Nashauri iwe lazima vyombo vyote vya moto viwe na kiboksi cha huduma ya kwanza chenye gloves ili kurahisisha msaada kwa majeruhi

Nashauri iwe lazima vyombo vyote vya moto viwe na kiboksi cha huduma ya kwanza chenye gloves ili kurahisisha msaada kwa majeruhi

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Habari wadau!
Ushauri wangu kuna watu wanaweza kuupuuza! Lakini itakuwa na maana tukijadili humu kwa pamoja!

Hakuna aliyesalama hata ukijihesabia haki kwa utajili/cheo na Mali ulizo Nazo.
Huko barabarani hata viongozi hupatwa ajali, hata matajili hupatwa ajali, wachungaji hupatwa ajali n.k
HIVYO KUPEWA MSAADA NA JAMII NI LAZIMA
usalama wetu upo mikononi kwa wenzetu!

Jeshi la polisi kitengo cha trafiki kwa kushauriana na wizara ya afya!
Waweke ulazima wa kila chombo cha moto kitumiacho barabara kuwa na kiboksi kidogo chenye GLOVES na nylon nyembamba!

Hili litasaidia sana wananchi kutoa msaada wa haraka kwa majeruhi punde ajali inapotokea kwa kutokuogopa damu za majeruhi.

Majeruhi wa ajali wamekua wakikosa misaada kwa wakati kutokana na watu kuogopa kushika damu!
Hata wenye magari ya kujitolea wengi huhofia magari yao kuchafuka kwa kuwa hakuna kapeti laini la kutanguliza ili kumlaza majeruhi

Haya ndiyo mambo ya msingi sana kwa trafiki kukagua kila chombo kuliko hata stika ya nenda kwa usalama!

Viwembe, spirit I au painkiller vinaweza kuhitaji muda lakini majeruhi hahitaji muda kupelekwa hospital!
Wizara ya afya pia inaweza kuliboresha zaidi hili kwa kuwatambua watu waliojitolea vyombo vyao vya moto kubeba majeruhi!.
Wanaweza kutoa hata motisha hati ya utambuzi ili mtu huyo imfae kupewa punguzo la bei endapo siku akihitaji huduma kwenye hospital!

Hospital iondoe dalili za usumbufu wowote unaoweza kukatisha moyo wa kujitolea n.k

Kila mtumia barabara ni mhanga! Hili linatakiwa lisimamiwe kikamilifu na jeshi la polisi barabarani ili kurahisisha wahanga kupata huduma!
Ajali inapotokea pikipiki, magari wakitoa gloves na kapeti msaada utapatikana haraka kuliko sasa watu hutegeana! Au mpaka wamjue kwanza majeruhi ndipo hujitolea!

Pia traffic wa eneo au njia husika wawe wa kwanza kufika kwenye tukio na wakichelewa wawajibishwe! Haiwezekani penye dili wawahi lakini kwenye tukio wachelewe! Mali za majeruhi zikipotea walipishwe trafiki wa eneo hilo ili kuwawajibisha!
 
Mbona vipo ni vile tuu wanaweka huko viberiti ugoro na vichungi vya sigara wakati mwingine maganda ya ndizi kabisa
 
Mbona vipo ni vile tuu wanaweka huko viberiti ugoro na vichungi vya sigara wakati mwingine maganda ya ndizi kabisa
Hakuna gloves kabisa huduma kwa majeruhi zimekuwa zikichelewa
 
Nafikiri ni takwa kisheria kuwa vyombo vya moto kuwa na kiboksi cha huduma ya kwanza sema ufatiliaji ndiyo shida japo huko nyuma miaka kama ya 2014 walikuwa wanakagua kabisa, sina uhakika kwenye bodaboda.
 
