"Naseeb" Diamond Platnumz, kwa hili umeionyesha kuudharau dini yako "Islam""

"Naseeb" Diamond Platnumz, kwa hili umeionyesha kuudharau dini yako "Islam""

Status
Not open for further replies.
ni vazi km mengine sio dini
Kanzu ni Vazi kama Vazi lingine . !Vaa kanzu nenda Zanzibar tafuta Bar ya Karibu Kam,uagize na Castle Lager Baridi.
Ukifanikiwa kurudi Uje utueleze Kanzu ni Vazi la Kawaida ama lah.
 
View attachment 416520

1.Kama sikosei Kanzu ni Vazi linalotumiwa na saana na dini ya Kiislamu,japo hata wakristo hutumia lakini si kwa kiwango kikubwa.
Nikizungumzia Upande wa Dini yako yaani "Muslim" Vazi hilo kidogo nyie mmefika nalo mbali na kulichulia ni Sehemu ya ibada na kwa desturi yake linahitaji heshima kwa yeyote yule atakaye livaava.

2.Kwa muumini wa Dini yako si sahihi kutumia au kujihusisha na Pombe/kilevi.
Kwenye Picha panaonekana jamii za Pombe mbalimbali.

3.Kwa mujibua wa Location kwnye hiyo picha nadhani kilikua ni kipindi cha EATV,Friday Night Live kwa kifupi "FNL" kinachorushwa Ijumaa .Siku hii ni siku ya maalumu ya Ibada kwa Dini ya Kiislamu.

Kwa mambo hayo Matatu umeonekana kuidharau na kuidhalilisha Dini yako.

Hayo yanaweza kua ni maoni ya wengi pamoja na mm , lakini pia nitabaki nikijikosoa kama ni sahihi saana kumjaji mtu kutokana na mavazi pamoja na kumtolea hukumu ilhali wengi wetu si wakamilifu. !
Ila pia naweza kua sahihi kukushauri hili, ukiwa kama kioo cha jamii huna budi kua makini na matendo yako kwa lolote unalolifanya hususani linapofika swala nyeti linalogusa Jamii moja kwa moja.

Ushauri pia kwa EATV. Picha hii mmeitumia nyie kwnye page yenu FB basi inawapasa Mue makini kuchagua picha za kutumia ,palikua hapan ulazima wa kutumia picha hiyo.

Ahsante

Hapo kwenye wekundu, binadamu tupo tofauti kimtazamo hata kimuonekano, Je! Yeye Nasibu analichukuliaje vazi hilo au anamtazamo upi kwa vazi hilo?
 
kwani picha yenyewe imechukukiuliwa akiwa anajipa haya mabia ama yupo kazini na bahati mtangazaji kakutana naye mazingira haya wakafanya mahojiano mambo mengine hata mungu mwenyewe anaangalia kazi ya hyu ina changamoto nyingi
 
Hapo kwenye wekundu, binadamu tupo tofauti kimtazamo hata kimuonekano, Je! Yeye Nasibu analichukuliaje vazi hilo au anamtazamo upi kwa vazi hilo?
Excttly na ndio.Maana hata Mwishoni nikasema maweza nikawa nakosea Kujaji,lakini.pia anapaswa kua makini na Reaction za Jamii kutokana na matokeo ya kile anachoweza kukufanya,ukizingatia tayari ni mtu mwenye Influence.
 
Af kingine we chokoraa mtoa thread acha kufatilia dini za wenzako nyie mbona dini yenu wasichana wanaingia kanisani na vimini mbona hatusemi??
 
Dini zimeletwa tu hizi..
Kwa nini tutoane macho sababu ya dini...?
Avae kanzu disco sawaa..
Avae rozali kilabuni sawaa...
Mwisho wa maisha kila mja na fungu lake...
 
Kitimoto pekee ndiyo waislamu wote huwa hawataki kuhusishwa nayo lakini hayo mengine naona wanayachukulia poa tu.

Muislamu hata akengeuke vipi lazima ajifiche ndiyo ale kitimoto.
 
Kuna tofauti ya islam na arab culture. Kanzu ni nguo na utamaduni wa waarabu hata kabla uislamu haujaja.
Avae tu vasi sio dini
 
Kufuata maadili ya Uandishi ,nadhani Chombo cha habari ni vyema makini katika matumizi ya picha zisiweza leta karaha kwa jamii na ndio.maana hata kipindi hicho huonyeshwa usiku ili kukwepa baadhi ya Jamii ikiwamo watoto.
Sidhani kama Nasibu kwa siku hiyo alikua na picha moja tu .
Kwa point yako hii ina maana hata kwenye tv basi hizo pombe hazikutakiwa kuonekana eti kisa diamond kavaa kanzu.. Kitu ambacho ni impossible. Kama unafuatilia mpira, kuna team kibao zina wachezaji waislam na bado wanavaa jezi zinazotangaza pombe. Sasa hao nao utasingizia maadili ya vyombo vya habari? FNL kuoneshwa usiku sio sababu ya hizo picha za pombe.
 
Excttly na ndio.Maana hata Mwishoni nikasema maweza nikawa nakosea Kujaji,lakini.pia anapaswa kua makini na Reaction za Jamii kutokana na matokeo ya kile anachoweza kukufanya,ukizingatia tayari ni mtu mwenye Influence.
Ni kwli kabisa!! huenda yeye anamisingi yake.."Who knows?🙄"
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom