Narudi zangu kijijini, maisha ya mjini siyataki tena

Narudi zangu kijijini, maisha ya mjini siyataki tena

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Nimeamua nikazeekee kijijini kwa sababu zifuatazo:-​
  • Kule kijijini nitapata hewa safi isiyokuwa na mchafuko​
  • Kule kijijini nitapata majirani wema wasiokuwa na choyo​
  • Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana bila chuki​
  • Kule kijijini tutakuwa tunakunywa togwa pamoja​
  • Kule kijijini tutapunguza msongo wa mawazo​
  • Kule kijijini tutaingia shamba lolote kuchuma matunda na kula​
  • Kule kijijini tutakuwa tunasikia milio ya ndege na viumbe mbali mbali​
  • Kule kijijini tutafurahia uoto wa asili​
  • Kule kijijini tutakuwa tunaenda kuwinda kama sehemu ya michezo​
  • Kule kijijini tutapata marafiki wengi ambao sio wanafiki​
  • Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana panapotokea mmoja wetu anaumwa.​
  • Kukaa kwenye nyumba ya nyasi yenye hewa safi na ya kuvutia​
  • Kula vyakula vilivyopikiwa kwenye vyungu na kuwa na ladha nzuri​
  • Kendwa kuogelea mitoni na kuvua samaki kama sehemu ya michezo na uwindaji​
Kwa ujumla maisha ya kijijini yatakuwa ni mazuri sana

kijiji.jpg


Kwa nyie mnaobaki mjini, nawaachia mpambane na:-​
  • Majungu na fitina zenu​
  • Mchafuko wa hali ya hewa​
  • Jua kali​
  • Msongamano wa watu​
  • Makelele ya baa na kumbi za starehe zinazoharibu utulivu wa ubongo​
  • Misongo ya mawazo kutokana na changamoto za kimazingira​
  • Kudharauliwa na vijana​
  • Kununua kila kitu; nyanya, yai ,mchicha n.k​
  • Kutokuwa na marafiki wa kweli​
  • Kila mmoja kumuona mwenzie fursa​
  • Kuzeeka kabla ya umri wako​
  • Kupata magonjwa ya moyo na presha n.k​
  • Kula vyakula vyenye kemikali katika kukuzia au usindikaji​
town.jpg


Fanya maamuzi mapema; njoo kijijini tukawinde kanga pori, sungura, n.k pamoja na kuongeza miaka mingi ya kuishi.
 
Nimeamua nikazeekee kijijini kwa sababu zifuatazo:-​
  • Kule kijijini nitapata hewa safi isiyokuwa na mchafuko​
  • Kule kijijini nitapata majirani wema wasiokuwa na choyo​
  • Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana bila chuki​
  • Kule kijijini tutakuwa tunakunywa togwa pamoja​
  • Kule kijijini tutapunguza msongo wa mawazo​
  • Kule kijijini tutaingia shamba lolote kuchuma matunda na kula​
  • Kule kijijini tutakuwa tunasikia milio ya ndege na viumbe mbali mbali​
  • Kule kijijini tutafurahia uoto wa asili​
  • Kule kijijini tutakuwa tunaenda kuwinda kama sehemu ya michezo​
  • Kule kijijini tutapata marafiki wengi ambao sio wanafiki​
  • Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana panapotokea mmoja wetu anaumwa.​
  • Kukaa kwenye nyumba ya nyasi yenye hewa safi na ya kuvutia​
  • Kula vyakula vilivyopikiwa kwenye vyungu na kuwa na ladha nzuri​
  • Kendwa kuogelea mitoni na kuvua samaki kama sehemu ya michezo na uwindaji​
Kwa ujumla maisha ya kijijini yatakuwa ni mazuri sana

View attachment 3121969

Kwa nyie mnaobaki mjini, nawaachia mpambane na:-​
  • Majungu na fitina zenu​
  • Mchafuko wa hali ya hewa​
  • Jua kali​
  • Msongamano wa watu​
  • Makelele ya baa na kumbi za starehe zinazoharibu utulivu wa ubongo​
  • Misongo ya mawazo kutokana na changamoto za kimazingira​
  • Kudharauliwa na vijana​
  • Kununua kila kitu; nyanya, yai ,mchicha n.k​
  • Kutokuwa na marafiki wa kweli​
  • Kila mmoja kumuona mwenzie fursa​
  • Kuzeeka kabla ya umri wako​
  • Kupata magonjwa ya moyo na presha n.k​
  • Kula vyakula vyenye kemikali katika kukuzia au usindikaji​
View attachment 3121971

Fanya maamuzi mapema; njoo kijijini tukawinde kanga pori, sungura, n.k pamoja na kuongeza miaka mingi ya kuishi.
Kjjn raha, burudani & mustarehe
 
Na simu uiache mjini kama unataka kufaidi maisha vizuri
Yaani ukitaka kuongea na mtu unamfuata huko aliko ndio maisha hayo
Tangulia nakuja
Kweli mkuu, simu ni kisababishi namba moja kilichosababisha kupungua kwa upendo katika jamii; imeondoa ile dhana ya kutembeleana na kusaidiana.​
 
Mkuu nami plan zangu mwakani ni kwenda kuanzisha maisha Tukuyu!

Mji wa Dar es salaam umenikinai na sidhani tena napaswa kuishi hapa!,Zamani tulishindwa kukaa vijijini kwasababu hakukuwa na miundo mbinu Bora,Maji,Umeme na Hospitali nzuri!

Lakini hivi Sasa hata Wilayani huko Kuna maisha mazuri sana na watu Wana enjoy maisha kuliko tunaong'ang'ania hapa mjini!

Mungu akinipa Uhai mwakani nauhama huu mji rasmi!,Nipo kwenye mchakato wa kuuza Nyumba zangu Ili nikajenge huko Tukuyu Nika- enjoy maisha mazuri yenye Hali nzuri ya hewani!
 
Back
Top Bottom