Narudi tena kwenye Kilimo cha Nyanya. Mniombee

Narudi tena kwenye Kilimo cha Nyanya. Mniombee

Kwanza hela 1.25 ya nyanya kulimwa kwa sh 2 ni kujitakia kufeli tu.


Eka 1 ya nyanya andaa 1.5 Hadi million 2 ukitaka kulimwa nyanya na nyanya ikupe faida kweli otherwise achana na nyanya utadondokea pia Mara ya pili.


Nyanya sio zao la kukimbilia kbs inabidi uwe mwamba kweli kweli
Je unaweza ukapata mavuno/faida kiasi gani?
 
Nakuomba uanze kuwepo shamba kuanzia siku ya kuweka mbegu kwenye kitalu na siku za kupandikiza, na kila siku kukagua afya ya mimea kwenye magonjwa na mahitaji ya mbolea.
Kwenda shamba kwa wiki mara moja au mbili tu utarudi hapa kuniambia nilikuwa sahihi.

Hakikisha unajua vipimo vyote vya matuta au vitalu, kati ya shina na shina, aina bora za mbegu na ukanunue mwenyewe, pia uhakikishe zinamwagwa zile ulizonunua, kifupi uwepo kila hatua.

Siwezi kuandika mambo unayoweza kutendewa kwa uzembe wa msimamizi, shamba boy, mshirika wako au kupigwa ni mengi sana kwa namna tofauti, siwezi kuandika hapa nitakuchosha.
Hao watu wa shamba wote wanafanana mizengwe yao karibu mikoa yote Tanzania, trust me.
Mkuu nimeipta hii kwangu ni elimu kubwa sana
 
Je unaweza ukapata mavuno/faida kiasi gani?

Kwa eka moja nyanya ya kisasa ni tenga 700-1200 ,tenga za debe tatu.

Ukipata kuanzi 800-1000 tunasema ulihudumia vizuri

Ukipata 1000 kuendelea tunasema mbegu ni bora na shamba lako linarutuba sana ,matunzo mazuri
 
Je unahitaji kulima mahindi na hauna muda wa kusimamia? Au unataka upate mavuno mengi zaidi? Njoo ofisini kwetu.

Ofisi ya YAD yenye wataalamu wabobezi wa kilimo sasa inakuletea mpango wa kusimamia shughuli zote za shambani. Mkulima utatukabidhi shughuli zako pale shambani kwako sisi tutafanya kila kitu kwa utaalamu zaidi na kukukabidhi mazao yako yakiwa yamekomaa. Gharama zetu ni nafuu sana na tunakuhakikishia kwa ekari moja kuvuna mahindi zaidi ya gunia 30. Usihangaike sasa, sisi tupo kwa ajili yako, Kwa Wale ambao hawana mashamba tutakuwezesha kupata mashamba ya kukodi kwa elfu 40 tu na mashamba ya kununua kwa elfu 60 tu hata ukihitaji ekari 100 za kununua utazipata kwa bei hiyo hiyo.

Kwa maelezo zaidi fika ofisini kwetu.
Jengo la NSSF SONGEA
Ghorofa ya 3 chumba no. 317
Simu. 0621133117
 
Mnamo mwezi wa 12/2018 na Januari 2019 niliingia kwenye kilimo cha Nyanya. Nikiri kua nilikua sina maarifa wala uzoefu wowote kweny kilimo cha nyanya. Kuna rafiki yangu mmoja ndo alinishauri na kunishawishi kuingia kwenye kilimo cha nyanya(alinichukua na kunitembeza kweny mashamba ya nyanya na niliona jinsi watu walivyofanikiwa kupitia kilimo cha nyanya) hivyo nilishawishika vilivyo

Tulikubaliana tulime shamba la pamoja kwa kushirikiana na kushare gharama sawa kwa sawa. Tulikodi shamba na tukalima kwa trekta, baada ya wiki moja tu tangu kulima uyu rafiki yangu akapata kazi nyingne mkoa mwingine. Hivyo nikabaki peke yangu nikilisimamia shamba.

