Nelson Kileo
JF-Expert Member
- Oct 29, 2011
- 3,053
- 3,259
1.Kama sikosei Kanzu ni Vazi linalotumiwa na saana na dini ya Kiislamu,japo hata wakristo hutumia lakini si kwa kiwango kikubwa.
Nikizungumzia Upande wa Dini yako yaani "Muslim" Vazi hilo kidogo nyie mmefika nalo mbali na kulichulia ni Sehemu ya ibada na kwa desturi yake linahitaji heshima kwa yeyote yule atakaye livaava.
2.Kwa muumini wa Dini yako si sahihi kutumia au kujihusisha na Pombe/kilevi.
Kwenye Picha panaonekana jamii za Pombe mbalimbali.
3.Kwa mujibua wa Location kwnye hiyo picha nadhani kilikua ni kipindi cha EATV,Friday Night Live kwa kifupi "FNL" kinachorushwa Ijumaa .Siku hii ni siku ya maalumu ya Ibada kwa Dini ya Kiislamu.
Kwa mambo hayo Matatu umeonekana kuidharau na kuidhalilisha Dini yako.
Hayo yanaweza kua ni maoni ya wengi pamoja na mm , lakini pia nitabaki nikijikosoa kama ni sahihi saana kumjaji mtu kutokana na mavazi pamoja na kumtolea hukumu ilhali wengi wetu si wakamilifu. !
Ila pia naweza kua sahihi kukushauri hili, ukiwa kama kioo cha jamii huna budi kua makini na matendo yako kwa lolote unalolifanya hususani linapofika swala nyeti linalogusa Jamii moja kwa moja.
Ushauri pia kwa EATV. Picha hii mmeitumia nyie kwnye page yenu FB basi inawapasa Mue makini kuchagua picha za kutumia ,palikua hapan ulazima wa kutumia picha hiyo.
Ahsante