rahisi, anza kutafuta soko mapema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kilimo Cha nyanya masika Bila greenhouse Ni janga,nimelima hela tano morogoro bei 50000 nilichuma tenga 27 tu presha juu,mbegu Kama laki 7,bado madawa karibu 1.2 m
QUOTE]
[/

Duuh pole sana Mkulima mwenzangu, tatizo bei za greenhouse ni kubwa sana ndo mana tunaona bora tulime ivoivo. Nyanya za masika zina changamoto sana afu uku kwetu naona mvua zimechanganya sana mwaka huu. Tuendelee kukomaa ipo siku
 
Nilipata milioni nane ya kwanza katika maisha yangu kwa kulima eka moja ya nyanya mwaka 1998. Kama unakumbuka wakati wa el nino. Nina uzoefu sana kwenye hilo basi muda umekua sina baada ya kujiunga kwenye BABYLON system. Kwa anaetaka kushare nitamjuza lini kulima na lini kuacha kadiri ya bei.
 
Kilimo Cha nyanya masika Bila greenhouse Ni janga,nimelima hela tano morogoro bei 50000 nilichuma tenga 27 tu presha juu,mbegu Kama laki 7,bado madawa karibu 1.2 m
Ni hatari sana lakini huwa tunapunguza madhara kwa kuchagua eneo lenye mvua hafifu na udongo usiotuamisha maji.

Miongoni mwa magonjwa yenye kuleta uharibifu mkubwa ni early bright, si rahisi kuondoa kabisa shambani hasa kwa viuatilifu vyetu hivi ila athari zake zinaweza kupunguzwa kwa kwa spray program ya hata kila baada ya siku tatu ikiwa hali ya hewa ina-favour kuzaliana kwa kuvu(joto na unyevu).

Wadudu waharibifu hasa hasa ni tuta absoluta ambae anadhibika vizuri kwa indoxacarb, emamectin benzoate, acetamiprid n.k, cha muhimu ni kuhakikisha mmea umetunzwa vizuri na unamajani ya kutosha. Hii ni kwa kuwa ni rahisi kumdhibiti akiwa kwenye majani kuliko akianza kutoboa matunda.
 
Hakuna kukata tamaa, ila usiache kuzingatia baadhi ya ushauri wa wadau hapo juu.
 
Ongeza bidii na maarifa.. mafanikio hayataepukika
 
Mwambie atafute masoko ya uhakika kwanza kabla ya yote.
Nzuri hiyo, wekeza sana kwenye utaalam kabla hujaanza kulima, uliza bwanakilimo best popote alipo aje akuongoze na kukupa muongozo kuanzia kuandaa shamba, kupanda mpaka kuvuna. Epuka mabwanakilimo wa bei rahisi, anza kutafuta soko mapema

Sent using Jamii Forums mobile app

dodge
 
nmemtafuta mwenyej mzoefu nashirikiana nae, mim natoa gajarama yeye katoa shamba na nguvukazi yake.
Kama hautakuwepo shambani wewe mwenyewe ukishirikiana na jamaa kufanya au kusimamia kazi zote kila siku, ikiwemo kukagua magonjwa, ratiba za dawa na mbolea nakuomba uachane na hii biashara haraka sana.

Acha kabisa.
Huyo mwenyeji ndio anakuja kukuangusha vibaya sana haijalishi anaonekana mwema, mwaminifu kiasi gani au ana uchungu wa maendeleo kiasi gani.
Ukibisha tunza post yangu kisha uje unitafute mwezi April au May 2020.
 
Kama hautakuwepo shambani wewe mwenyewe ukishirikiana na jamaa kufanya au kusimamia kazi zote kila siku, ikiwemo kukagua magonjwa, ratiba za dawa na mbolea nakuomba uachane na hii biashara haraka sana.

Acha kabisa.
Huyo mwenyeji ndio anakuja kukuangusha vibaya sana haijalishi anaonekana mwema, mwaminifu kiasi gani au ana uchungu wa maendeleo kiasi gani.
Ukibisha tunza post yangu kisha uje unitafute mwezi April au May 2020.
Sawa mkuu nmekuelewa. Shamba likishachanganya nitakua sikauki shambani, sahizi shughuli bado hazijakomaa kwahiyo naenda mara moja moja lakin niseme tu kua nipo karibu sana na shamba
 
Ni hatari sana lakini huwa tunapunguza madhara kwa kuchagua eneo lenye mvua hafifu na udongo usiotuamisha maji.