Nilienda vijijini nikatafuta vijana wa kazi nikawapeleka shamba shughuli iliendelea. Hapa nikiri kua gharama zote za shamba nilitoa mim uyu rafiki yangu ni kama alinisusia shamba(kumbuka tulilima shamba kubwa kama hekari 1.25 ivi kwa minajili ya kushare gharama)

Kufupisha stori
Katika kilimo hiki nyanya zilipofikia hatua ya kukomaa ziliingiliwa na ugonjwa wa wadudu na mnyauko hivyo mwisho wa siku sikuvuna hata ndoo moja ya nyanya. Pia vijana waliokua wanahudumia shamba wamenifelisha kwa kiasi kikubwa
Nilivopiga hesabu nilikua nimetumia zaidi ya Milioni 2 lakini sikuvuna kitu

Sijakata tamaa
Mwaka huu 2020 nimerudi tena kweny kilimo cha nyanya, saizi nna maarifa na uzoefu kidgo pia nmemtafuta mwenyej mzoefu nashirikiana nae, mim natoa gajarama yeye katoa shamba na nguvukazi yake. Kama mambo yakienda vizuri nategemea mwezi wa 4 nyanya zitakua tayari
Tukutane mwezi wa 4 kwa ajili ya mrejesho wa mavuno
Mkuu mrejesho wako hatujaupata tafadhali
 
Mnamo mwezi wa 12/2018 na Januari 2019 niliingia kwenye kilimo cha Nyanya. Nikiri kua nilikua sina maarifa wala uzoefu wowote kweny kilimo cha nyanya. Kuna rafiki yangu mmoja ndo alinishauri na kunishawishi kuingia kwenye kilimo cha nyanya(alinichukua na kunitembeza kweny mashamba ya nyanya na niliona jinsi watu walivyofanikiwa kupitia kilimo cha nyanya) hivyo nilishawishika vilivyo

Tulikubaliana tulime shamba la pamoja kwa kushirikiana na kushare gharama sawa kwa sawa. Tulikodi shamba na tukalima kwa trekta, baada ya wiki moja tu tangu kulima uyu rafiki yangu akapata kazi nyingne mkoa mwingine. Hivyo nikabaki peke yangu nikilisimamia shamba.

Nilienda vijijini nikatafuta vijana wa kazi nikawapeleka shamba shughuli iliendelea. Hapa nikiri kua gharama zote za shamba nilitoa mim uyu rafiki yangu ni kama alinisusia shamba(kumbuka tulilima shamba kubwa kama hekari 1.25 ivi kwa minajili ya kushare gharama)

Kufupisha stori
Katika kilimo hiki nyanya zilipofikia hatua ya kukomaa ziliingiliwa na ugonjwa wa wadudu na mnyauko hivyo mwisho wa siku sikuvuna hata ndoo moja ya nyanya. Pia vijana waliokua wanahudumia shamba wamenifelisha kwa kiasi kikubwa
Nilivopiga hesabu nilikua nimetumia zaidi ya Milioni 2 lakini sikuvuna kitu

Sijakata tamaa
Mwaka huu 2020 nimerudi tena kweny kilimo cha nyanya, saizi nna maarifa na uzoefu kidgo pia nmemtafuta mwenyej mzoefu nashirikiana nae, mim natoa gajarama yeye katoa shamba na nguvukazi yake. Kama mambo yakienda vizuri nategemea mwezi wa 4 nyanya zitakua tayari
Tukutane mwezi wa 4 kwa ajili ya mrejesho wa mavuno
Mkuu mwezi wa nne ndio huu tupe mrejesho😅
 
Katika kilimo hiki nyanya zilipofikia hatua ya kukomaa ziliingiliwa na ugonjwa wa wadudu na mnyauko hivyo mwisho wa siku sikuvuna hata ndoo moja ya nyanya.
Nimejaribu kufuatilia mno kiini cha ugonjwa huu ni kipi maana kinaathiri si nyanya tu bali mazao mengi - jibu ni kwamba ugonjwa hauna dawa maalum unachoshauriwa ni ku-treate ardhi yako vizuri na kupata mbegu bora.
 
Back
Top Bottom