Nafikiri ni takwa kisheria kuwa vyombo vya moto kuwa na kiboksi cha huduma ya kwanza sema ufatiliaji ndiyo shida japo huko nyuma miaka kama ya 2014 walikuwa wanakagua kabisa, sina uhakika kwenye bodaboda.
Kuna ajali nyingi sana watu wanarundikana lakini hakuna hatammoja mwenye gloves!

Watangaze operesheni hiyo kila baada ya miezi mitatu pasipo kuchoka
 
Shida ya watu wengi ni kutokuguswa na jambo kama hajaona ndugu yake kafikwa na jambo
 
Nasikitika hii thread ni ya maana sana lakini kama kawaida ya vitu vya msingi tunapuuza na vya kipuuzi tunavikuza, daaah Tanzania hii sijui tutabadilika lini hii mitazamo.

Mleta mada dmkali mie nipo pamoja nawe kwenye hili sisi tuongeze gloves kwenye vyombo vyetu na ata nylon nyepesi tuwe nazo, nilishawahi kukuta hali kama hii kwenye gari fulan hilux watu wameshindwa kutoa msaada kisa hawana gloves nashukuru nilikuwa nazo pea 4 tukaingia kazini na kufanya mawasiliano na wahusika kupitia simu za wahanga maana zilikuwa zimepigwa ikawa ni rahisi ofisi husika kupata taarifa..R.I.P kwa watu wale huwa sisahau lile tukio na kunikumbusha mwendo sahihi na kutokuwa na papara niwapo barabarani.
 
Nasikitika hii thread ni ya maana sana lakini kama kawaida ya vitu vya msingi tunapuuza na vya kipuuzi tunavikuza, daaah Tanzania hii sijui tutabadilika lini hii mitazamo.

Mleta mada dmkali mie nipo pamoja nawe kwenye hili sisi tuongeze gloves kwenye vyombo vyetu na ata nylon nyepesi tuwe nazo, nilishawahi kukuta hali kama hii kwenye gari fulan hilux watu wameshindwa kutoa msaada kisa hawana gloves nashukuru nilikuwa nazo pea 4 tukaingia kazini na kufanya mawasiliano na wahusika kupitia simu za wahanga maana zilikuwa zimepigwa ikawa ni rahisi ofisi husika kupata taarifa..R.I.P kwa watu wale huwa sisahau lile tukio na kunikumbusha mwendo sahihi na kutokuwa na papara niwapo barabarani.
Kuna watu huwacheka nyumbu wanavyoshindwa kusaidiana!
Lakini hata binadam kuna wakati hatueleweki kama tunajitambua!
Hatujui kutambua usalama wa wenzetu upo mikononi mwetu!

Ajali zinatweza utu wa watu wengi! Watu hutegeana kutoa misaada kwasababu hawana protection ya mikono
 
Kuna watu huwacheka nyumbu wanavyoshindwa kusaidiana!
Lakini hata binadam kuna wakati hatueleweki kama tunajitambua!
Hatujui kutambua usalama wa wenzetu upo mikononi mwetu!

Ajali zinatweza utu wa watu wengi! Watu hutegeana kutoa misaada kwasababu hawana protection ya mikono
Tena huenda nyumbu wananafuu kwa sababu ni wanyama, binadamu tunepewa utashi kama huu wa kuwa na tahahari na kujua ni nini tunapaswa kufanya endapo tunakutana na janga kama hilo.

Badala yake tumegeuka wapiga picha na video wa kujitegemea pasipokutoa msaada husika kwa wahanga.
 
Tena huenda nyumbu wananafuu kwa sababu ni wanyama, binadamu tunepewa utashi kama huu wa kuwa na tahahari na kujua ni nini tunapaswa kufanya endapo tunakutana na janga kama hilo.

Badala yake tumegeuka wapiga picha na video wa kujitegemea pasipokutoa msaada husika kwa wahanga.
Halafu wakiona mtu akiwa uchi ndo wanageuza story lakini mambo ya msingi watu tunageuka vipofu kama hayatuhusu
 
Back
Top Bottom