Miongoni mwa magonjwa yenye kuleta uharibifu mkubwa ni early bright, si rahisi kuondoa kabisa shambani hasa kwa viuatilifu vyetu hivi ila athari zake zinaweza kupunguzwa kwa kwa spray program ya hata kila baada ya siku tatu ikiwa hali ya hewa ina-favour kuzaliana kwa kuvu(joto na unyevu).

Wadudu waharibifu hasa hasa ni tuta absoluta ambae anadhibika vizuri kwa indoxacarb, emamectin benzoate, acetamiprid n.k, cha muhimu ni kuhakikisha mmea umetunzwa vizuri na unamajani ya kutosha. Hii ni kwa kuwa ni rahisi kumdhibiti akiwa kwenye majani kuliko akianza kutoboa matunda.
Ahsante mkuu, tilio zuri sana hili. Endelea kutugea madini ya ukweli sisi wakulima chipukizi
 
Sawa mkuu nmekuelewa. Shamba likishachanganya nitakua sikauki shambani, sahizi shughuli bado hazijakomaa kwahiyo naenda mara moja moja lakin niseme tu kua nipo karibu sana na shamba
Nakuomba uanze kuwepo shamba kuanzia siku ya kuweka mbegu kwenye kitalu na siku za kupandikiza, na kila siku kukagua afya ya mimea kwenye magonjwa na mahitaji ya mbolea.
Kwenda shamba kwa wiki mara moja au mbili tu utarudi hapa kuniambia nilikuwa sahihi.

Hakikisha unajua vipimo vyote vya matuta au vitalu, kati ya shina na shina, aina bora za mbegu na ukanunue mwenyewe, pia uhakikishe zinamwagwa zile ulizonunua, kifupi uwepo kila hatua.

Siwezi kuandika mambo unayoweza kutendewa kwa uzembe wa msimamizi, shamba boy, mshirika wako au kupigwa ni mengi sana kwa namna tofauti, siwezi kuandika hapa nitakuchosha.
Hao watu wa shamba wote wanafanana mizengwe yao karibu mikoa yote Tanzania, trust me.
 
Nakuomba uanze kuwepo shamba kuanzia siku ya kuweka mbegu kwenye kitalu na siku za kupandikiza, na kila siku kukagua afya ya mimea kwenye magonjwa na mahitaji ya mbolea.

Kwenda shamba kwa wiki mara moja au mbili tu utarudi hapa kuniambia nilikuwa sahihi.
Na mimi namsihi azingatie sana hiki ulichokiandika.
 
Ukianza kupanda mbegu sio sahihi, au vipimo sio sahihi au umwagiliaji sio sahihi lazima mavuno yatakuwa sio sahihi.
Kitu kidogo tu kisipofanyika kwa tofauti ya saa 24 tu unaweza kukuta nyanya zimelala kifo cha huzuni, au zimeliwa na wadudu zote.
 
Hivi kwa nyanya dawa za wadudu ni zipi

Sent using Jamii Forums mobile app
Inategemeana na aina ya wadudu lakini kwa ujumla dawa hizo ni kama wilcron, dudumectin super, belt, cutter, liberate n.k., hizi zinaua jamii nyingi za viwavi jeshi ikiwemo 'kantangaze' tuta absoluta. Jambo la muhimu ni kuangalia dawa hiyo ina kiambata gani ambacho ndio dawa. Kunaweza kuwa na brands tofauti madukani ila zote zinakiambata kimoja.
 
Mnamo mwezi wa 12/2018 na Januari 2019 niliingia kwenye kilimo cha Nyanya. Nikiri kua nilikua sina maarifa wala uzoefu wowote kweny kilimo cha nyanya. Kuna rafiki yangu mmoja ndo alinishauri na kunishawishi kuingia kwenye kilimo cha nyanya(alinichukua na kunitembeza kweny mashamba ya nyanya na niliona jinsi watu walivyofanikiwa kupitia kilimo cha nyanya) hivyo nilishawishika vilivyo

Tulikubaliana tulime shamba la pamoja kwa kushirikiana na kushare gharama sawa kwa sawa. Tulikodi shamba na tukalima kwa trekta, baada ya wiki moja tu tangu kulima uyu rafiki yangu akapata kazi nyingne mkoa mwingine. Hivyo nikabaki peke yangu nikilisimamia shamba. Nilienda vijijini nikatafuta vijana wa kazi nikawapeleka shamba shughuli iliendelea. Hapa nikiri kua gharama zote za shamba nilitoa mim uyu rafiki yangu ni kama alinisusia shamba(kumbuka tulilima shamba kubwa kama hekari 1.25 ivi kwa minajili ya kushare gharama)
Kufupisha stori
Katika kilimo hiki nyanya zilipofikia hatua ya kukomaa ziliingiliwa na ugonjwa wa wadudu na mnyauko hivyo mwisho wa siku sikuvuna hata ndoo moja ya nyanya. Pia vijana waliokua wanahudumia shamba wamenifelisha kwa kiasi kikubwa
Nilivopiga hesabu nilikua nimetumia zaidi ya Milioni 2 lakini sikuvuna kitu

Sijakata tamaa
Mwaka huu 2020 nimerudi tena kweny kilimo cha nyanya, saizi nna maarifa na uzoefu kidgo pia nmemtafuta mwenyej mzoefu nashirikiana nae, mim natoa gajarama yeye katoa shamba na nguvukazi yake. Kama mambo yakienda vizuri nategemea mwezi wa 4 nyanya zitakua tayari
Tukutane mwezi wa 4 kwa ajili ya mrejesho wa mavuno
Kila la kheri!
 
Hivi kwa nyanya dawa za wadudu ni zipi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mnamo mwezi wa 12/2018 na Januari 2019 niliingia kwenye kilimo cha Nyanya. Nikiri kua nilikua sina maarifa wala uzoefu wowote kweny kilimo cha nyanya. Kuna rafiki yangu mmoja ndo alinishauri na kunishawishi kuingia kwenye kilimo cha nyanya(alinichukua na kunitembeza kweny mashamba ya nyanya na niliona jinsi watu walivyofanikiwa kupitia kilimo cha nyanya) hivyo nilishawishika vilivyo

Tulikubaliana tulime shamba la pamoja kwa kushirikiana na kushare gharama sawa kwa sawa. Tulikodi shamba na tukalima kwa trekta, baada ya wiki moja tu tangu kulima uyu rafiki yangu akapata kazi nyingne mkoa mwingine. Hivyo nikabaki peke yangu nikilisimamia shamba. Nilienda vijijini nikatafuta vijana wa kazi nikawapeleka shamba shughuli iliendelea. Hapa nikiri kua gharama zote za shamba nilitoa mim uyu rafiki yangu ni kama alinisusia shamba(kumbuka tulilima shamba kubwa kama hekari 1.25 ivi kwa minajili ya kushare gharama)
Kufupisha stori
Katika kilimo hiki nyanya zilipofikia hatua ya kukomaa ziliingiliwa na ugonjwa wa wadudu na mnyauko hivyo mwisho wa siku sikuvuna hata ndoo moja ya nyanya. Pia vijana waliokua wanahudumia shamba wamenifelisha kwa kiasi kikubwa
Nilivopiga hesabu nilikua nimetumia zaidi ya Milioni 2 lakini sikuvuna kitu

Sijakata tamaa
Mwaka huu 2020 nimerudi tena kweny kilimo cha nyanya, saizi nna maarifa na uzoefu kidgo pia nmemtafuta mwenyej mzoefu nashirikiana nae, mim natoa gajarama yeye katoa shamba na nguvukazi yake. Kama mambo yakienda vizuri nategemea mwezi wa 4 nyanya zitakua tayari
Tukutane mwezi wa 4 kwa ajili ya mrejesho wa mavuno
Nenda google... Seaech "kilimotajirimaarifa"...tafuta namba zake ana pdf anauza za mazao kama nyanya, kabeji etc!!

Ukizisoma slzitakusaidia sana.

Pia humu jf yupo japo sijaona sana nyuzi zake kama zamani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom